Njoo tuongee na January Makamba: Asema nyumba ya mama Lwakatare inasubiri maamuzi ya mahakama kubomolewa

Sauti za Wananchi

Senior Member
Sep 2, 2014
113
138
makamba Jan.jpg

Kwa ushirikiano wa karibu na JamiiForums, tunatarajia kuanza kwa kipindi kipya kiitwacho 'Njoo Tuongee' ambacho kitahusisha mjadala na Mawaziri kutoka Serikalini kuhusiana na masuala ya wananchi.

Kwa muda wa wiki 7, Mawaziri mbalimbali watawekwa 'Kitimoto' LIVE kupitia Star TV ili kujibu maswali kutoka kwa wanaowaongoza.

Kipindi cha kwanza kitaanza kurushwa kesho (Ijumaa O3, 2017), SAA 12:30 JIONI na Waziri tutakayeanza naye atakuwa ni Mheshimiwa January Makamba ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira.

Lengo kuu la kipindi hiki ni kuwapa nafasi wananchi kujua wanachokifanya Mawaziri na kuwauliza ni wapi wanakwama katika kutatua changamoto mbalimbali.

Sasa kupitia JamiiForums, unaweza kuuliza maswali au kutoa maoni ambayo baadhi yao yatakayopata nafasi, yatakusanywa na kuwasilishwa kunakohusika kisha kuulizwa moja kwa moja kwa mgeni wa siku hiyo.

Je, una swali, maoni, jambo lolote unataka kuliwasilisha kwa Ndg. January Makamba?

Karibu sana..
--------

UPDATES > 3/11/2017..

Kipindi hiki kimetayarishwa na Twaweza kwa kushirikiana na Star TV, Compass Communications na JamiiForums.

Mgeni: January Makamba (Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano)
Watangazaji: Aidan Eyakuze na Maria Sarungi-Tsehai

UNAWEZA KUFUATILIA MJADALA HUU LIVE HAPA CHINI;


======

UPDATES:

Maria Sarungi: Katika kipindi hiki tutakuwa tunajikita katika taarifa zenye takwimu sahihi kabisa.

Swali: Mnafanyaje kazi kwa pamoja?

Majibu: Mwanzoni mazingira ilikuwa chini ya wizara ya maliasili na mazingira. Kwa sasa ipo chini ya ofisi ya Makamu ya rais.

Swali: Ilikuwaje mkatoa kibali cha ujenzi eneo ambalo lina mafuriko pale Jangwani?

Majibu(Makamba): Eneo hili lilipata kibali mahususi na waziri alijiridhisha kwamba eneo lile lisingeweza kuhatarisha maisha ya watu

Swali(Sarungi): Maeneo wanayoishi wananchi kuna uchafu, wizara yako imejipanga vipi kuhakikisha wananchi wanaishi katika mazingira mazuri

Majibu(Makamba): Inabidi tupange mkakati mzuri ili tuweze kuhimili maafa katika mazingira yetu kwa kushirikiana na mamlaka zote. TANROADS, manispaa, TANESCO

Swali(Sarungi): Wizara imefikia wapi katika suala mbunge na Mchungaji Rwakatare kujenga katika eneo la mto na kuharibu uoto wa mikoko?

Majibu: Hilo swala lipo mahakamani na mpaka sasa linasubiria maamuzi yamahakama. Pia kwa wale waliokuwa wanabomolewa Mkwajuni bado shauri hilo halijaamuliwa.

Swali(Aidan): Ni hatua gani serikali imechukua kuambatanisha teknolojia kwenye mazingira?

Majibu(Makamba): Moja ya mambo yanayoweza kupunguza uharibifu wa mazingira ni matumizi ya nishati mbadala kwa mfano gesi asili

Swali(Aidan): Tumejiandaa vipi kutumia nishati rafiki?

Majibu(Makamba):Tumeandika sera mpya ya mazingira na katika sera hii tumeweka vichocheo vya teknolojia rafiki kama viwandani na kupikia. Vichocheo hivyo ni kurahisishaji uagizaji na uingizaji wa teknolojia rafiki.

Swali(Aidan): Una mkakati gani wa kuwarudishaia wananchi wa kibiti mazingira mazuri na kuendelea na shughuli zao?

Majibu(Makamba): Mkaa haupunguzi gharama ya nishati. Tunapoelekea tunaweka mkakati wa kuweza kupata nishati mbadala. Kuna mkaa unaotokana na taka au mabaki ya mazao. Nitakachofanya ni kuwajengea uwezo wajasiriamali hawa ili kuongeza uzalishaji

Swali: Ni lini gesi itapungua bei?

Majibu(Makamba): Gesi inayotumika inatoka kwa Mtwara kwa njia ya mabomba ambayo inasambazwa majumbani. Gesi inayotumia mitungi inatoka nje.

Swali(Aidan): Kenya na Uganda wamefanikiwa kuzuia mifuko ya plastiki na hakuna madhara. Nini mpango wa wizara yako.

Majibu(Makamba): Tumefanya ziara Rwanda na Zambia kuona jinsi walivyoweza kufanya na tumerudi tumefanya tathmini na suala hili linajumuisha wizara ya viwanda na nyinginezo. Kwasasa lipo katika mchakato wa kiserikali.

Swali(Aidan): Nini mchakakati wa serikali yako katika kuzuia kelele za mabaa, vigodoro na muziki.

Majibu: Tunachofanya ni kupokea malalamiko na kuyashughulikia. Kama baa imefuata makazi ya watu. Hata juzi kuna baa tumeifungia kule Dodoma.


Swali(Sarungi): Ulijisikiaje maamuzi juu ya NEMC kupinduliwa? Unafikiri una moral authority juu ya bodi ya NEMC?

Majibu(Makamba): Kwa kiongozi wa serikali kufanya maamuzi alafu wakubwa wako wakafanya tofauti ni jambo la kawaida.

Amabacho kilifanyika tulikubaliana wapewe nafasi nyingine kwa muda. Lakini mimi nina moral authority juu yao.

Swali(Aidan): Mmewahi kuwauliza wananchi kama kero za muungano zimetatuliwa?

Majibu(Makamba): Sheria ya haki za binadamu ilikuwa haitumiki Zanzibar. kwa haya mambo ya muungano

Swali(Sarungi): Kuhusu swala la tofauti tozo za kodi kati ya Zanzibar na Bara

Majibu(Makamba): Changamoto ni mifumo tofauti ya ukadiriaji wa kodi. Tulikubaliana iwekwe mifumo inayofanana katika ukadiriaji wa kodi. Na kwa sasa mifumo hiyo ishafungwa Zanzibar ili wananchi wasiendelee kutozwa hiyo tofauti ya kodi.

Swali(Aidan): Kuna mkanganyiko kati ya watanzania waishio bara na Zanzibar. Nini kifanyike kuondoa mkanganyiko huu?

Makamba: Dhana tuliyonayo katika kuunda muungano ni kutoua haiba ya Uzanzibar


Swali(Swali): Katika kushughulikia maswala ya muu, kunapaswa kuwepo ofisi sehemu zote mbili

Makamba: Ofisi zipo pande zote mbili.

Swali(Sarungi): Zanzibar na Tanganyika ni nchi moja kwanini tuna serikali mbili?
Ni swala la muundo wa serikali na ilikubaliwa kuwe na serikali mbili.

Swali(Aidan): Je umejikita vipi kumbadilisha mwananchi tabia ili asiharibu mazingira?

Majibu(Makamba): Inahitaji falsafa ya kufungamanisha suala hili katika malengo yetu.

Swali(Aidan): Ipi unaipenda zaidi kati ya Mazingira na muungano? Na unaipangaje siku yako

