NMB Chalinze kumeoza, mnaohusika litazameni lile tawi

TAWA

JF-Expert Member
Jun 23, 2013
3,667
1,566
Katika pita pita zangu za kutafuta ridhiki huwa napita sana chalinze na kufanya biashara kidogo pale na wadau wangu wa eneo lile. hivyo katika muktadha huo Bank ninayoitumia ni NMB tawi la chalinze kwani ndiyo tawi la Bank pekee lililopo eneo lile ingawa pamechangamka kibiashara na uwekezaji. uendeshaji wa tawi hili la Benk ni tofauti sana na ukiukwaji mwingi wa taratibu na sheria za kibenk unaoendelea kufanyika, hizi ni baadhi ya kasoro na kero nilizojionea hapa

1. wafanya biashara wanaokuja kuweka (deposit) fedha nyingi kuchanganyika na wale wanaokuja kuweka au kutaka huduma za kawaida dirishani badala ya kwenda au kutengewa chumba maalumu yaani bulk kwa ajili ya kufanya miamala yao. hii hufanya huduma katika madirisha ya kutolea huduma kuchukua muda mrefu kwani huchukua muda mrefu kuhesabu mfano milioni kumi na tano au ishirini ambazo mtu amekuja kuweka hasa siku za jumatatu na Alhamisi, Pia kuhatarisha usalama wa huyu anyefanya miamala mara kwa mara kwani watu humkariri na hivyo kuwa hatari kwa siku za baadae.
2. usirogwe uombe bank statement, inaweza kukuchukua wastani wa saa moja au saa moja na nusu kupata bank statement hiyo. hapa nashindwa kuelewa wanakwama wapi

3. Wafanyakazi wanafanya kazi kwa kujuana sana na baadhi ya wateja. kuna wateja inafikia hatua hawapangi foleni. Akifika kwenye mlango wa bank, anapiga simu kwa mhudumu wa bank, mhudumu anajifanya kama anakwenda toilet then kama ni muamala zinachukuliwa fedha pamoja na bank paying slips zinagongwa muhuli mtamuona mwenzenu huyoo anaondoka nyie mnakodoa tu macho kwenye foleni. hii inatokea sana kati ya wahudumu na wafanya biashara wakubwa ambao wanakuja kufanya miamala mikubwa hapa kwenye tawi

4. Rushwa kwenye kitengo cha mikopo, ingawa hii inaweza kuwa ni tatizo ndani ya NMB yote lakini kwa chalinze imekithiri. kuna tatizo kubwa sana katika kitengo cha mikopo NMB chalinze, unaweza kuomba mkopo lakini mpaka kuja kuingiziwa mkopo laima umtafute "kikubwa" afisa mikopo
5. cheque transaction ndiyo "kimeo" ukideposit cheque unaweza kaa mpaka siku tatu mpaka nne cheque haijaingizwa katika account ya mteja husika. hii huwafanya wafanya biashara kugombana sana na wateja wao.

jambo la nyie NMB kumshukuru Mungu, ni kwamba katika eneo hili la Chalinze, hakuna tawi lingine la Bank nyingine, lakini kama kungekuwa hata na katawi ka bank yoyote ile, naamini hapa mngebaki na walimu na manesi tu.

niwatakie kazi njema katika ujenzi wa serikali ya viwanda
NMB Bank
close to you
 
Wahudumu wa pale ni wapuuzi. Dirisha za teller ziko zaidi ya 4 ila huwezi kukuta zote zinafanya kazi.

Pale customer care kuna mama mmoja mtu mzima huwa ana majibu ya dharau sana
 
Huu ni umbea, kukaa kidogo tu ndo umeyajua yote hayo mpaka mambo ya mikopo?

Fitina si afya!
 
Huu ni umbea, kukaa kidogo tu ndo umeyajua yote hayo mpaka mambo ya mikopo?

