North Korea yalaani jaribio la Marekani, yasema ni matayarisho ya vita vya nuclear

ze kokuyo

JF-Expert Member
Jan 24, 2014
7,142
9,114
26a110c8c0e91242158cc77dd1a85875.jpg


Korea ya kaskazin imesema kwamba jaribio la hivi karibuni la udunguzi wa kombora la masafa marefu(ICBM) lililofanywa na Marekani ni hatua ya hatari ambayo inaleta chokochoko za kijeshi.
Pia imeeleza kwamba jaribio hilo linaonyesha kwamba matayarisho ya vita vya nuclear yapo kwenye hatua za mwisho kwa upande wa Marekani. Na kuendelea kwa kuionya Marekani kwamba isidhani inaweza kuhimili mashambulizi yao(Nkorea) na kwamba Marekani haiwez kushinda vita hivyo kwa kua itageuzwa kua majivu.

Kauli hiyo tata inafuatia baada ya marumbano na vitisho vya muda mrefu kati ya Marekani na korea kaskazini kuhusiana na mpango wa nyuklia wa Korea kaskazini.

Hapo awali, Rais wa Marekani Donald Trump alituma meli kubwa ya kubeba ndege(aircraft carrier) 'armada' kwenye pwani ya Korea ambapo Jeshi la korea kaskazini lilitisha kuizamisha meli hiyo na pia kushambulia ngome za jeshi zilizopo Japan na Korea kusini.

Vyanzo mbalimbali vinaeleza kwamba mfumo huo uliotumiwa na Marekani (Ground Based MidCourse Defense System) kudungua kombora hilo ulianza kufanya kazi mwaka 2005.Ulibuniwa kwa ajili ya kudungua makombora ya masafa marefu(ICBM).Pia una uwezo wa kudungua kombora likiwa hata nje ya dunia (exosphere).

f18ce21731d18ab7b3fca4e2c70c704a.jpg


Kwa sasa mifumo hiyo kama 30 imefungwa Alaska na California kulinda Marekani dhidi ya shambulizi lolote huku mingine 15 ikitarajiwa kumalizika 2017.

 
Duu nimeamini sisi tulikuja kusindikiza duniani haiwezekan wenzetu wako mbali sisi ndio tuko kweny uhakiki wa vyeti.
Cjui tulikosea wapi bora tufe wotd uumbaji uanze upya pengine tunaweza jikuta na sis tumekuwa wa israel
Bora ndugu unanisaidia kufikiri kama mm,
Mm huwa najiuliza nakosa mjibu, wetu weusi mungu alichanganya material gani mpaka sikawa nzito kiasi hicho,
Hata miarabu mijingajinga tu imetuzdi ubunifu, hiv tuliumbwaje et? Au tuanzishe mradi Wa kutwangana makonzi kuchemsha akili!!!
 
Bora ndugu unanisaidia kufikiri kama mm,
Mm huwa najiuliza nakosa mjibu, wetu weusi mungu alichanganya material gani mpaka sikawa nzito kiasi hicho,
Hata miarabu mijingajinga tu imetuzdi ubunifu, hiv tuliumbwaje et? Au tuanzishe mradi Wa kutwangana makonzi kuchemsha akili!!!
Kwani hujui giza ni jeusi. Kwahiyo tafsiri ya mtu mweusi ni giza. Ndo maana wenyewe walisema wamegundua bara la giza/dark continent. Usiwaze sana kula ulale
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom