nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Wednesday, 13 April 2011 20:53
Midraji Ibrahim na Joyce Mmasi, Dodoma
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, amesema watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho, wanapaswa kusahau uwezekano wa wao kujipanga na kusimamisha hatua zilizoanza kuchukuliwa.Nnauye alisema chama kitashinda vita ya ufisadi na kwamba, kama kuna watu wanajifanganya kuwa wanaweza kufifisha moto uliowashwa, wajaribu.
Akizungumza mjini Dodoma jana, Nnauye alisema kilichofanywa na Halmashauri Kuu ya CCM, ni mwanzo wa mapambano ya kufagia mafisadi ndani ya chama hicho kinachotawala."Chama kitashinda vita hivyo, kama kuna watu wanafikiri wanaweza kujaribu, Tumeanza tutamaliza,"alisema.
Kuhusu madai kwamba tamko kuhusu watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kupewa siku 90 kujiuzulu Nec alilotoa na Naibu Katibu Mkuu CCM Bara, John Chiligati, lilikuwa lao na kwamba si la Nec, alisema maamuzi yote ya kikao yapo kwenye maandishi."Maamuzi yako kimaandishi si yangu, yanasema wajiuzulu wenyewe wasipofanya hivyo chama kitawawajibisha chenyewe," alisisitiza Nnauye.
Akitoa tamko hilo juzi usiku baada ya kumalizika kwa kikao cha Nec, Chiligati alisema "wenyewe wapime na kuchukua hatua za kuwajibika ndani ya chama kama tulivyokubalina hapa ndani, wasipofanya hivyo katika kipindi cha miezi mitatu, chama hakitasita kufanya hivyo kwa niaba yao."
"Hata kama hatuna ushahidi, hisia tu kutoka kwa wananchi zitoshe kuwafanya wajipime wao wenyewe, na kama kuna hoja ya kuonewa kwa nini usemwe wewe tu." alisema.
Nnauye aliwataka wanachama waliokimbia kwa hasira, kurejea CCM kwa sababu walichotaka kimefanyika na kwamba, tayari ana maombi mengi ya wanafunzi na wanachama kutaka kurejea.Kuhusu muda wa kufanya marekebisho kwenye chama ngazi zote, Nnauye alisema mpango wa kazi upo na utatekelezwa kwa hatua."Hata unapoanza kuoga huanzi mwili mzima, unakwenda hatua kwa hatua. Mpango kazi upo utatekelezwa," alisema.
Alisema kufuatia uamuzi wa Nec, baadhi ya wanachama wameomba kukutana na sekretarieti na kwamba, itaongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM bara, Pius Msekwa.Nnauye alisema ziara ya kukutana na wanachama hao ilianza jana mjini Dodoma na leo, itaendelea mkaoni Morogoro.
Kwa mujibu wa Katibu huyo, Aprili 16, mwaka huu, sekretarieti itakutana na wanachama wa Chalinze, Kibaha na Dar es Salaam na kabla ya kwenda Zanzibar, Aprili 17 mwaka huu.
Midraji Ibrahim na Joyce Mmasi, Dodoma
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, amesema watuhumiwa wa ufisadi ndani ya chama hicho, wanapaswa kusahau uwezekano wa wao kujipanga na kusimamisha hatua zilizoanza kuchukuliwa.Nnauye alisema chama kitashinda vita ya ufisadi na kwamba, kama kuna watu wanajifanganya kuwa wanaweza kufifisha moto uliowashwa, wajaribu.
Akizungumza mjini Dodoma jana, Nnauye alisema kilichofanywa na Halmashauri Kuu ya CCM, ni mwanzo wa mapambano ya kufagia mafisadi ndani ya chama hicho kinachotawala."Chama kitashinda vita hivyo, kama kuna watu wanafikiri wanaweza kujaribu, Tumeanza tutamaliza,"alisema.
Kuhusu madai kwamba tamko kuhusu watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kupewa siku 90 kujiuzulu Nec alilotoa na Naibu Katibu Mkuu CCM Bara, John Chiligati, lilikuwa lao na kwamba si la Nec, alisema maamuzi yote ya kikao yapo kwenye maandishi."Maamuzi yako kimaandishi si yangu, yanasema wajiuzulu wenyewe wasipofanya hivyo chama kitawawajibisha chenyewe," alisisitiza Nnauye.
Akitoa tamko hilo juzi usiku baada ya kumalizika kwa kikao cha Nec, Chiligati alisema "wenyewe wapime na kuchukua hatua za kuwajibika ndani ya chama kama tulivyokubalina hapa ndani, wasipofanya hivyo katika kipindi cha miezi mitatu, chama hakitasita kufanya hivyo kwa niaba yao."
"Hata kama hatuna ushahidi, hisia tu kutoka kwa wananchi zitoshe kuwafanya wajipime wao wenyewe, na kama kuna hoja ya kuonewa kwa nini usemwe wewe tu." alisema.
Nnauye aliwataka wanachama waliokimbia kwa hasira, kurejea CCM kwa sababu walichotaka kimefanyika na kwamba, tayari ana maombi mengi ya wanafunzi na wanachama kutaka kurejea.Kuhusu muda wa kufanya marekebisho kwenye chama ngazi zote, Nnauye alisema mpango wa kazi upo na utatekelezwa kwa hatua."Hata unapoanza kuoga huanzi mwili mzima, unakwenda hatua kwa hatua. Mpango kazi upo utatekelezwa," alisema.
Alisema kufuatia uamuzi wa Nec, baadhi ya wanachama wameomba kukutana na sekretarieti na kwamba, itaongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM bara, Pius Msekwa.Nnauye alisema ziara ya kukutana na wanachama hao ilianza jana mjini Dodoma na leo, itaendelea mkaoni Morogoro.
Kwa mujibu wa Katibu huyo, Aprili 16, mwaka huu, sekretarieti itakutana na wanachama wa Chalinze, Kibaha na Dar es Salaam na kabla ya kwenda Zanzibar, Aprili 17 mwaka huu.