Njombe: Mfungwa apora Bunduki kwa Askari na kumpiga kaka yake kwa kushindwa kumtoa Gerezani na kuuza mashamba ya familia

Juzi askar wa Iringa walichachamaa kutafuta wafungwa, inasemekana walikua kazini wakampiga askr magerz na mapanga halafu wakatoroka na bunduki.
Sasa story ya hapo juu inachanganya sijui inazungumzia tukio la Njombe au hili la Iringa.
Ndiyo tukio hilo hilo mkuu. Wengine walikimbilia Iringa na ndiyo maana walifatwa huko.
 
Juzi askar wa Iringa walichachamaa kutafuta wafungwa, inasemekana walikua kazini wakampiga askr magerz na mapanga halafu wakatoroka na bunduki.
Sasa story ya hapo juu inachanganya sijui inazungumzia tukio la Njombe au hili la Iringa.
Kwa nini wahehe mnafuga majambazi sana?
 
Miss Zomboko

Umekuja kupost haraka bila kutofautisha km njombe IPO Iringa au ?

Pia tukio lilikuwa Iringa sio njombe!


Na uwasilishaji taarifa umekiuka maadili unawafanya polisi waonekane hamnazo.


Sikuingine utulie ndio upost.
 
Askari wa sikuizi sijui depo huwa wanaenda kufanyaje tu si bora mafunzo wafanyie nyumbani tu
 
Kaka na mdogo wake wanatofautiana umri kwa miaka 37!!
Kuna wale wazazi wanaozaa watoto wa uzeeni, anakuwa na watoto wakubwa anaenda kuchukua dogodogo na kuanza kufyatua vijukuu, wapo wengi tu hasa maeneo ya vijijini. Sasa automatically huo utakuwa mzigo wa watoto wakubwa maana mara nyingi wazee wa dizani hiyo huwa hawana mwelekeo wowote.
 
Hii habari labda mm pekee nimeshindwa kuielewa,

Yaan uwe mfungwa umpore Askari silaha umpige nayo mtu(hapa ni Kama tukio lililotekelezwa kwa haraka sana) sasa inakuaje kaenda kufanya nayo matukio mbali mbali na kutumia risasi zote7 wakati ni mfungwa?

Alafu et asingekufa angeeleza aliwezaje kutoka na silaha(hapa hakumpora mtu)
Mkuu hui habari inaonekana mbili tofaut lkn inamhusu marehemu mtuhumiwa afande kashindw kuelezea vizur hata mm nimeshindwa kumwelewa afande 😀
 
Askar magerez kupokonyw silahi ni kawaida kutokana na mazingr ya wanayo yawek na wafungwa.
Utakut wanapiga story na kuwa jiran bila kujua siku hiyo wafungwa wameamkaje.
 
Umeona eeeh.
Bado hawajajua aliporaje, si wamuulize aliye porwa.
Siku hiyo hiyo apore silaha
Kawaruhusu wenzake watoroke
Amuadhibu Kaka yake
Halafu dogo Yuko 24 only.
Hiz ndio zile picha mtu mmoja anapiga watu200 bila bunduki
 
KWA AMBAO HAWAJAELEWA

Askari magereza aliwapeleka wafungwa kufanya kazi. Walikuwa jumla ya wafungwa wanne.

Kazi ilihusisha utumiaji wa panga. Sasa nyampara katika kundi hilo ambaye ndiye mtajwa hapo juu akam-time askari kashangaa akamshushia panga la haja.

Baada ya askari magereza kwenda chini,wakamnyang'anya hiyo bunduki na kutokomea.

Ndiyo hiyo bunduki akaenda kumjeruhi nduguye. Hata hivyo wote baadae walipatikana.
Mkuu hii habari yako ni hii hii au ni mpya maana habari haina chochote kinachohusu hii yakwako
 
” Ukimnyang’a askari silaha namna pekee ya kuipa hiyo silaha ni kwa kutumia silaha hivyo wanapaswa kuwa makini,” Kamanda Issah

Amemaanisha nini hapo huyo kamanda?
 
Back
Top Bottom