NMB wamekataa kupokea taarifa ya kuzuia miamala baada ya kadi ya benk kuibiwa matokeo yake wahalifu wamefanikiwa kutoa pesa

Anold

JF-Expert Member
Jul 15, 2010
1,456
614
Nimesikitishwa sana na uzembe ambao Maofisa wa NMB- BANK HOUSE wameufanya na kusababisha wezi waliopora begi la kijana wangu pamoja na kadi ya Bank ya NMB wapate mwanya wa kuiba hela kwa kupitia kwenye ATM. Tukio lenyewe ni kuwa jana tarehe 27/02/2020 muda wa asubuhi kijana wangu aliporwa begi ambalo ndani yake kulikuwa na simu pamoja na kadi ya Bank.

Hivyo baada ya kunijulisha uporaji huo mara moja niliwasiliana na mtu ambaye alikuwa karibu na tawi la Bank ya NMB ili aweze kutoa taarifa za awali ili kuzuia wahalifu hao wasiweze kutumia hiyo kadi hiyo. Nilimpata mtu na kaenda moja kwa moja mpaka NMB bank house ambapo alikutana na maofisa ambao mmoja wao alikuwa tayari kusaidia, hata hivyo wakati anaendelea kujaribu kuzuia miamala isifanyike inasemekana alitokea afisa mwingine wa bank na kumueleza Afisa aliyekuwa anaendelea na zoezi la kufunga miamala kuwa hairuhusiwi mtu mwingine kutoa taarifa Bank ya kufunga miamalla isipokuwa mhusika mwenyewe hivyo ikaelekezwa kuwa lazima mwenyewe akatoe taarifa. Jambo hili limesababisha uzembe mkubwa kwani wezi hao wameweza kutoa hela bila wasiwasi wowote.

Nashauri uongozi wa NMB waangalie baadhi ya taratibu ambazo hazina msingi katika usalama wa hela za wateja. Hakukuwa na sababu yeyote ya kupuuza taarifa za awali ilitakiwa kukubali taarifa na kuzifanyia kazi. Hili jambo kwa kweli limenisikitisha sana maana endapo mwenye akauti yupo hospitali au amekufa n.k itakuwaje? hizi ni kanuni mbovu kwenye usalama wa fedha za watu, sasa mmekataa na pesa zimeibwa kipi bora?
 
Tuambiane kwanza NYWILA ya akaunti waliipataje hao wezi?kisha utuambie kulikuwa na ugumu gan wa huyo kijana wako kushindwa kufika kwenye tawi alilokuwa karibu nalo
Hao wezi walijuaje Password ya kijana wako?

Sent using Jamii Forums mobile app
Itakuwa labda aliziandika kwenye kikaratasi akakunja na kadi,si unajua wazee ambao umri umeenda niwasahaulifu..

Ona sasa wamekomba kapensheni kote
 
Ungefuata taratibu zao. Benki zote anayetakiwa kutoa taarifa ni mhusika mwenyewe ndio wanafunga
Unajua ni vema ukatumia akili ingalau kidogo ili kujibu, taarifa za awali ni muhimu kama uhalifu unatokea, mtu aliyetumwa kutoa taarifa alikuwa na vitambulisho, alikuwa namba za mmiliki wa kadi kikubwa ni kujiridhisha, kwa hiyo kutoa taarifa za kuzuia uhalifu usifanyike dhambi? ndiyo maana afisa wa kwanza alikubali baada ya kujua uharaka na umumu.
 
Tuambiane kwanza NYWILA ya akaunti waliipataje hao wezi?kisha utuambie kulikuwa na ugumu gan wa huyo kijana wako kushindwa kufika kwenye tawi alilokuwa karibu nalo
Nywila ilikuwa kwenye simu.
 
Unajua ni vema ukatumia akili ingalau kidogo ili kujibu, taarifa za awali ni muhimu kama uhalifu unatokea, mtu aliyetumwa kutoa taarifa alikuwa na vitambulisho, alikuwa namba za mmiliki wa kadi kikubwa ni kujiridhisha, kwa hiyo kutoa taarifa za kuzuia uhalifu usifanyike dhambi? ndiyo maana afisa wa kwanza alikubali baada ya kujua uharaka na umumu.
Nakuambia hivi kwa taratibu za benki hilo haliwezekani, huyo kwa kwanza alifanya mistake tu kukubali
 
Anold,
Yaani hao wezi wamebuni password yake kwa muda mfupi hivyo? au ndio aliiandika kwenye diary yake! Poleni, ni sahihi mwenye kadi yake ndie atoe taarifa
 
dogo kaibiwa akashindwa enda benki mwenyewe aya sawa akakupa taarifa ukashindwa mshauri akatoe taarifa benki kuzuia miamala
Aya nayo ngumu ukashindwa ww kwenda ili ufosi king

sawa ukamwambia jirani akajikongoja akaenda akapata hayo majibu, akakupa taarifa ukashindwa enda tena wala kumtuma muhusika aende unakaa kusubiri yatokee ya kutokea ulaumu

nmb walikuwa sawa ww ndo mzembe
 
Vielelezo kama Loss report au RB alikuwa navyo mtoa taarifa? Walau hata picha iliyotumwa kwa whatsapp, e mail n.k.
Mwenye nia ovu pia anaweza kuomba kufungiwa/ kuzuia miamala kwa akaunti ya mtu mwingine ilimradi tu anazo baadhi ya taarifa za anayetaka mhusika.

Pole kwa hilo. Lakini usiwahi kutoa lawama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom