NMB mobile jamani

Kv-london

JF-Expert Member
Jan 24, 2014
2,816
4,802
Wakuu naomba kama kuna mtu ambye anafahamu jinsi ya kujiunga na nmb mobile bila kufka katka taw lolote la nmba naomba anisadie

natanguliza shukran zangu kwenu
 
Hii huduma mbovu sana mwezi jana nilituma ela transaction ikawa aborted nikajaribu tena haikukamilika kuangalia salio nikaona kiasi kimepungua mara mbili na sikupata sms wala niliyemtumia nae..jana nikatuma ela mpaka leo hakuna ujumbe wowote unao onesha kua muamala umekamilika.
 
Wakuu naomba kama kuna mtu ambye anafahamu jinsi ya kujiunga na nmb mobile bila kufka katka taw lolote la nmba naomba anisadie

natanguliza shukran zangu kwenu

Upo serious au unatania?au una hamu ya kuibiwa hela?
 
Hiyo huduma ni lazima kwanza ukasajiliwe kwenye bank husika yaani branch ya bank husika huwezi kutumia mpaka uende bank kuomba kuunganishwa mkuu
 
Hiyo huduma ni lazima kwanza ukasajiliwe kwenye bank husika yaani branch ya bank husika huwezi kutumia mpaka uende bank kuomba kuunganishwa mkuu

Nenda kwenye ATM yoyote ya NMB iliyoko karibu na wewe ujisajiri.
 
Wakuu naomba kama kuna mtu ambye anafahamu jinsi ya kujiunga na nmb mobile bila kufka katka taw lolote la nmba naomba anisadie

natanguliza shukran zangu kwenu

Kusajili na NMB MOBILE nenda kwenye ATM yoyote ya NMB iliyoko karibu na wewe.
 
Hii huduma mbovu sana mwezi jana nilituma ela transaction ikawa aborted nikajaribu tena haikukamilika kuangalia salio nikaona kiasi kimepungua mara mbili na sikupata sms wala niliyemtumia nae..jana nikatuma ela mpaka leo hakuna ujumbe wowote unao onesha kua muamala umekamilika.

Acha kutoposha watu, hakuna huduma bora kama za NMB Mobile. Jiunge sasa kupitia ATM yoyote ya NMB iliyoko karibu na wewe.
 
Mimi nadhani #Binary ameeleza alichokutana nacho kama mteja ambacho watu wengine pia kinawatokea.. Hiz huduma za Simbanking,nmb mobile na zinginezo ni nzuri maana zinasaidia kuokoa muda kwa kufanya mihamala bila kwenda benki ila zinapaswa ziboreshwe.

Wateje warejeshewe fedha zao kwa wakati kunapotokea makato mara mbili na wapewe taatifa namna malalamiko yao yanavyoshughurikiwa... nina rafiki yangu alipata tatizo kama la ndugu #Binary (ila kwa benki nyingine) aliripoti benki tatizo lake ilimchukua mwezi mzima kulifuatilia na kupatiwa utatuzi.

La msingi kwa wadau ni kujenga utamaduni wa kuchukua bank statements kila mwezi ikiwezekana pia kwenda benki mara upatapo tatizo nao watawasiliana na wahusika maana benki zingine wame outsource hivi vitengo vya mobile banking

Pia benki kuboresha huduma zao kwa kutatua matatizo ya wateja kwa wakati.
Asante

Hii huduma mbovu sana mwezi jana nilituma ela transaction ikawa aborted nikajaribu tena haikukamilika kuangalia salio nikaona kiasi kimepungua mara mbili na sikupata sms wala niliyemtumia nae..jana nikatuma ela mpaka leo hakuna ujumbe wowote unao onesha kua muamala umekamilika.

Acha kutoposha watu, hakuna huduma bora kama za NMB Mobile. Jiunge sasa kupitia ATM yoyote ya NMB iliyoko karibu na wewe.
 
Acha kutoposha watu, hakuna huduma bora kama za NMB Mobile. Jiunge sasa kupitia ATM yoyote ya NMB iliyoko karibu na wewe.

Yawezekana huduma ni bora lakini wahudumiaji wakawa wabovu. Mimi ninatumia huduma ya NMB tawi la Ifakara, mara ya kwanza nilikuwa ninatumia huduma ya NMB mobile baadaye ikawa ina goma, nilipo fika dawati la huduma kwa wateja wakasema nijaze form ya NMB mobile kuomba nitumiwe namba , nikajaza na wakasema nitapata ujumbe jioni yake kupitia simu yangu, sasa ni mwezi wa pili sijapata ujumbe walanini. Chakushanga kila ninapo enda kuulizia ninapewa majibu tofauti, mara simu yako haina uwezo wa kupokea ujumbe, mara hudumu hii mpaka itoke makao makuu sasa hata kama inatoka makao makuu ndo ichuke miezi miwili? Haya majibu niliona yana dalili za ubabaishaji.
 
Back
Top Bottom