North Korea imetengeneza mvua kupitia roketi na mizinga iliyobebeshwa kemikali maalumu ili kupambana na ukame

Sikirimimimasikini

JF-Expert Member
Dec 27, 2019
2,919
15,604
Baada ya North Korea kuwa na changamoto ya ukame kwa muda mrefu, hatimae wamefanikiwa kutengeneza mvua (artificial rain).

Utafiti huo ambao kwa mara ya mwanzo uliripotiwa mwaka 2017 ambapo Chuo Kikuu Cha Kim-Il Sung nchini humo, kiliamua kutengeneza roketi na mizinga maalumu ya kuibusha (induce) mvua. Silaha hizo (maroketi na mizinga) walizibebesha kemikali ya Silver Iodide na dry Ice kisha kuzivurumisha kwenda tabakahewa (artmosphere). Kemikali hizo hubadili kiwango cha unyevunyevu ktk tabakahewa, kufanya mawingu mvua, kisha mvua kumwagika ardhini.

Teknolojia hiyo itabadili mabadiliko hatarishi ya hali ya hewa na hivyo kuepusha ukame, kuhakikisha upatikanaji wa maji ya kutosha (mvua) na ya uhakika kwa ajili ya matumizi ya kilimo na ufuaji umeme.

Halafu utasikia Wamarekani wa Nanyamba wakiibeza North Korea ktk maendeleo ya sayansi na teknolojia!

Source: Fox News
======
Screenshot_2020-05-06-00-07-24-1.png

Screenshot_2020-05-05-23-22-16-1.png

Screenshot_2020-05-05-23-17-00-1.png

Screenshot_2020-05-05-23-17-00-2.png

Screenshot_2020-05-05-23-16-05-1-1.png
 
Halafu utasikia Wamarekani wa Nanyamba wakiibeza North Korea ktk maendeleo ya sayansi na teknolojia!
Mkuu hiyo ni teknolojia rahisi sana, tena hauhitaji maroketi kusambaza hiyo chemical angani.

Iran ilishafanya hii kazi tangu miaka ya 1970 na kitu nahisi 1975, nimesahau tarehe kamili nilisoma kwenye kitabu flani miaka mingi iliyopita wakati nataka kufanya Final year school project ya Form Six ilihusu mambo ya uharibifu wa mazingira chini ya usimamizi wa Mwalimu wangu mmarekani Jack Ashcroft.

Kwa waliosoma shule ile maarufu alikozikwa Balozi jasusi majuzi watakuwa wanamjua huyu mwalimu wa mradi wa Peace Corps kama walisoma enzi hizo za akina mwalimu Dale Larson (Mzee wa Ma-Calculus ya Pure Math, the basket baller) na Miss Allison King.

Pia miaka ya karibuni Mzee Pinda akiwa PM alienda Asia nadhani Indonesia, Thailand au Malaysia au Vietnum akaomba msaa wa TZ tuje tufundishwe hii teknolojia kwa vitendo, hiyo enzi za mkwere mwamba wa mjini.
 
Mkuu hiyo ni teknolojia rahisi sana, tena hauhitaji maroketi kusambaza hiyo chemical angani...
Mkuu, teknolojia zote huwa ni rahisi mno ukisoma theory kwenye makaratasi (vitabu) ila ukija kwenye real life applications ndio utaelewa kwa nini kuna nchi zilizo mbele kiteknolojia na zingine ziko nyuma kiteknolojia. Uzuri umetaja mfano mmoja wa nchi ambayo iliomba kufundishwa na nchi nyingine namna ya kutengeneza mvua. Kama ingekuwa rahisi kama ulivyodai, hiyo nchi (iliyoomba) kwa nini ilishindwa kutumia na mpaka leo haijatumia wanasayansi wake (maprofesa na madokta (PhD) kedekede ilionao) watengeneze hiyo mvua? Au hakuna mikoa yenye ukame nchini?

Toka A level wasomi wetu hufundishwa kurusha satellite angani na kuitia kwenye parking orbit, wakakokotoa tungamo, mchepuko na sampuli mbalimbali za speed zinazohusika. Wakakokotoa maswali kedekede, mepesi na mazito zaidi, kwenye vitabu laini (mfano Nelcon) na pia vigumu zaidi (kama vile University Physics, UP), watu wakapata A kwenye mitihani mbalimbali kuonesha walielewa somo vema. Wengine wakaendelea na taaluma hizo vyuo vikuu. Lakini umewahi kusikia nchi kama nchi imerusha satellite angani? Au wadhani hatuhitajii nasi kuwa na satellite yetu huko juu?

North Korea kutumia makombora na mizinga yake ni katika upekee wake wa kufanya kile ambacho yenyewe yaona ndio bora zaidi. Ukisoma theory, sio lazima ukopi na kupaste kama ilivyo, unapaswa nawe uchangie knowledge fulani ktk jambo hilo.
 
Mkuu hiyo ni teknolojia rahisi sana, tena hauhitaji maroketi kusambaza hiyo chemical angani.
Iran ilishafanya hii kazi tangu miaka ya 1970 na kitu nahisi 1975, nimesahau tarehe kamili nilisoma kwenye kitabu flani miaka mingi iliyopita wakati nataka kufanya Final year school project ya Form Six ilihusu mambo ya uharibifu wa mazingira chini ya usimamizi wa Mwalimu wangu mmarekani Jack Ashcroft.

Kwa waliosoma shule ile maarufu alikozikwa Balozi jasusi majuzi watakuwa wanamjua huyu mwalimu wa mradi wa Peace Corps kama walisoma enzi hizo za akina mwalimu Dale Larson (Mzee wa Ma-Calculus ya Pure Math, the basket baller) na Miss Allison King.

Pia miaka ya karibuni Mzee Pinda akiwa PM alienda Asia nadhani Indonesia, Thailand au Malaysia au Vietnum akaomba msaa wa TZ tuje tufundishwe hii teknolojia kwa vitendo, hiyo enzi za mkwere mwamba wa mjini.
Alikua ni Waziri Mkuu Mstaafu Edward Ngoyayi Lowassa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, teknolojia zote huwa ni rahisi mno ukisoma theory kwenye makaratasi (vitabu) ila ukija kwenye real life applications ndio utaelewa kwa nini kuna nchi zilizo mbele kiteknolojia na zingine ziko nyuma kiteknolojia. Uzuri umetaja mfano mmoja wa nchi ambayo iliomba kufundishwa na nchi nyingine namna ya kutengeneza mvua. Kama ingekuwa rahisi kama ulivyodai, hiyo nchi (iliyoomba) kwa nini ilishindwa kutumia na mpaka leo haijatumia wanasayansi wake (maprofesa na madokta (PhD) kedekede ilionao) watengeneze hiyo mvua? Au hakuna mikoa yenye ukame nchini?
Mkuu yaani hiyo hapa bongo haijafanyika siyo kwamba wasomi wetu hawawezi bali ni gharama na hatujapata ukame mkubwa kiasi cha kutulazimisha kutengeneza mvua.

Nchi nyingi sana duniani ikiwemo Iran wanatumia ndege tu kusambaza hiyo silver iodide wakati wa cloud seeding.

Wala hizo PR za kwenye media za serikali mbalimbali duniani zisikutishe ukadhani hiyo ni sayansi ngumu,kwa hakika hata wewe unaweza kufanya kama ukipewa chemical na usafiri wa kusambazia hewani.

Hao akina Mzee Pinda, Membe na boss wao walikuwa wanaenda kupiga misele tu huko duniani na wengine kwenda kubembea kwenye cable transport kwa Hayati Bob Marley. Wakirudi ndiyo wanakuja na mbwembwe nyingi za ku-justify safari zao na jinsi walivyotumia pesa zetu walipa kodi.
 
Yale mastori kuhusu gharika yalivyoharibu bongo za wabongo sijui wafuasi wa stori hizo wata-react vipi
Zina uhusiano gani na hii habari ni vitu viwili tofauti tupende kujikita kwenye mada, Kila mtu anauhuru wa kuamin kile anachoona ni sawa as long sio kikwazo kwake
 
Zina uhusiano gani na hii habari ni vitu viwili tofauti tupende kujikita kwenye mada, Kila mtu anauhuru wa kuamin kile anachoona ni sawa as long sio kikwazo kwake
We ndo unayetoka kwenye mada, chunguza vizuri ulichokiandika
 
Mkuu hiyo ni teknolojia rahisi sana, tena hauhitaji maroketi kusambaza hiyo chemical angani.

Iran ilishafanya hii kazi tangu miaka ya 1970 na kitu nahisi 1975, nimesahau tarehe kamili nilisoma kwenye kitabu flani miaka mingi iliyopita wakati nataka kufanya Final year school project ya Form Six ilihusu mambo ya uharibifu wa mazingira chini ya usimamizi wa Mwalimu wangu mmarekani Jack Ashcroft.

Kwa waliosoma shule ile maarufu alikozikwa Balozi jasusi majuzi watakuwa wanamjua huyu mwalimu wa mradi wa Peace Corps kama walisoma enzi hizo za akina mwalimu Dale Larson (Mzee wa Ma-Calculus ya Pure Math, the basket baller) na Miss Allison King.

Pia miaka ya karibuni Mzee Pinda akiwa PM alienda Asia nadhani Indonesia, Thailand au Malaysia au Vietnum akaomba msaa wa TZ tuje tufundishwe hii teknolojia kwa vitendo, hiyo enzi za mkwere mwamba wa mjini.
Habari yako haijakaa sawa sana.
Kwanza umerahisisha mno hiyo technolojia, na pili umedanganya kuwa Mzee Pinda alihusika kwenda Malasyia kwa issue ya mvua . Ukweli alikuwa ni Mzee Lowasa.
 
Habari yako haijakaa sawa sana.
Kwanza umerahisisha mno hiyo technolojia, na pili umedanganya kuwa Mzee Pinda alihusika kwenda Malasyia kwa issue ya mvua . Ukweli alikuwa ni Mzee Lowasa.
Could be either one of them but that does not change the fact that our former Prime Minister went to Asian country and asked for the assistance.
Tusijichojua ni details za makubalino ya kile alicho omba, hatujui aliomba pesa, au chemicals, au wataalam au vifaa kama ndege za kuja kufanya hiyo kazi hapo hatujui.

Unafikiri kama hiyo teknolojia ingekuwa lazima itumie rockets hiyo nchi ingeweza kuja kutusaidia mamilioni ya dola za kutengeneza launchpad ya rockets, kisha rockets zenyewe wakati nchi husika haina hiyo teknolojia aghali ya rockets?

Au haujui Morocco, Mali, na Senegal wanafanya hiyo Cloud seeding miaka mingi tu?
Ni kwamba hizo nchi za Africa wanatofautiana sana kwa teknolojia na Tanzania?

Hiyo teknolojia ya kutengeneza mvua ni rahisi sana lakini ni aghali (expensive), tena kwa kutumia hata ndege ndogo tu za kupulizia dawa mashambani kama Cesna 210 au za kuulia nzige na wadudu wengine inaweza kwenda kusambaza hizo chemical anga la eneo husika na mvua ikanyesha. Hakuna ulazima wa kuvumbua kemikali au formula za michanganyiko yake wakati tayari zipo, why reinvent the wheel if you want to make a car? Just use available tech, we could buy the already made chemical composition or buy the formula of the composition.
Hizo Cesna 210 ni ndege ndogo sana ambazo zinafanana na zile wanazo miliki vikampuni vidogo hapa Tanzania hasa Zanzibar au kule Arusha na Kilimanjaro vinatumika na wazungu kwenye utalii na mashamba ya ngano na shairi ya wazungu na watanzania wenye asili ya Asia.
Nenda pale Arusha Airport ya Kisongo pale karibu na Magereza ya Kisongo Arusha au nenda Zazibar vipo hivyo vindege.

Unakuwa haujui jinsi awamu zilizopita zilivyo kuwa za kipigaji? Kitu kinakuuzwa kisha watu wa ugavi na wakubwa zao wanafanya yao na 10%.

North Korea labda alitaka kusambaza mvua sehemu kubwa sana ndiyo maana alitumia njia aghali ya maroketi. Hata hivyo jamaa kwa maroketi kila kitu kama vichaa.
Au umesahau jina la utani la Kim alilopewa na Trump la "The Rocket Boy"?
That is just an overkill!!
Hiyo ni kama una muuwa swala na RPG au na bomu wakati ungeweza kumuuwa kwa shortgun tu!!
 
India nao wanatumia roketi badala ya ndege ktk kutengeneza mvua kupitia cloud seeding. Halafu mmarekani mmoja wa Nanyamba abeza North Korea kutumia roketi! Eti kwa kuwa tu alikosoma theory kwenye vitabu alikaririshwa njia ya kutumia ndege tu.

Screenshot_2020-05-06-19-29-25-1.png

Screenshot_2020-05-06-19-28-53-1.png

Screenshot_2020-05-06-19-32-06-1.png

Screenshot_2020-05-06-19-30-42-1.png
 
Back
Top Bottom