Fitina si afya!
Hapana, ni tawi ninalolitumia mara kwa mara ingawa mimi si mkazi wa hapa. ninaishi Mbele kidogo na hapa chalinze nina biashara zangu maeneo haya. kwa hiyo nimeanza kutumia hili tawi toka 2009 mkuu. si suala la umbea
 
Mkuu, nakupongeza kwa observation nzuri kabisa uliyoamua kuiweka hapa.

Chalinze mimi ni mpitaji tu,nikishuka ni kununua mananasi,machungwa lakini nilishapata huduma kwenye ATM zao pale. Mamba ya kadi za kisasa hizi unazama popote.

Hii inaweza peleka hata pia wakaongezewa wafanyakazi.

Lakini bado inasikitisha kuona pamoja na mabadiliko makubwa ya teknolojia hapo kwenu mmeamua kutokubadilika. Hii itaendelea kuwa gharimu hata zije benki kumi.
Hizo changamoto za hundi nazo zinabaki hapo hapo,ingawa kwa sasa matumizi yake kwa malipo ya third parties yamepungua. Serikalini hupewi tena hundi. Pia uelewa wa hizo hundi ni za wapi.

Rushwa ni jambo mtambuka,bado wanauongozi sijui kama ulijaribu kuyapeleka haya yote kwa uongozi na walilujibu nini?

Vinginevyo watanzania tunapaswa kubadilika hasa utendaji wa kazi lakini pia kupokea mabadiliko ya teknolojia.
 
YULE MAMA WATEJA WANAPOMWENDEA WANAKWENDA KWA TAHADHARI KAMA WANKWENDA CHUMBA CHA SINDANO
Niliwahi kwenda na jamangu pale kumsindikiza alisahau PIN yake ya kadi, yule mama akampa form ya kujaza wakati tunajaza akapita mlango wa uwani na kusepa zake. Tumesubiri mpaka tumechoka mama hakurudi. Ikabidi tusepe zetu.

Afu branch meneja wa pale sijui ni mchaga wa wapi, ni mlevi sana hadi anashindwa kuwasimamia wafanyakazi wa chini yake.

Yaani vi-teller vya pale vinafanya kazi kama benki ni ya hawara zao. Wana kauli mbovu, ukifika pale muda wote wanachati. Dirisha ziko zaidi ya 4 ila ukienda hata saivi utakuta moja tu ndio linafanya kazi kwa kusuasua.

Muda mwingi wako jikoni wanajitengenezea chai na kwenda kuzurura huku na huko
 
Huu ni umbea, kukaa kidogo tu ndo umeyajua yote hayo mpaka mambo ya mikopo?

Fitina si afya!
Huo siyo umbea acha kutetea Uovu kama kuna usumbufu acha waanike humu ili wamiliki wa Bank wazinduke waboreshe huduma vizuri
 
Hapana, ni tawi ninalolitumia mara kwa mara ingawa mimi si mkazi wa hapa. ninaishi Mbele kidogo na hapa chalinze nina biashara zangu maeneo haya. kwa hiyo nimeanza kutumia hili tawi toka 2009 mkuu. si suala la umbea
NMB zipo kero nyingi hususani foleni ndefu huku baadhi ya madirisha yakiwa wazi bila wahudumu, na ipo Tabia mbovu hufanywa hasa na wanawake kupanga foleni kisha anaenda kukaa kwenye viti na foleni ikikaribia kufika Dirishani anajitokeza na kujichomeka mbele kuwa alikuwepo hapo, huu ujinga haupo Bank nyingi za kijanja , cha kushangaza wazee wanakaa kwenye foleni lakini Binti mchanga anakaa kwenye viti akitegea foleni isogee.
 
YULE MAMA WATEJA WANAPOMWENDEA WANAKWENDA KWA TAHADHARI KAMA WANKWENDA CHUMBA CHA SINDANO
Kupitia JF mtambo wa kurekebisha Tabia mbovu analo la kujifunza sasa nina imani akipata taarifa akasoma maoni ya wachambuzi atazinduka haraka na kuachana ujinga wake.
 

Mkuu, ebu wasiliana nao hapo
 
Back
Top Bottom