NMB acheni mambo ya kizamani, mnapoteza wateja wengi zama hizi za ushindani

Blueface

Member
May 2, 2020
46
47
Kama kuna benki yenye kiwango cha chini kwenye ubunifu basi NMB ni moja wapo! Wakati benki zingine zikiwa zimeshaachana na lile sharti la kung'ang'ania mfanyakazi anayetaka mkopo lazima mshahara wake upitie benki yao, NMB wao ndo kwanza wanazidi kusisitiza hilo sharti kama kigezo namba moja!

Benki nyingi zilishaachana na hilo sharti baada ya kuona wanapoteza wateja wengi ambao mishahara inapitia benki nyingine. Kwa mfano CRDB, Barclays, NBC benki ya posta na benki zingine ndogo ndogo kama Bank ABC zote hizi zimeshaondoa hicho kipengele.

Ni sharti ambalo halina maana kwa sababu mshahara unalipwa kutoka hazina hivyo benki ina uhakika wa kupata makato ya mkopo wa mfanyakazi hata kama hapokelei mshahara kwao! Chondechonde NMB badilikeni mmebakia nyinyi peke yenu wenye masharti ya hovyo kama hayo!
 
Kwa hiyo kelele zote kumbe umenyimwa mkopo

Si ungeenda Headoffice ukaonana na Head of Credit
.
Na kama wamekuambia hivyo jua hiyo ni sera au policy ya Bank na imepitishwa na Board Members na sio Manager au Afisa mikopo

Halafu kumbuka wanaangalia credit worthness yako

Je wewe unastahili?Unaaminika?
 
Kuna hatari ya kumpa mkopo mtumishi ambaye mshahara wake haupitii kwako. Hata CRDB na NBC hawakupi mkopo kama mshahara haupiti kwao.
 
Kwa hiyo kelele zote kumbe umenyimwa mkopo

Si ungeenda Headoffice ukaonana na Head of Credit..
Nazungumzia mikopo ya wafanyakazi tena wa serikali wenye ajira za kudumu. Kwani hata kama ni Sera si huwa zinabadilishwa kuendana na mazingira ya biashara?Benki zote zilianza na hilo sharti baadae zikaamua kuliondoa wamebakia NMB tu ndo bado wanang'ang'ana nalo
 
Wewe Itakuwa unashida

Kuna kitu unaficha Itakuwa una mikopo mingi kila Bank
Kukopa sio dhambi wala siyo jambo la aibu.Matajiri wengi wana mikopo kwenye mabenki, serikali zote duniani zina mikopo na Marekani na utajiri wote ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa kukopa hela ndani na nje ya nchi.

Mtu mwenye uelewa mdogo anadhani kukopa ni jambo la aibu au ni dhambi!Kama ingekua hivyo matajiri wasingekopa kwa kuona aibu!Kama tajiri anakopa we masikini utashindwaje kukopa?
 
Back
Top Bottom