Bullava
JF-Expert Member
- Dec 28, 2014
- 618
- 999
Habari JF members!!
Balozi wa North Korea nchini Hispania KIM HYOK - CHOL amewakaribisha watu /watalii toka sehemu mbalimbali za dunia kwenda kuitembelea North Korea ili kujionea mambo mbalimbali na kueleza kuwa waombaji wa Visa watapatiwa chini ya mwezi mmoja tangu tarehe ya kuomba, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na gazeti la EL Pais jijini Madrid siku ya Alhamisi wiki hii. Balozi KIM HYOK - CHOL alivilaumu vyombo vya habari vya magharibi kwa kupotosha ukweli kuhusu nchi yao kwa kuandika mambo mabaya yenye kuichafua nchi yao.
Source : RT news
Hapa JF kumekuwa na mada nyingi kuiponda North Korea kuwa kuna shida, njaa na maisha magumu kwa ujumla wake. Nadhani hii ni fursa sasa kwa wale waliokuwa wanatamani kwenda kumuona Mapanki Mzee wa Kiduku uwanja ni wenu wakuu. Mkirudi mtuletee mrejesho wa hali ya huko
Balozi wa North Korea nchini Hispania KIM HYOK - CHOL amewakaribisha watu /watalii toka sehemu mbalimbali za dunia kwenda kuitembelea North Korea ili kujionea mambo mbalimbali na kueleza kuwa waombaji wa Visa watapatiwa chini ya mwezi mmoja tangu tarehe ya kuomba, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na gazeti la EL Pais jijini Madrid siku ya Alhamisi wiki hii. Balozi KIM HYOK - CHOL alivilaumu vyombo vya habari vya magharibi kwa kupotosha ukweli kuhusu nchi yao kwa kuandika mambo mabaya yenye kuichafua nchi yao.
Source : RT news
Hapa JF kumekuwa na mada nyingi kuiponda North Korea kuwa kuna shida, njaa na maisha magumu kwa ujumla wake. Nadhani hii ni fursa sasa kwa wale waliokuwa wanatamani kwenda kumuona Mapanki Mzee wa Kiduku uwanja ni wenu wakuu. Mkirudi mtuletee mrejesho wa hali ya huko