Njombe: Polisi Waua Jambazi sugu Makambako

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Heshima kwenu wakuu,

Usiku wa kuamkia leo, Polisi Mjini Makambako wameua Jambazi baada ya kurushiana risasi.

Polisi wa Doria walipata taarifa kwamba majambazi wanataka kuiba katika kituo cha Mafuta Makambako ndipo walipoenda.

Walipofika wale majambazi wakaanza kurusha risasi ovyo ovyo, ndipo polisi Mmoja mwenye shabaha alipomlenga jambazi mmoja risasi na kufa hapopo.

Nawapongeza Jeshi la polisi kwa jinsi wanavyokula shani moja na Wahalifu, Wanalala nao mbele haswaa

Nawashauri wale wenye Tabia za Ujambazi waache kwani siku zao zinahesabika. Zama zimebadilika pia.

Ni wakati wa Makonda kuwapa hawa Askari wa Makambako Milioni yao.


==================

Jambazi auawa na Polisi Njombe
Temuuu.JPG

Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, John Temu.

Mtu anaye daiwa kuwa ni jambazi ameuwawa katika majibizano ya risasi na jeshi la Polisi katika mji wa Makambako mkoani Njombe ambako majambazi hao walitaka kufanya tukio la uvamizi katika kituo cha mafuta.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe, John Temu, amesema jeshi la polisi lilibaini kuwapo kwa watu wanaohisiwa kuwa ni majambazi majira ya saa 3:30 usiku ambao walikusudia kuvamia kituo hicho ambapo polisi walifika eneo la tukio na kuanza kufyatuliana risasi.

Polisi baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamalia wema walifika eneo la tukio lakini watuhumiwa hao baada ya kuona gari ya polisi walianza kurusha risasi hovyo ndipo askari walipoanza kujibu mashambulizi na kumpiga risasi mmoja kati ya watuhumiwa hao aliye kuwa na silaha

Katika majibizano ya silaha baina ya polisi na watuhumiwa hao polisi walimpiga mmoja kati ya watuhumiwa hao na ambaye alikimbizwa katika hospitali ya halmashauri ya mji wa makambako ambapo mtuhumiwa alifariki dunia kabla hajafikishwa hospitalini.

Aidha, Temu amebainisha aina ya silaha waliyoikamata kuwa ni Long Life Caliber 22mm yenye namba za usajili A 194300 ambayo ina Darubini ya kuona mbali na kuongeza kuwa silaha hiyo imetengenezwa nchini Czech na ilikutwa ikiwa na risasi tano zilizo kuwa kwenye magazine.

Chanzo: Blogs
 
Nakumbuka mwishoni mwa miaka ya 70 au mwanzoni mwa miaka ya 80 alikuwepo jambazi tishio aliyeitwa Kipagatyee
Hata mimi babu yangu alinisimulia kuhsu jambazi kipagate wa mafinga .Alikuwa akitumia dawa kuiba hata ungeweka walinzi wangapi... yeye lazima aingie ndani tu na afanye yake.
serikali waliamua kumtumia dada mrembo wa usalama wa taifa, alijigonga kwake hadi wakakubaliana wafunge ndoa.nasikia siku ile ya ndoa muda wa HONEY MOON wakiwa hotelini wakati huo illitwa JOHN'S CORNER(kwa sasa ni ka- bar uchwara kanaitwa john's corner ndogo) ndo mchizi alikamatwa kwani yule dem alimuomba atoe zile hirizi kiunoni wakaoge...ile amemaliza tu kutoa na kwenda bafuni polis hao .eti jamaa alitaka kukimbilia hirizi zake wajomba wakam-miminia risasi za maana miguuni kumbuka kuwa before; risasi zilikuwa zikidunda na muda mwingine alikuwa akiyeyuka hewani, mhhhh ni kama movie jaman, bas jamaa ndo alidakwa kwa fashion hiyo. lol nilicheka sana. mwanamke ni kitu kingine hapana chezea kabsa!
 
Daah mbona Jana nlilala makambako nkiwa naelekea songea, mida hyo nlikua natuliza koo Durban hotel Makambako, sikusikia hii issue aisee na hata asbh sijaisikia kabisa. Kazi nzuri kwa askari wetu
 
Hata mimi babu yangu alinisimulia kuhsu jambazi kipagate wa mafinga .Alikuwa akitumia dawa kuiba hata ungeweka walinzi wangapi... yeye lazima aingie ndani tu na afanye yake.
serikali waliamua kumtumia dada mrembo wa usalama wa taifa, alijigonga kwake hadi wakakubaliana wafunge ndoa.nasikia siku ile ya ndoa muda wa HONEY MOON wakiwa hotelini wakati huo illitwa JOHN'S CORNER(kwa sasa ni ka- bar uchwara kanaitwa john's corner ndogo) ndo mchizi alikamatwa kwani yule dem alimuomba atoe zile hirizi kiunoni wakaoge...ile amemaliza tu kutoa na kwenda bafuni polis hao .eti jamaa alitaka kukimbilia hirizi zake wajomba wakam-miminia risasi za maana miguuni kumbuka kuwa before; risasi zilikuwa zikidunda na muda mwingine alikuwa akiyeyuka hewani, mhhhh ni kama movie jaman, bas jamaa ndo alidakwa kwa fashion hiyo. lol nilicheka sana. mwanamke ni kitu kingine hapana chezea kabsa!

mmhh! ni udesi!! risasi zinadunda!! halafu jamaa anayeyukia angani!!
 
mmhh! ni udesi!! risasi zinadunda!! halafu jamaa anayeyukia angani!!
hata mie sikwepo ndo maana nimesema nlisimuliwa ni kitu ambacho sikukishuhudia. na kama hauamini mambo ya giza yapo basi kaa kimya. pale igowole mufindi mwaka jana tu wamekamata majambazi waliokuwa wakitumia nguvu za giza. wao ni kama unamfukuzia usiombe tu akate kona bila wewe kumuona ndo ntolee hiyo. na walipokamatwa walimtaja hadi mganga anayewapa hirizi. oweee kalaga bakho! lol
 
Hata mimi babu yangu alinisimulia kuhsu jambazi kipagate wa mafinga .Alikuwa akitumia dawa kuiba hata ungeweka walinzi wangapi... yeye lazima aingie ndani tu na afanye yake.
serikali waliamua kumtumia dada mrembo wa usalama wa taifa, alijigonga kwake hadi wakakubaliana wafunge ndoa.nasikia siku ile ya ndoa muda wa HONEY MOON wakiwa hotelini wakati huo illitwa JOHN'S CORNER(kwa sasa ni ka- bar uchwara kanaitwa john's corner ndogo) ndo mchizi alikamatwa kwani yule dem alimuomba atoe zile hirizi kiunoni wakaoge...ile amemaliza tu kutoa na kwenda bafuni polis hao .eti jamaa alitaka kukimbilia hirizi zake wajomba wakam-miminia risasi za maana miguuni kumbuka kuwa before; risasi zilikuwa zikidunda na muda mwingine alikuwa akiyeyuka hewani, mhhhh ni kama movie jaman, bas jamaa ndo alidakwa kwa fashion hiyo. lol nilicheka sana. mwanamke ni kitu kingine hapana chezea kabsa!
Mkuu hiyo siyo muvi ya kinaijeria kweli.
 
mmhh! ni udesi!! risasi zinadunda!! halafu jamaa anayeyukia angani!!
hivi we jamaa unajua kusoma kweli,teh teh teh ni nouma. usipende kukurupuka soma vizuri. mie nimesema HEWANI wewe wewe unaongelea ANGANI. ni hatari kwa afya. LOL
 
Nakumbuka mwishoni mwa miaka ya 70 au mwanzoni mwa miaka ya 80 alikuwepo jambazi tishio aliyeitwa Kipagatyee
ebwana unanikumbusha mbali. Yani huyu jambaz alikuwa hatari sana. Ilikuwa 1978 hadi 1983 kama sijakosea alivyouwawa akijaribu kupora duka flan hiv. Nakumbuka nilikuwa kwenye mid teens hivi
 
Back
Top Bottom