Njoolay amsifu Said Afri asema ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
BAADHI ya viongozi wa ngazi ya juu serikalini mkoani Rukwa na Katavi wamemwagia sifa Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi (Chadema) kuwa ni mfano wa kuigwa kwa wabunge wengine hususani wa upinzani kwa vile ni muelewa na wanafurahia kufanya naye kazi pamoja.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti , baadhi ya viongozi hao wakizungumzia hali ya kisiasa mkoani hapa hususani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, walidai kuwa hali ya kisiasa mkoani ni shwari kabisa.

Miongoni mwa viongozi hao ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa , Daniel Ole Njoolay ambaye bila kuumauma maneno alimmwagia sifa kemkem Arfi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni mchapakazi na kwamba ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema.

"Mheshimiwa Arfi hakika ni Mbunge wa mfano na yupo tofauti sana na wabunge wengine hususani wa Chadema kwani tunafurahia kufanya naye kazi pamoja.

“Hata kwenye vikao anachangia kwa hoja za msingi na si kwa kubeza au vinginevyo kwa kweli anastahili sifa, hana matatizo kabisa labda ndiyo maana hatuna purukushani zozote za kisiasa mkoani hapa,” alisema.

Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa mkoani hapa, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa hali ya kisiasa mkoani hapa baada ya uchaguzi Mkuu ni imara na shwari kabisa na kwamba wakazi wanaendela na shughuli za kimaendeleo kwa amani na utulivu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk. Rajab Rutengwe alimmwagia sifa Mbunge huyo akidai kuwa hajutii kuwa na Mbunge wa upinzani wilayani kwake kwani ametoa mchango mkubwa wa kuwahimiza wananchi kushiriki shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.

“Mheshimiwa Arfi si mwanasiasa anayehubiri amani na utulivu na si mtu wa shari wala vurugu …kwa kweli sijutii kufanya naye kazi hakika yuko tofauti sana na wabunge wenzake wa upinzani hususani wa chama chake cha Chadema kwani amekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wafuasi na mashabiki wa chama chake kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao wanakoishi,” alisema Arfi ambaye ni maarafu jimboni kwake kama ‘Babu’ ameweza kutetea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mpanda Kati sasa Mpanda Mjini kwa tiketi ya Chadema kwa vipindi viwili mfululizo, ni mbunge pekee kutoka chama cha upinzani mkoani hapa.
 
Kumfananisha Arfi na wabunge wengine wa upinzani ni kama kufanisha maziwa na tui la nazi, vyote ni vyeupe lakini tofauti zake ni kubwa saaaana. Arfi ni mtu makini na asiye kurupuka na wala hana papara, yeye ni mchapa kazi. Wala hana haja ya kujitafutia umaarufu usio na mpango kama wabunge wengine wa Chadema na vijikinda vyao vya juzi.
 
Hivi Bw. Majimshindo huoni kwamba nchini kwetu tunapata matatizo/changamoto nyingi sana (hospitalini-huduma si nzuri, dawa hazi kidhi mahitaji, umeme matatizo, rushwa n.k), na kwamba kila moja akikaa kimya basi walewalio na majukumu watakaa tu wakifikiri kila kitu kiposhwari! nimuhimu kuwe na watu wanapiga kelele ili viongozi wetu wasisale! wazidi kututumikia........
 
Hivi Bw. Majimshindo huoni kwamba nchini kwetu tunapata matatizo/changamoto nyingi sana (hospitalini-huduma si nzuri, dawa hazi kidhi mahitaji, umeme matatizo, rushwa n.k), na kwamba kila moja akikaa kimya basi walewalio na majukumu watakaa tu wakifikiri kila kitu kiposhwari! nimuhimu kuwe na watu wanapiga kelele ili viongozi wetu wasisale! wazidi kututumikia........

Kelele za mlango hazimshtuwi mwenye nyumba, kuna njia mbadala za upinzani kutumia badala ya makelele. Tumuulize Arfi, vipi jimbo lake anachaguliwa yeye na hana kelele na mambo huko mazuri kabisa, ana njia gani mbadala wa kelele?
 
Kelele za mlango hazimshtuwi mwenye nyumba, kuna njia mbadala za upinzani kutumia badala ya makelele. Tumuulize Arfi, vipi jimbo lake anachaguliwa yeye na hana kelele na mambo huko mazuri kabisa, ana njia gani mbadala wa kelele?

Ndo tabu ya Mpemba mzoea taarab. Nani mwenye nyumba sasa, katiba haioneshi uhusiano kati ya chama tawala na uenye nyumba. Suck you !
 
BAADHI ya viongozi wa ngazi ya juu serikalini mkoani Rukwa na Katavi wamemwagia sifa Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi (Chadema) kuwa ni mfano wa kuigwa kwa wabunge wengine hususani wa upinzani kwa vile ni muelewa na wanafurahia kufanya naye kazi pamoja.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti , baadhi ya viongozi hao wakizungumzia hali ya kisiasa mkoani hapa hususani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, walidai kuwa hali ya kisiasa mkoani ni shwari kabisa.

