Njombe: CCM yachora alama ya umiliki katika nyumba ya mjane mwenye umri wa miaka 80

kilagalila

JF-Expert Member
Nov 8, 2018
320
154
Bibi mjane ambaye amefahamika kwa jina la TULAHUMBA KILAMILA mwenye umri wa miaka 80 na mama ambaye amejitambulisha kwa jina la DORICY MWINAMI mwenye miaka 46 wote wakazi wa kijiji cha ilembula wilayani wanging'ombe mkoani njombe wamekilalamikai chama cha mapinduzi ccm kwa kujumuisha nyumba zao kuwa ni mali za chama hicho.

Akizungumza na kituo hiki bibi huyo amesema kuwa hali hiyo imetokea pindi zoezi la uhakiki wa mali za chama hicho ukiendelea wilayani wanging'ombe ,ambapo ameshangazwa kuona nyumba yake ambayo ameijenga kwa ajili ya vibanda vya biashara ambayo amejenga kwenye eneo lake halali ambalo amelimiliki mwaka 1961 limejumuishwa kuwa ni mali ya chama hicho bila ufafanuzi wowote.

"Tulionaga maandishi tu mimi nimefika hapa tangu stini na moja tukanunua jengo hili tukanunua juu na chini sasa ilipofika 73 ulianza ujamaa wakaomba wajenge godauni akawapa wakajenga sehemu huku kwingine nikawa na lima ujamaa ukaisha wakapangisha mtu sasa tunaona juzi tena wameandika ccm mnisaidie jengo langu sasa wakati mimi najenga mlikuwa wapi"alizungumza bibi

Aidha DORICY MWINAMI amesema kuwa eneo hilo ni mali yao kwa kuwa awali walilianzimisha eneo hilo kwenye ofis za serikali kwa ajili ya ufugaji wa kuku lakini baada ya serikali kushindwa kuendeleza mradi huo eneo hilo lilirejeshwa kwao na mpaka sasa wanalimiliki lakini anashangazwa kuona chama hicho kwa sasa kinasema ni eneo lao.

Naye katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi (CCM) wilayani wanging'ombe REUBEN NYAGAWA amethibitisha kufanyika kwa zoezi hilo la uhakiki wa mali za chama hicho na kueleleza kuwa zoezi hilo linafuata taratibu zote kulingana na mali ambazo zipo kwenye orodha kwa makatibu wa chama hicho.

"ni kweli kuna zoezi la uhakiki wa mali za chama linaendelea kila kata na vijiji lakini kuna vitu ambavyo vinazingatiwa maana kulikuwa kuna watu kujitaifishia mali za chama cha mapinduzi na tunapofika kila eneo tumekuwa tukitoa elimu kwamba tunahakiki mali za chama kwa kuzingatia mwongozo na tumekuwa tukishirikisha wazee wale waasisi wa chama cha mapinduzi kwa hiyo kwa katibu wa chama kata tunaorodha za mali zote za chama kwahiyo tunajiridhisha kama mtu amejenga kwenye kiwanja cha chama basi huyo anakuwa amevamia eneo la chama"alisikika katibu Nyagawa

Hata hivyo katibu mwenezi huyo amesema kuwa licha ya zoezi hilo kufanyika lakini kwa baadhi ya maeneo ambayo wananchi washajenga nyumba za kuishi hawewezi kuhamishwa katika nymba zao ,japo kwa wale ambao wamejenga vibanda vya biashara katika maeneo ya chama hicho watapewa muda,Pindi fedha zao za ujenzi zitakapo patikana basi majengo hayo yatakuwa chini ya chama hicho.
MWISHO
mr.mtaani

SAUTI HIZI HAPA CHINI
 

Attachments

  • BANDA.MP3
    919.7 KB · Views: 18
  • BIBI.MP3
    950.5 KB · Views: 14
  • KATIBU .MP3
    856.1 KB · Views: 12
  • MAMA.MP3
    970.5 KB · Views: 14
Hivyo viwanja CCM walipewa na nani? Kwa utaratibu upi na wanavielelezo gani kuonyesha kiwa walilipa au kulipia hivyo viwanja? Hichi chama naona wameamua kuchukua vyao mapema kwa kuwa nwisho wao umefika
kutokea huko ujamaa:D:D
 
CCM haijawahi kumiliki mali yoyote kwa njia halali. Siku Ikiondolewa madarakani lazima mali zao zote zirudi kwa wananchi. CCM ni waporaji wa mali za wananchi na kodi zetu. Hata wakihakiki wanapoteza tu muda na kuturahisishia kazi ya kutaifisha.
 
