Kitotole
Senior Member
- Jan 18, 2020
- 138
- 228
Nakumbuka Miaka ya 90 na kitu hivi kuna sehemu inaitwa Mwananyamala mchangani, kuna kaeneo wamekapa jina "jitu kubwa" ama "mtini" kwenye mti huu panasifika sana kufanyika mambo ya kishirikina, na inasemekana kwenye huu mti ndio makutano yao wazee wa kazi. Wazazi walikuwa wanatukataza na kutuonya sana tusiende kucheza maeneo yale. Lakini cha ajabu watu kila kukicha watoto kwa wakubwa tulikuwa tukikutana pale na kukaa kwenye mizizi ya mti huo ambayo ni mikubwa mfano wa magogo(ma benchi) na kupiga soga pamoja na kuendelea na michezo mbali mbali ya kitoto bila kujali maonyo ya wazazi wetu. Hii nadhani ni kutokana na hewa nzuri inayopatikana mtini hapo.
Basi siku moja tukiwa tunaendelea na michezo mimi na mwenzangu chini ya mti, mara matunda mfano wa vitunguu vikamwangukia kichwani, kila akijaribu kutoa havitoki, ikabidi akimbilie nyumbani kwao, nami nikimbilie home kwetu. Baada ya muda kidogo tunasikia vilio kwa majirani kwamba yule dogo amefariki, hakika niliogopa sana na sikutoka nje siku nzima kwa hofu. Ilifikia stage nikitumwa dukani natafuta njia nyingine ama nikipita pale napita na speed 100 hata iwe mchana. Hili tukio sitalisahau na leo kwa mara ya kwanza ndio nalisimulia kwani sikuwahi kumwambia mtu yeyote hii kitu.
Pmengi yametokea ktk mti huo ikiwemo la jamaa aliyekutwa amekufa akiwa amelala hapo mtini.
Kwa sasa ni miaka takriban 30 imepita najiuliza km vile vitu vingeniangukia mimi sijui ningekuwa wapi le hii. Sina hakika km huu mti bado upo maana kila watu wakijaribu kuukata kunatokea vikwazo eidha uwake moto ama kwa baadh ya watu kupinga zoezi hilo. Kuna mzee alikuwa anasifika kwa zoezi la ukataji miti lkn kwenye huu alichemka na mara baada ya kumaliza jaribio la kuukata naye akapoteza maisha.
Wachawi wanapata faida gani kwani?
Mungu ashukuriwe.
Basi siku moja tukiwa tunaendelea na michezo mimi na mwenzangu chini ya mti, mara matunda mfano wa vitunguu vikamwangukia kichwani, kila akijaribu kutoa havitoki, ikabidi akimbilie nyumbani kwao, nami nikimbilie home kwetu. Baada ya muda kidogo tunasikia vilio kwa majirani kwamba yule dogo amefariki, hakika niliogopa sana na sikutoka nje siku nzima kwa hofu. Ilifikia stage nikitumwa dukani natafuta njia nyingine ama nikipita pale napita na speed 100 hata iwe mchana. Hili tukio sitalisahau na leo kwa mara ya kwanza ndio nalisimulia kwani sikuwahi kumwambia mtu yeyote hii kitu.
Pmengi yametokea ktk mti huo ikiwemo la jamaa aliyekutwa amekufa akiwa amelala hapo mtini.
Kwa sasa ni miaka takriban 30 imepita najiuliza km vile vitu vingeniangukia mimi sijui ningekuwa wapi le hii. Sina hakika km huu mti bado upo maana kila watu wakijaribu kuukata kunatokea vikwazo eidha uwake moto ama kwa baadh ya watu kupinga zoezi hilo. Kuna mzee alikuwa anasifika kwa zoezi la ukataji miti lkn kwenye huu alichemka na mara baada ya kumaliza jaribio la kuukata naye akapoteza maisha.
Wachawi wanapata faida gani kwani?
Mungu ashukuriwe.