Majibu(Makamba): Napenda sana mazingira na nimefungamana nayo hata nikistaafu katika wizara hii.
Muungano ni suala pana sana kitaifa na kimataifa na linanipa pia.
Wakati mwingine nakuwa Zanzibar na wakati mwingine nakuwa bara

~~~MWISHO~~~
 
Imepita miaka mingi nyumba ya mama Lwakatare haijabomolewa pamoja na NEMC kutoa notisi ya kuvunja nyumba kwa sababu za kimazingira ambapo inadaiwa ujenzi wake unazuia mto Numbwi na uko jirani na Mikoko, wizara imefikia wapi? Hawaoni kwamba watu waliobomolewa wanajisikia vibaya pamoja kuwa walikuwa na zuio la mahakama kama mama Lwakatare?
 
Wataulizwa maswali kwa wananchi kupiga simu moja kwa moja au watakuwa wanapewa maswali wanalala nayo alafu wanakuja kupiga poyoyo hapo. Kama maswali yataulizwa moja kwa moja na wannchi kwa njia ya simu,hicho kipindi ijumaa ndio itakuwa mwanzo na mwisho wake.
 
Imepita miaka mingi nyumba ya mama Lwakatare haijabomolewa pamoja na NEMC kutoa notisi ya kuvunja nyumba kwa sababu za kimazingira ambapo inadaiwa ujenzi wake unazuia mto Numbwi na uko jirani na Mikoko, wizara imefikia wapi? Hawaoni kwamba watu waliobomolewa wanajisikia vibaya pamoja kuwa walikuwa na zuio la mahakama kama mama Lwakatare?

Unaota wewe. Hilo jengo halitakaa liguswe maana hata Magufuli kamteua huyo mama kwa moyo safi kuwa Mbunge viti maalumu.. Kuna watu na viwatu!
 
Mkuu how shuld we trust u. Ungejitambulisha ikiwa wewe ndo January au host husika. Intro yako inaelea bado
 
Unaota wewe. Hilo jengo halitakaa liguswe maana hata Magufuli kamteua huyo mama kwa moyo safi kuwa Mbunge viti maalumu.. Kuna watu na viwatu!
Aktaka ibomolewe ahamie upinzani kwanza. Hivi yale masaa aliyotoa kangi yataisha lini
 
Kuna kauli mbalimbali Mheshimiwa Waziri amezitoa katika vipindi mbalimbali vya bunge la bajeti kuhusiana na kupiga marufuku mifuko ya Plastiki, kauli hizo zimeshindwa kutekelezwa hadi sasa pamoja na athali kubwa kwenye mazingira zinazosababishwa na mifuko hii. Je Waziri analipi la kutwambia juu ya hatima ya jambo hili katika nchi yetu?
 
Kwa kiwango gani swala la kuzuia uuzwaji wa viroba limesaidia kutunza mazingira?

Na je upi mkakati wa serikali juu ya kuzuia upigaji wa kelele zilizopitiliza kwenye makazi ya watu? Kwani mabaa, vigadoro, kelele za miziki imekuwa kero sana kwenye mitaa
 
Aktaka ibomolewe ahamie upinzani kwanza. Hivi yale masaa aliyotoa kangi yataisha lini

Achana na hayo.. Mimi swali langu kwa Mheshimiwa Waziri ni kuhusu tatizo la kule Kibiti.

Gazeti la Mwananchi liliwahi kuripoti kuwa chanzo cha vurumai za kule, pamoja na mambo mengine, ni wananchi kuzuiwa kufanya shughuli za mazao ya rasilimali (mainly kukata mkaa) na kunyang'anywa baadhi ya mali zao na watendaji wa kule..

Je,yeye akiwa kama Waziri, ana mkakati gani wa kuwarudishia wananchi wa Kibiti mazingira mazuri ya kufanya shughuli za kuwaingizia kipato ikiwemo ukataji wa mkaa kwa sababu ndio biashara kuu kwa eneo husika?
 
Hao ni host wa hicho kipindi. Fuatilia threads zao za nyuma ni watu serious..
Oohh okay sawasawa.
Mhrshimiwa atupe majibu ya nyumba ya Rwakatare, nyumba za kimara na nyumba za mwanza. Kimsingi kuna majibu mengi hapa kuliko maswali
 
Kutokana na kupanda kwa bei ya gesi kila wakati wizara yake inachukua hatua gani kupambana na hili swala ukizingatia kwamba matumizi ya gesi ndio yangeweza kupunguza matumizi ya kuni na mkaa ambavyo vinachochea ukataji miti (uharibifu WA mazingira)?
 
Miaka ya nyuma kidogo ilikuwa ukitembea unakutana na hali nzuri ya mazingira nikiwa na maama ya uoto wa asili lakini kadri miaka inavyozidi kwenda ukame unazidi.

Licha ya changamoto za mabadiliko ya kimazingira duniani wizara imejipangaje kupunguza hii hali ? Au imekubali kisa tu ni tatizo la dunia nzima? Elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari haitoshi waende hadi mashinani mtaa kwa mtaa nchi zitbaki jangwa.
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom