No Entry signs Posta mpya

Mlachake

JF-Expert Member
Oct 13, 2009
4,412
4,558
Jamani weekend hii nimepita posta nimeteseka sana.

Unakuta bara bara ina alama ya no Entry unakoingilia na unakotokea kuna no Entry pia.

Hebu mamlaka husika tuelewesheni.

what are you Up to guys????????????????
 
Pole sana.
Huo ulikuwa ni mpango kazi wa kuneemesha matumbo ya watu.
Vibao vile vimewekwa kama mapambo tu
 
Inakera sana. Hata mie imenitokea mara kadhaa, hasa katikati ya jiji.
 
Hili ndo tatizo,
Kuna NO ENTRY zinazotumika na zisizotumika.
Cha ajabu huwezi kujua zipi zatumika na zipi hazitumiki, labda uwe alwatan sana mitaa ile!!
 
Walivifunika na magazeti ikija mvua yanaachia walivyo na akili fupi. Vinachanganya kinoma
 
sio posta tu bali mjini kote kuna no entry kwenye barabara ambazo zinapitika hata sielewi hua wanamaanisha nini...hapo watu washakula hela zao lazima
 
Barabara ya morogoro inapoanzia pale boma kunakibao kinaonyesha usipinde kulia wakati magari yote yanatoka posta ya zamani sasa sijui pale walikuwa wanamaanisha nini!!
 
barabara ipi mkuu?. mia

Nakumbuka baadhi: Mkwepu kuingia Samora,na kuingia Sokoine Drive, Moro road kuingia Samora, kuna kabarabara fulani pia kanaconnect Samora kanatokezea Kivukoni front. Kote ama kuna no entry au vibao viwili!
 
Nakumbuka baadhi: Mkwepu kuingia Samora,na kuingia Sokoine Drive, Moro road kuingia Samora, kuna kabarabara fulani pia kanaconnect Samora kanatokezea Kivukoni front. Kote ama kuna no entry au vibao viwili!
mkuu mtaa wa samora unaingiza magari hayatoki. morogoro road inaingiza na kutoa. mkwepu inatoa, pamba road inaingiza na kutoa, uhio road inaingiza na kutoa, ile barabara iliyopo mambo ya ndani inaingiza na kutoa, sokoine drive inatoa tu. barabara ipi imezibwa kote?. mia
 
Barabara inayopita nje ya SOUTHERN SUN HOTEL ina vibao vinavyokataza kuelekea Ohio Street kama umetokea baharini, lakini magari yanapita.
 
Kulikua na mpango wa kubadili matumizi ya barabara, sasa kuna wakawahi kuweka vibao vikiwa vimefunikwa.....ni muda mrefu umepita, nadhani zaidi ya mwaka.
hawa halmashauri ya jiji ni wapuuzi kweli.
 
haswa hiyo samora ndio inachanganya kweli, kuanzia mnara wa askari hadi shaban robert. Na Sokoine drive kuanzia posta ya baharini hadi stesheni. Kama mtu ni mgeni huwezi kuendesha gari mjini kati, tunaendeshea uzoefu tu.
 
Kwani wakati walifunika na Magazeti wakawa wanasema wanasubiri uzinduzi, sasa sijui uzinduzi umeisha wapi badala yake watu wamejifunulia wenyewe. Shida ni kwamba hujui no entry ipi inatumia na ipi haitumiki. Nawaonea huruma sana wageni na wala wanafuata sheria za usalama barabarani hasa katikati ya jiji.
 
Kulikua na mpango wa kubadili matumizi ya barabara, sasa kuna wakawahi kuweka vibao vikiwa vimefunikwa.....ni muda mrefu umepita, nadhani zaidi ya mwaka.
hawa halmashauri ya jiji ni wapuuzi kweli.

Mkuu, issue ni deal tu....kwani vile vituo vya mabasi yaendayo kasi vilivyojengwa fasta fasta vitatumika? Barabara inapita kwingine, vituo vipo kwingine
 
mkuu mtaa wa samora unaingiza magari hayatoki. morogoro road inaingiza na kutoa. mkwepu inatoa, pamba road inaingiza na kutoa, uhio road inaingiza na kutoa, ile barabara iliyopo mambo ya ndani inaingiza na kutoa, sokoine drive inatoa tu. barabara ipi imezibwa kote?. mia

Mkuu, have you been down town recently?

Jiji walikula tenda ya kuweka vibao vya no entry almost kila barabara.
Nafikiri i uzembe wetu tu, tulitakiwa kununa spray colours na kuvifuta vyote.
 
Mkuu, have you been down town recently?Jiji walikula tenda ya kuweka vibao vya no entry almost kila barabara.Nafikiri i uzembe wetu tu, tulitakiwa kununa spray colours na kuvifuta vyote.
hizo ndo akili za rukuvi. ulikua mpango wa kupunguza foleni. sio mjini tu. mwenge to moroco na airport to banana barabara ina njia tatu. je mgeni wa dar atajua apite wapi? pembeni au katikati. sehemu nyingine barabara zinafungwa na kuruhusu za upande mmoja kila nusu saa. mia
 
hizo ndo akili za rukuvi. ulikua mpango wa kupunguza foleni. sio mjini tu. mwenge to moroco na airport to banana barabara ina njia tatu. je mgeni wa dar atajua apite wapi? pembeni au katikati. sehemu nyingine barabara zinafungwa na kuruhusu za upande mmoja kila nusu saa. mia
Ile ya banana to airpot ina vibao vinavyoonesha muda ambao unaweza kutumia njia mbili..vibao vipo mwanzo kabisa kwa kila upande
 
Back
Top Bottom