Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,191
- 4,104
Mwanamke ambaye ni mjamzito Mkazi wa Mtaa wa Joshoni Halmashauri ya Mji wa Njombe amebakwa na Wanaume wanne kwa masharti ya kutokupiga kelele akiwa ametishiwa kuuawa huku akiwa amefungwa kitambaa mdomoni pamoja na kamba mikononi.
Mwanamke huyo amesema tukio hilo lilimtokea July 10,2022 majira ya saa saba usiku nje ya nyumba anayoishi huku Wanaume hao wakihitaji fedha kabla ya kufanyiwa ukatili huo.
“Nilikuwa nimelala nikasikia komeo inachezewa, nilipofungua mlango Watu wanne wakaingia wawili wakiwa wameshika panga na wawili wakiwa wameshika visu wakapekua kwenye pochi na kuchukua hela pamoja na simu iliyokuwa kitandani”
Aidha Mwanamke huyo amesema mara baada ya kupekuliwa kwa lengo la kuhitaji fedha zaidi na kushindwa kuzipata kwa kuwa hakuwa na kiasi kingine ndipo walipomuamuru kutoka nje kwakuwa ndani alikuwa amelala na Mtoto wa jirani yake na kumfanyia ukatili huo akiwa amefungwa kitambaa mdomoni na baada ya kumaliza kitendo hicho waliweza kuondoka na nguo zake za ndani.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Joshoni, Amon Swale amekiri kutokea kwa tukio hilo katika Mtaa wake na kusema Serikali ya mtaa imejipanga kuitisha mkutano wa dharura ili kujadili kwa pamoja kwa kuwa licha ya tukio hilo lakini siku za karibuni kumekuwa na matukio mengine yakiwemo ya uporaji na uvunjaji wa nyumba nyakati za usiku.
Mwanamke huyo amesema tukio hilo lilimtokea July 10,2022 majira ya saa saba usiku nje ya nyumba anayoishi huku Wanaume hao wakihitaji fedha kabla ya kufanyiwa ukatili huo.
“Nilikuwa nimelala nikasikia komeo inachezewa, nilipofungua mlango Watu wanne wakaingia wawili wakiwa wameshika panga na wawili wakiwa wameshika visu wakapekua kwenye pochi na kuchukua hela pamoja na simu iliyokuwa kitandani”
Aidha Mwanamke huyo amesema mara baada ya kupekuliwa kwa lengo la kuhitaji fedha zaidi na kushindwa kuzipata kwa kuwa hakuwa na kiasi kingine ndipo walipomuamuru kutoka nje kwakuwa ndani alikuwa amelala na Mtoto wa jirani yake na kumfanyia ukatili huo akiwa amefungwa kitambaa mdomoni na baada ya kumaliza kitendo hicho waliweza kuondoka na nguo zake za ndani.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Joshoni, Amon Swale amekiri kutokea kwa tukio hilo katika Mtaa wake na kusema Serikali ya mtaa imejipanga kuitisha mkutano wa dharura ili kujadili kwa pamoja kwa kuwa licha ya tukio hilo lakini siku za karibuni kumekuwa na matukio mengine yakiwemo ya uporaji na uvunjaji wa nyumba nyakati za usiku.