nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
BAADHI ya viongozi wa ngazi ya juu serikalini mkoani Rukwa na Katavi wamemwagia sifa Mbunge wa Mpanda Kati, Said Arfi (Chadema) kuwa ni mfano wa kuigwa kwa wabunge wengine hususani wa upinzani kwa vile ni muelewa na wanafurahia kufanya naye kazi pamoja.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti , baadhi ya viongozi hao wakizungumzia hali ya kisiasa mkoani hapa hususani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, walidai kuwa hali ya kisiasa mkoani ni shwari kabisa.
Miongoni mwa viongozi hao ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa , Daniel Ole Njoolay ambaye bila kuumauma maneno alimmwagia sifa kemkem Arfi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni mchapakazi na kwamba ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema.
"Mheshimiwa Arfi hakika ni Mbunge wa mfano na yupo tofauti sana na wabunge wengine hususani wa Chadema kwani tunafurahia kufanya naye kazi pamoja.
Hata kwenye vikao anachangia kwa hoja za msingi na si kwa kubeza au vinginevyo kwa kweli anastahili sifa, hana matatizo kabisa labda ndiyo maana hatuna purukushani zozote za kisiasa mkoani hapa, alisema.
Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa mkoani hapa, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa hali ya kisiasa mkoani hapa baada ya uchaguzi Mkuu ni imara na shwari kabisa na kwamba wakazi wanaendela na shughuli za kimaendeleo kwa amani na utulivu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk. Rajab Rutengwe alimmwagia sifa Mbunge huyo akidai kuwa hajutii kuwa na Mbunge wa upinzani wilayani kwake kwani ametoa mchango mkubwa wa kuwahimiza wananchi kushiriki shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.
Mheshimiwa Arfi si mwanasiasa anayehubiri amani na utulivu na si mtu wa shari wala vurugu kwa kweli sijutii kufanya naye kazi hakika yuko tofauti sana na wabunge wenzake wa upinzani hususani wa chama chake cha Chadema kwani amekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wafuasi na mashabiki wa chama chake kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao wanakoishi, alisema Arfi ambaye ni maarafu jimboni kwake kama Babu ameweza kutetea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mpanda Kati sasa Mpanda Mjini kwa tiketi ya Chadema kwa vipindi viwili mfululizo, ni mbunge pekee kutoka chama cha upinzani mkoani hapa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti , baadhi ya viongozi hao wakizungumzia hali ya kisiasa mkoani hapa hususani baada ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika mwezi Oktoba mwaka jana, walidai kuwa hali ya kisiasa mkoani ni shwari kabisa.
Miongoni mwa viongozi hao ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa , Daniel Ole Njoolay ambaye bila kuumauma maneno alimmwagia sifa kemkem Arfi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa kuwa ni mchapakazi na kwamba ipo tofauti kubwa kati yake na wabunge wengine wa Chadema.
"Mheshimiwa Arfi hakika ni Mbunge wa mfano na yupo tofauti sana na wabunge wengine hususani wa Chadema kwani tunafurahia kufanya naye kazi pamoja.
Hata kwenye vikao anachangia kwa hoja za msingi na si kwa kubeza au vinginevyo kwa kweli anastahili sifa, hana matatizo kabisa labda ndiyo maana hatuna purukushani zozote za kisiasa mkoani hapa, alisema.
Akizungumzia kuhusu hali ya kisiasa mkoani hapa, Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa hali ya kisiasa mkoani hapa baada ya uchaguzi Mkuu ni imara na shwari kabisa na kwamba wakazi wanaendela na shughuli za kimaendeleo kwa amani na utulivu.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Dk. Rajab Rutengwe alimmwagia sifa Mbunge huyo akidai kuwa hajutii kuwa na Mbunge wa upinzani wilayani kwake kwani ametoa mchango mkubwa wa kuwahimiza wananchi kushiriki shughuli za maendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.
Mheshimiwa Arfi si mwanasiasa anayehubiri amani na utulivu na si mtu wa shari wala vurugu kwa kweli sijutii kufanya naye kazi hakika yuko tofauti sana na wabunge wenzake wa upinzani hususani wa chama chake cha Chadema kwani amekuwa mstari wa mbele kuwahimiza wafuasi na mashabiki wa chama chake kushiriki kwenye shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao wanakoishi, alisema Arfi ambaye ni maarafu jimboni kwake kama Babu ameweza kutetea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mpanda Kati sasa Mpanda Mjini kwa tiketi ya Chadema kwa vipindi viwili mfululizo, ni mbunge pekee kutoka chama cha upinzani mkoani hapa.