Acha masikhara Mkuu, kipara kipya kajitoa CCM? Toka lini?
Sio kajitoa tuu, bali kamwambia mwnyekiti wao aache ubazazi. Wao wanamvesha nguo kumsitiri utupu lakini yeye anatupa kule nguo ilihali anakatiza katikati ya soko kuu saa saba mchana.
kipara kipya hataki ufala huo tena na sio ajabu sasa akawa yeye anashiriki kumvua nguo badala ya kumsetiri. Hakika amechukia sana hadi kipara kinatoa mvuke utadhani pasi ya mkaa
 
Duh
Kama aliwapa watumie.. kwanini wameandika kama mali yao?
Uchunguzi zaidi unatakiwa kufanyika.

Kutakuwa kuna majanga mengi basi nchini.. wengine labda hawajapata nafasi ya kuongea yao.


Ninachofahamu ni kuwa watu wa kule ni wakarimu sana na hasa kwa taasisi zinazohudumia jamii, inawezekana kabisa huyo mzee alitoa eneo kwa chama kwa nia njema ila hao viongozi ndiyo wamegeuza kitabu wanasoma upside down kwa interest zao binafsi, inafahamika wazi kuwa kuna sehemu nyingi yalofanyika hayo wakati wa cooperative unions, watu waliruhusu nyumba zao na maeneo yao kutumika for free
 
Duh
Kama aliwapa watumie.. kwanini wameandika kama mali yao?
Uchunguzi zaidi unatakiwa kufanyika.

Kutakuwa kuna majanga mengi basi nchini.. wengine labda hawajapata nafasi ya kuongea yao.
Hizo mali za kupora na nyingine CCM inazokalia kimabavu huwa inazilipia kodi? Hii kazi aliyopewa Dr. Bashiru ya kurudisha mali imemmaliza kabisa na falsafa zake za haki na ujamaa. Akitoka huko atakuwa kafungwa mdomo na hataweza kufungua tena mdomo wake milele...

CCM wabaya sana. Wakikuhitaji na hasa kama ulikuwa mpinzani au msemaji sana wanakupa kazi zilizo haramu na ambazo zitaharibu CV yako kwa kiwango kikubwa mno. Inahakilisha imekupaka tope, hata ukija kutoka huna pa kwenda na hakuna atakayekuamini.
 
Haaah! Haaaah! Haaaah! Haaah! Haaah!
Sio kajitoa tuu, bali kamwambia mwnyekiti wao aache ubazazi. Wao wanamvesha nguo kumsitiri utupu lakini yeye anatupa kule nguo ilihali anakatiza katikati ya soko kuu saa saba mchana.
kipara kipya hataki ufala huo tena na sio ajabu sasa akawa yeye anashiriki kumvua nguo badala ya kumsetiri. Hakika amechukia sana hadi kipara kinatoa mvuke utadhani pasi ya mkaa
 
Ninachofahamu ni kuwa watu wa kule ni wakarimu sana na hasa kwa taasisi zinazohudumia jamii, inawezekana kabisa huyo mzee alitoa eneo kwa chama kwa nia njema ila hao viongozi ndiyo wamegeuza kitabu wanasoma upside down kwa interest zao binafsi, inafahamika wazi kuwa kuna sehemu nyingi yalofanyika hayo wakati wa cooperative unions, watu waliruhusu nyumba zao na maeneo yao kutumika for free
nimekuelewa
 
Back
Top Bottom