Miongoni mwa viongozi hao ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa , Daniel Ole Njoolay ambaye bila kuumauma maneno alimmwagia sifa kemkem Arfi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni mchapakazi na kwamba ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema.

"Mheshimiwa Arfi hakika ni Mbunge wa mfano na yupo tofauti sana na wabunge wengine hususani wa Chadema kwani tunafurahia kufanya naye kazi pamoja.

"Hata kwenye vikao anachangia kwa hoja za msingi na si kwa kubeza au vinginevyo kwa kweli anastahili sifa, hana matatizo kabisa labda ndiyo maana hatuna purukushani zozote za kisiasa mkoani hapa," alisema.

Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa mkoani hapa, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa hali ya kisiasa mkoani hapa baada ya uchaguzi Mkuu ni imara na shwari kabisa na kwamba wakazi wanaendela na shughuli za kimaendeleo kwa amani na utulivu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk. Rajab Rutengwe alimmwagia sifa Mbunge huyo akidai kuwa hajutii kuwa na Mbunge wa upinzani wilayani kwake kwani ametoa mchango mkubwa wa kuwahimiza wananchi kushiriki shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.

"Mheshimiwa Arfi si mwanasiasa anayehubiri amani na utulivu na si mtu wa shari wala vurugu …kwa kweli sijutii kufanya naye kazi hakika yuko tofauti sana na wabunge wenzake wa upinzani hususani wa chama chake cha Chadema kwani amekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wafuasi na mashabiki wa chama chake kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao wanakoishi," alisema Arfi ambaye ni maarafu jimboni kwake kama ‘Babu' ameweza kutetea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mpanda Kati sasa Mpanda Mjini kwa tiketi ya Chadema kwa vipindi viwili mfululizo, ni mbunge pekee kutoka chama cha upinzani mkoani hapa.

hao ndio viongozi tunaotaka,bwana Arfi nami namkubali sana na hana makeke kabisa kama wapinzni wengine esp yule bwana mdogo lema! siasa sio maandamano wala kelele ni vitendo,hongera sana bwana Arfi we tumikia wananchi wako na nina imani wananchi wa huko walikuchagua wewe na sio chadema na unaweza ukagombea chama chochote na ukashind tena coz we ni mtu wa vitendo,washauri wenzako watulie majimboni wawatumikie wapigakura wao na sio kwenda kuandamana kwani wananchi hatukuwatuma kwenda kuandamana bali kututumikia majimboni
 
mmeanza kujiandaa kukabiliana na maandamano. tuko liberia tukirudi tutasona muda mwafaka kuja kulianzisha huko rukwa!
 
hao ndio viongozi tunaotaka,bwana Arfi nami namkubali sana na hana makeke kabisa kama wapinzni wengine esp yule bwana mdogo lema! siasa sio maandamano wala kelele ni vitendo,hongera sana bwana Arfi we tumikia wananchi wako na nina imani wananchi wa huko walikuchagua wewe na sio chadema na unaweza ukagombea chama chochote na ukashind tena coz we ni mtu wa vitendo,washauri wenzako watulie majimboni wawatumikie wapigakura wao na sio kwenda kuandamana kwani wananchi hatukuwatuma kwenda kuandamana bali kututumikia majimboni

mmmmmmmmmh, sidhani kama hongera hii yatoka moyoni. Inonesha labda viongozi serikali wa mkoa wa katavi na wilaya ya mpanda ni waelewa na wanaweza kuchukua changamoto kama njia ya kujifunza; na mikoa mingine wako regid-km arusha ambao kitu kidogo tu-uhuru wa watu kuandamana na kutoa hisia zao uiwapa kiwewe na kutamani kuzuia. Hivyo, si suala la mbunge nani bali ni namna gani kiongozi wa serikali anavyoweza kuwa msikivu. Ndo maana hukusikia machafuko mz, kagera, syinganga na bukoba wakati wa maandamano.
 
huyo mong'oo hana jipya, wabunge wote wa CDM safi, wanatekeleza duty yao ya kukeep the government on its toes, aache kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
 
mmh leo tena! Au kwa kuwa Babu? Hapa kutakuwa kuna kamchezo wanamchezea Mr. Arfi!
 
Ndo tabu ya Mpemba mzoea taarab. Nani mwenye nyumba sasa, katiba haioneshi uhusiano kati ya chama tawala na uenye nyumba. Suck you !

Taabu ya mlevi mla nguruwe anayeishi Mbezi asiyejua Kiswahili vizuri lakini anadhani nchi hii ni ya kwake pekee yake!
 
