Norway: Mauzo ya magari ya umeme yapiku yale yatumiayo petroli na dizeli

Kwani mkuu ukitaka kuingiza hapa nchini gari la umeme unakatazwa?
Hajaongelea kukatazwa kuingiza gari za umeme nchini.

Ameongelea kuwa hakuna sheria inayohusiana na gari za umeme Tanzania.

Mfano:Norway,Denmark,Sweden gari zote zinazotumia umeme kodi zake ziko chini, nk.

Mapunguzo ya kodi imewafanya watu wanunue hizo gari zinazotumia umeme kwa wingi.
 
Dewij alikua anawapa ujumbe waliomtea kuwa bado ana mkwanja hata kama walimtoa upepo wa kutosha.... Mumbuoa hii ilitangazwa wiki chache baada ya tukio la kutekwa
Yaani kama alifanya hivyo basi nae ni mtoto bado.

Hio Tesla model 3 aliyonunua ndio the cheapest model kwny Tesla,ikigharimu kati ya $40,000-60,000 ikitegemea kama ni base model au full loaded,sasa pesa kama hio ataikosaje aiseeeee.
 
Hajaongelea kukatazwa kuingiza gari za umeme nchini

Ameongelea kuwa hakuna sheria inayohusiana na gari za umeme Tanzania

Mfano:Norway,Denmark,Sweden gari zote zinazotumia umeme kodi zake ziko chini, nk.

Mapunguzo ya kodi imewafanya watu wanunue hizo gari za zinazotumia umeme kwa wingi
Wenzetu hata hybrid cars walipewa mpk Tax credit ya $7,500,sisi huku hata habari hatuna aiseee.
 
MO Dewji aliagiza Tesla Model 3 ila sijui iliishia wapi.
Hivi aliagiza au alionekana analitembelea akiwa USA!? Unadhani akiendaga USA MO anafikia hotel sio? Huyo ni wa huko pia so labda hilo gari anatembeleaga akiwa zake huko huko alikosomea.
 
Kama una mafua na hujachimba, baada ya miaka 10 yatakosa market nzuri.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
NDIO. halitambuliki kama chombo cha usafiri kinachoweza kusajiriwa na TRA kwa sheria za nchi yetu. labda upate special clearance. sasa kama una mpango wa kuagiza tesla hakikisha hunaga presha, mana hakatok bandarin!
Uongo narabarani mbona z iko.pikipiki kibao zinatumia umeme na -zimesajiliwa?
 
Nilikua na mpango wa kununua kituo cha mafuta yaani petrol station ila
NIMEAKHIRISHA
Mkuu nunua usisikilize maneno ya mtandaoni.

Hizo gari za umeme huku zitaenea Sana miaka 20+ ijayo wajukuu zako ndio watazikuta. Sisi kwenye uzuiaji uchafuzi hali ya hewa kutokana na magari tunakubali mpaka gari zenye Euro Emmision Regulation 1( Euro 1). Mabasi ya mchina na Maroli yake yana Euro 3.

Wazungu sasa wapo Euro 6 na bado wanakaza masharti ili gari kukidhi vigezo. Hata Serikali na pesa zake hawaagizi Electric Vehicles ni mwendo wa V8.

Sisi uchafuzi kwetu bado siyo ishu NEMC wenyewe wanatumia gari za mafuta V8 na Nissan Patrol unadhani wameahindwa kununua Nissan Leaf au Tesla model 3 Kwa pesa ya V8 moja.
 
Mkuu nunua usisikilize maneno ya mtandaoni.

Hizo gari za umeme huku zitaenea Sana miaka 20+ ijayo wajukuu zako ndio watazikuta. Sisi kwenye uzuiaji uchafuzi hali ya hewa kutokana na magari tunakubali mpaka gari zenye Euro Emmision Regulation 1( Euro 1). Mabasi ya mchina na Maroli yake yana Euro 3.

Wazungu sasa wapo Euro 6 na bado wanakaza masharti ili gari kukidhi vigezo. Hata Serikali na pesa zake hawaagizi Electric Vehicles ni mwendo wa V8.

Sisi uchafuzi kwetu bado siyo ishu NEMC wenyewe wanatumia gari za mafuta V8 na Nissan Patrol unadhani wameahindwa kununua Nissan Leaf au Tesla model 3 Kwa pesa ya V8 moja.
Mbona dar Kuna gari za umeme nimeshaanza kuziona.

Endelea kujidanganya
 
Mbona dar Kuna gari za umeme nimeshaanza kuziona.

Endelea kujidanganya
Dar gari za umeme nyingi ni hizo Nissan Leaf. Na ambazo nyingi wanazo kampuni ya kukodi magari inaitwa Xcar wapo pembeni ya Shoppers Mikocheni.

Toyota Prius chache watu ndio walinunua Electric Vehicle, zaidi ya hapo zimejaa Hybrid Electric Car kama Harrier, Crown, Prius, Honda na Mazda.
 
Duh kama nawaona waarabu wanavohaha dunia ikiachana na mafuta sijui watatuuzia tigo?
 
Tanzania hata sheria haijabadilishwa kuruhusu magari ya umeme kutambulika nchini. Hata kwenye calculator ya TRA option haimo. nadhan tunaisubiri mitumba ya ulaya ya petrol na diesel. range rover, bently, merc, vw, bmw, n.k watutupie!
Yes; will take sometimes at least mitumba ikianza kutoka 5 year or so to come ndio muswada upelekwe Bungeni. By then TRA itakuwa imepata picha kamili ya kodi mbalimbali na uchakavu unaotakiwa kutozwa ili kufikia lengo 3 tr.
 
... waarabu wame-invest sana kwenye sekta nyingine zaidi ya miaka 20 iliyopita. Walishaliona hilo.
Hata kama. Watayumba sana. Sema dunia bado inahitaji mafuta kwa miaka mingi mbele hasa diesel na mafuta mazito kwa mitambo. labda petrol ndo itapungua uzalishaj. Nadhan hata kwa ncho km Tz inayotegemea sekta ya mafuta kwa kodi na vyanzo ambata haijapenda sn tuondoke humo. Vita ni kali sana hii kiuchumi
 
Back
Top Bottom