Wilson Elisha Nkhambaku ameteuliwa na JK kuwa mkuu wa wilaya ya kishapu na jina lake ni la 62 kwenye orodha ya wakuu wa wilaya.Kijana huyu mwenye umri wa miaka 37 alishinda kura za maoni kupitia CCM nakupata kura 3499 dhidi ya mbunge wa sasa Mohamed Missanga aliyepata 3433 lakini akaenguliwa na kamati kuu ya CCM na kuamua kuhamia CHADEMA tarehe 16/08/2010 na kusema kilichomkimbiza kutoka CCM, ni mizengwe iliyopelekea kueguliwa bila sababu za msingi. Baada ya mda si mrefu alitangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro hicho cha ubunge na kurudi CCM huku akiiponda CHADEMA na Dr Slaa akifanya kampeni jimboni humo.Nkhambaku alikuwa anakubalika sana alikuwa akisomesha watoto wengi jimboni humo wakati huo inasemakana alikuwa anafanya kazi world vission.Jimbo la Singida kusini liliokuwa chini ya Missnga liligawanywa mara mbili kupata majimbo ya Singida mashariki ma magharibi CCm ikihofia moto uliowashwa na Tundu Lissu tangu 2007 akitoa elimu ya uraia jimbo zima.Ilisemekana kwamba anehongwa ukuu wa wilaya akiacha kugombea na kweli tetesi za wakati huo zimetimia.
nawasilisha.
nawasilisha.