Hakuna shida kama anatekeleza wajibu wake unavyopaswa ni kwa vile anatekeleza sera za chama chake kama wabunge wenzake wanavyofanya
 
BAADHI ya viongozi wa ngazi ya juu serikalini mkoani Rukwa na Katavi wamemwagia sifa Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi (Chadema) kuwa ni mfano wa kuigwa kwa wabunge wengine hususani wa upinzani kwa vile ni muelewa na wanafurahia kufanya naye kazi pamoja.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti , baadhi ya viongozi hao wakizungumzia hali ya kisiasa mkoani hapa hususani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, walidai kuwa hali ya kisiasa mkoani ni shwari kabisa.

Miongoni mwa viongozi hao ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa , Daniel Ole Njoolay ambaye bila kuumauma maneno alimmwagia sifa kemkem Arfi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni mchapakazi na kwamba ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema.

"Mheshimiwa Arfi hakika ni Mbunge wa mfano na yupo tofauti sana na wabunge wengine hususani wa Chadema kwani tunafurahia kufanya naye kazi pamoja.

"Hata kwenye vikao anachangia kwa hoja za msingi na si kwa kubeza au vinginevyo kwa kweli anastahili sifa, hana matatizo kabisa labda ndiyo maana hatuna purukushani zozote za kisiasa mkoani hapa," alisema.

Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa mkoani hapa, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa hali ya kisiasa mkoani hapa baada ya uchaguzi Mkuu ni imara na shwari kabisa na kwamba wakazi wanaendela na shughuli za kimaendeleo kwa amani na utulivu.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk. Rajab Rutengwe alimmwagia sifa Mbunge huyo akidai kuwa hajutii kuwa na Mbunge wa upinzani wilayani kwake kwani ametoa mchango mkubwa wa kuwahimiza wananchi kushiriki shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.

"Mheshimiwa Arfi si mwanasiasa anayehubiri amani na utulivu na si mtu wa shari wala vurugu …kwa kweli sijutii kufanya naye kazi hakika yuko tofauti sana na wabunge wenzake wa upinzani hususani wa chama chake cha Chadema kwani amekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wafuasi na mashabiki wa chama chake kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao wanakoishi," alisema Arfi ambaye ni maarafu jimboni kwake kama ‘Babu' ameweza kutetea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mpanda Kati sasa Mpanda Mjini kwa tiketi ya Chadema kwa vipindi viwili mfululizo, ni mbunge pekee kutoka chama cha upinzani mkoani hapa.

Mbinu zunu za kuigawa CHADEMA tumezishtukia hapa imekulakwenu manataka kumchooa Arfi muendeleze agenda ya Udini kama mnavyopanga na Zitto imekula kwenu mara mia.
 
hao ndio viongozi tunaotaka,bwana Arfi nami namkubali sana na hana makeke kabisa kama wapinzni wengine esp yule bwana mdogo lema! siasa sio maandamano wala kelele ni vitendo,hongera sana bwana Arfi we tumikia wananchi wako na nina imani wananchi wa huko walikuchagua wewe na sio chadema na unaweza ukagombea chama chochote na ukashind tena coz we ni mtu wa vitendo,washauri wenzako watulie majimboni wawatumikie wapigakura wao na sio kwenda kuandamana kwani wananchi hatukuwatuma kwenda kuandamana bali kututumikia majimboni

Habari yako Kashanga vp huko Russia? napita tu
 
Kazi ngumu kuliko zote ni kuwa kibaraka, kufanya kazi ambayo inapingana na nafsi yako na kusema vitu vya uongo ukitaka watu waviamini kuwa ni ukweli. Kuna watu hapa JF wanaonekana waziwazi kuwa ni vibaraka wakitumika kama vitendea kazi vya watu
 
Ndo tabu ya Mpemba mzoea taarab. Nani mwenye nyumba sasa, katiba haioneshi uhusiano kati ya chama tawala na uenye nyumba. Suck you !

Asiye juwa maana haambiwi maana, hata bibilia ina kitu kinaitwa "parables", jee, nayo ni taarabu?
 
Hakuna shida kama anatekeleza wajibu wake unavyopaswa ni kwa vile anatekeleza sera za chama chake kama wabunge wenzake wanavyofanya

Heko kwa kuliona hilo, kwenye red ndio nnposema mimi hao wabunge wenzake badili ya kukaa na kupoteza muda kwa makelele, maandamano, watu kuumia na mpaka kupoteza maisha, kwa nini hawafati mfano wa kuigwa wa Arfi?
 
Mbinu zunu za kuigawa CHADEMA tumezishtukia hapa imekulakwenu manataka kumchooa Arfi muendeleze agenda ya Udini kama mnavyopanga na Zitto imekula kwenu mara mia.

Hayo ya udini unayasema wewe. Sisi tunasema, heko Arfi. Upinzani si fujo na maandamano, upinzani ni kuchapa kazi zaidi ya waliopo kwenye madaraka ili waonekane hawafai.
 
Back
Top Bottom