Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.


Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe "Siri")
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom
Mnachelewesha uingizwaji wa hundi mfano utakuta taasisi imesambaza hundi kwa benki tofauti kwa lengo la kuwalipa watumishi, utakuta wale walio katika benki nyingine wanawahi kupata pesa lakini tulio na akaunti NMB pesa inachelewa mno kuingizwa wakati hundi zote zimepelekwa siku moja kwa wakati mmoja hilo litawakosesha wateja msipokua active hasa matawi ya mikoani na wilayani
 
Hivi nmb kwanini mnafanya kazi kizamani sana?au viongozi wa matawi yenu ni majipu yanahitaji kutumbuliwa?mtu anaeonana na wateja mara kwa mara lazima awe na afya nzuri, kwenye matawi yenu ya Posta kuna mfanyakazi wenu wa kike hayuko sawa, hembu jiangalieni, unahudumiwa na mtu hata kusema vizuri hawezi, kila wakati kama ana kitu kimemkaba mdomoni, acheni mambo yenu bana.
 
Ndugu wana JamiiForums

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.


Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe "Siri")
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom



MUUNGWANA NI VITENDO
nyie NMB mnatesa wateja wenu kwa kuwasimamisha foleni masaa mengi bila hata msaada wa viti ikumbukwe kuwa mna wateja wengi kuliko benki zingine hivyo msululu wa wateja ni mkubwa katika matawi yenu ila cha ajabu hakuna maboresho ya kuwa na hata viti na matokeo yake huduma inamchefua mteja kwakutojali kwenu.
nashauri kuwe na viti vya kutosha kwa kuwa kuna chanagamoto ya kuwahudumia wateja wenu kwa wakati.
fikiria kwa mfano nimetoka zangu vijijini nimechoka nafika benki nasimama masaa karibia manne, nachukia sana kitu hicho mbadilike.

kama hamna viti mboreshehuduma tusiwe tunakaa muda mrefu na usiozidi saa moja.
 
Kwakuwa kuboresha huduma na kuongeza kasi mmeshindwa, sasa basi tumechoka kusimama na simu tutaongea tukiwa ndani maana hatuwezi kuwekana masaa Matano tumesimama bila mawasiliano.

Au wekeni mabenchi twende mstari kwa kujivuta kama hospital
 
Naomba mnielekeze kuhusu hilo ongezeko la VAT la 18% kwa kuanzia tarehe 1/7/2016 kutokana na badiliko la sheria ya kodi kwa mfano halisi. Nitashukuru
 
Nataka nikope NMB muwe munakata marejesho tshs.185,000/= kwa mwezi nataka mda uwe miezi 60. Nitapata shilingi ngapi? Naomba hesabu yenu ili nilinganishe na bank nyingine. Nawasilisha.
 
Naona mnauliza tu bila majibu. Kwa nini msiende hukohuko mana hapa ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa. Hakuna wa kuwajibu wakuu angalieni namna nyingine
 
NMB MOBILE huduma ya kujiunga Nmb mobile inashindikana n mwenzi sasa nataka kujiunga na HUDUMA HII LAKINI NAAMBIWA HAKUNA MAWASILIANO NIMEENDA HADi nmb HOUSE BADO INASHindika
 
Kiukweli huduma zenu zinachosha sana afu watoa huduma wanajickia sana mkumbuke hii ni biashara na cku xote mteja ni mfalme na msipokuwa makini mtapoteza wateja lukuki!
 
NMB MOBILE huduma ya kujiunga Nmb mobile inashindikana n mwenzi sasa nataka kujiunga na HUDUMA HII LAKINI NAAMBIWA HAKUNA MAWASILIANO NIMEENDA HADi nmb HOUSE BADO INASHindika
Hiyo sahau ndugu
Mie nina miezi minne,sijaipata nikitaka pesa inabidi niteseke kidogo hadi wilayani kwenye ATM
Hii ni benki ya makanjanja
 
NMB Tanzania hii branch ya Kisarawe inanishangaza sana, kuna madirisha manne ya kuhudumia Ila kila siku ukifika inakera Ni dirisha moja tu likowazi mengine Ni imefungwa Kwa muda , temporarily closed.
Hii inakera.....
 
Back
Top Bottom