Nawapongeza nmb kwa huduma zenu nzuri. Ni mteja wenu kwa mikopo wa muda mrefu tangu 2004. Kuna maboresho mengi mazuri yametokea. Nawashauri mwangalie riba zenu, japo kuna udhibiti wa bot.

Kenya wamesogeza benki zao namanga mpakani. Watanzania wanavuka mpaka na kukopa, kisa riba zao ndogo.

Inaathiri uchumi, kulizuia mpira upo golini kwenu.
 
mm nina account nmb nimepitia bank statement nakatwa hela ndogondogo ya over draft na ukijumlisha unapata hela nyingi sana wakati sijawahi kuchukua OD acheni kutuuibia naona uvivu kufatilia na mpaka ss ni zaidi ya 20000 mshakata
 
Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya huduma mnazo pata kwenye matawi yetu nchini kote, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko yenu na tuna wahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi ya wafanyakazi waliotajwa na wengine wenye tabia kama hizo.

Ndugu wana jukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili moja wapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwa hakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.

Kama kutatokea umepata huduma isiyo ridhisha au ufanyaji kazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:

1. Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2. Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3. Kwa posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:

Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe "Siri")
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.

4. Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000 Tigo
0779 751 000 Zantel
0685 751 000 Airtel
0800 751 000 Vodacom
Mmepandisha riba ya mkopo (personal loan) kutoka asilimia 18 mpaka asilimia 20?

Maana leo nimeamkia nmb tawi fulani huku kanda ya ziwa na nilivyofika loan officer akaniomba salary slip na alivyocheck eligibility yangu akasema ninaweza kukopa million 10 plus kwa miezi 60 Nikamwambia mimi nataka million 10 tu kwa miaka mitano.

Akapiga hesabu akaniambia nitakuwa narejesha sh. 264,938 kwa mwezi. Nilivyopiga hesabu nikaona ni riba ya 20%. Nikaona niahirishe kwanza kuchukua huo mkopo
Swali: ni kweli mmepandisha riba?
Kwani mimi ninavyojua, million 10 kwa miezi 60 nitakuwa narejesha sh. 253,934.28 kama riba ni 18%
 
Naomba ufafanuzi,ikiwa akaunti yangu imesitishwa,na nikiwekewa pesa kutoka akaunti nyingne,je,ile pesa itaingia kwenye akaunti iliyositishwa? Kama itaingia naipataje?

Na kama haitaingia,inarudi kwenye akaunti iliyotuma? Nahitaji ufafanuzi,maana nina tatizo hilo
 
Wadau tunashukuru kwa kujibu na kutoa miongozo kwa wateja katika suala la kuboresha huduma.mimi napendekeza makao makuu macho yenu yaelekezwe mikoani pia.kuna tatizo na kero inapofikia tar za mwishoni.

ATM hazifanyi kazi.mtu anaweza kufikiri kuna hujuma zinafanyika kipindi hicho kwani unaweza panga fileni asubuhi hadi mchana na usipate huduma.kuna wafanyakazi mfano walimu na watu wa afya wanatoka mbali kusiko na huduma na mishahara inapitia NMB wanateseka kwani inabidi kulala mjini ili
wajaribu huduma siku inayofuata.

USHAURI NA MAPENDEKEZO
1;INUENI UWEZO WA MTANDAO KAMA UMBALI KUTOKA MAKAO MAKUU NDIO ISSUE.

2;TANUENI WIGO WA HUDUMA UWE
ASAMBAMBA NA ONGEZEKO LA WATEJA.NAM ZIONGEZEKE NA ZIPUNGUZE UMBALI WA WATEJA KUZIFUATA.

ASANTE.
 
NMB sasa hivi mmeishakuwa giant kwa nini ATM zenu zipo chache tena mwenye matawi yenu wekeni ATM kwenye shopping Mall, vituo vya mafuta.


Inachukuwa muda gani mteja kupata mkopo kama ana kila kitu.
 
jamani card ya bonus huu n mwezi wa 5 while nilifungua mwezi wa 9 2016,je n sawa mpaka sasa sjapata card
 
Nataka kufungua akaunti, taratibu zikoje? Majibu ya haraka tafadhali.

Pia napenda kujua makato yenu kwa mwezi na makato mbalimbali kwa huduma kama vile kutoa pesa atm, kuangalia salio, nmb mobile charges, nk.
 
NMB kwa nini mmefungia akaunti yangu bila taarifa? Yaaani mwaka huu mwanzoni nimeomba na kupatiwa kadi ya viza, nimeenda vijijini ambako huduma yenu haipo for three months, kurudi mmefunga akaunti, nauliza naambiwa sijafanya verification, why??
 
account inachukua muda gan kufungiwa Km huwek hela?
Baada ya kufungiwa unaweza kuirudisha na ina chukua muda gan mpaka zoez kukamilika?
 
Back
Top Bottom