Njombe: Biashara 148 Zimefungwa Ndani Ya Siku 90 - Manager Msaidizi TRA George Mapunda

Alexander The Great

JF-Expert Member
Aug 28, 2018
4,502
23,581
Habari Wana Jamvi,

Zaidi ya biashara 140 zimefungwa Njombe ndani za siku 90, kuanzia January 2021 mpaka March 2021, kutokana na sababu tofauti tofauti, miongoni mwao madeni na masoko kufa.

Kwa ufupi,

Taarifa hii imewekwa wazi na Manager Msaidizi Wa Mamlaka Ya Mapato Mkoa Wa Njombe, Bwana George Mapunda, katika kikao cha Ushauri Wa Mkoa kilichofanyika Njombe.

Amesema; Biashara nyingi sana zimefungwa ndani ya muda mfupi wa siku 90, kwasbabu ya wananchi kuwa na elimu ndogo juu ya ulipaji kodi, licha ya TRA kuwa na kitengo maalum cha Ushauri Kwa Walipa Kodi. Sambamba na kuwa na mikopo mibaya.

Nukuu; "Team kutoka Makao Makuu na hapa mkoani zimekua zikienda nyumba kwa nyumba kutoa elimu ya ulipaji kodi, wamekwenda Ludewa, Makambako na Njombe, na muendelezo bado upo, kwa madhumuni ya kuendelea kutoa elimu ya ulipa kodi kwa wananchi".

Amesema, biashara ndogo ndogo hutozwa kodi kwa kulingana na kumbukumbu za mauzo (Sales Record) ambayo ipo kisheria, kwa kutumia mashine za EFD wanauwezo wa kujua ni kiasi gani wanapaswa kulipa kama kodi stahiki.

Lakini, amesema kama mlipa kodi hato ridhika na makato ya kodi basi ana haki ya kwenda kupeleka malalamiko yake ngazi za juu, ili yafanyiwe kazi.

Amesema, nukuu; "Tuweke wazi, kwamba TRA haifungi biashara za watu, kuna watu wanadaiwa na TRA ila hatuwafungii biashara zao. Tunachofanya ni kuwaita na kuingia nao mikataba walipe madeni kwa awamu".

Nae RC wa Mkoa Wa Njombe, Engineer Marwa Rubirya, amewaasa TRA kufuata misingi na mapendekezo ya Rais Samia Suluhu kuhusiana na jinsi ya kukusanya kodi na mapato mengine.

Amesema, TRA wanapaswa kufuata taratibu na busara kwenye kukusanya kodi na kuwashawishi wananchi kulipa kodi kwa njia rafiki, sio kutumia nguvu na mabavu.

Amakweli "WAFANYABIASHARA (Wakubwa & Wadogo)" wameishi kama mashetani katika utawala wa Awamu Ya 5.

- Shukrani The Citizen.
maduka-data.jpg
 
Na bado...
Maana unaposikia KUONGEZA IDADI YA WALIPA KODI maana yake huyo huyo mtu mmoja atakuwa analipa mara nyingi mpaka kwenye maeneo ambayo awali alikuwa halipi kodi.

Mfano wenye nyumba mtaani wataanza kukatwa kodi wanapopokea kutoka kwa wapangaji wao.
 
Ukiona MTU anakodi fremu anafanya biashara muheshimu Sana.
Kweli Ma Mkubwa Wetu wa JamiiForums. Hujui huo mtaji wa biashara na kulipa fremu kajitoa vipi kuupata, wengine wanauza mpaka "UTU WAO (Nimetumia Tafsida Ma Mkubwa)" kupata mitaji.

Muheshimu sana, pengine katoa mpaka nyuma kusimamisha biashara katika fremu. Halafu TRA wanakuja kupiga kufuli la Solex. Hatari Ma Mkubwa.
 
Tanzania ina Kodi nyingi sana huenda kuliko Nchi yoyote Kusini mwa Jangwa la Saharawi
Tatizo ni Bunge La Job Ndugai Kupitisha Sheria Kandamizi, na TRA kutumia Mabavu Kuzitekeleza.

TRA kuanzisha EFD Machines ni jambo zuri sana kwenye kukusanya mapato, ila walikurupuka sana. Na sio kwamba hawafahamu au hawana uwelewa, bali wanajitia wazimu.

Zile mashine za EFD zinakadiria kodi kwa "MAUZO" ambayo mfanyabiashara anafanya, na sio kwamba zinakadiria kwa "FAIDA" mfanyabiashara anayopata.

Kodi huwezi ukatoza kwa mauzo mfanyabiashara anayofanya, kodi inatozwa kutokana na faida anayopata mfanyabiashara baada ya kutoa "GHARAMA ZA KUENDESHA BIASHARA".

Mfano,

Mfanyabiashara anaendesha biashara yake kwa Sh 100,000/= kwa mwezi (Gharama Za Umeme, Posho Kwa Vibarua, Fremu, Kununua Bidhaa, Usafiri), halafu kwa huo mwezi anauza mauzo ya Sh 150,000/=.

Wewe unaenda kumtoza kodi ya Sh 150,000/= ambayo inajumuisha mpaka gharama za kuendesha biashara hio. Badala uangalie gharama aliotumia ya Sh 100,000/= na uitoe kwenye mauzo yake ya Sh 150,000/= ndio umtoze kodi.

Ambayo inakua (Mauzo Ya Sh 150,000/=) kutoa kwenye (Gharama Ya Sh 100,000/=) unapata (Faida Ya Sh 50,000/=) ndio faida ya kutoza kodi.

Ukimtoza kodi kwa "MAUZO" badala ya "FAIDA" ni mwaka mmoja tu, mwaka wa pili lazima afunge biashara maana utakua umemkamua mpaka "MTAJI WAKE WOTE".

NOTE: Hata asilimia za kodi zipo juu sana sanaaaaaa pamoja na sheria ni kali na kandamizi nchi hii.
 
Kweli Ma Mkubwa Wetu JamiiForums. Hujui huo mtaji wa biashara na kulipa fremu kajitoa vipi kuupata, wengine wanauza mpaka "UTU WAO (Nimetumia Tafsida Ma Mkubwa)" kupata mitaji.

Muheshimu sana, pengine katoa mpaka nyuma kusimamisha biashara katika fremu. Halafu TRA wanakuja kupiga kufuli la Solex. Hatari Ma Mkubwa.
Issue wanunuaji, hela ikibana Sana binadamu ana Tabia ya kununua vya muhimu Tu. Sijui hii hali itatengemaa?. Magu aliharibu mzunguko WA fedha.
 
Kipindi kilichopita Wafanyabiashara wamepita kwenye njia Nyembamba sana..,
Yani Mtaji unakata unaushuhudia na Macho yako yani usipostuka mapema frem inabaki na leseni ya biashara na Tax payer certificate!
Unasubiri Giza totoro unarudi zako kufuta Jina na kubandua Matangazo, Sterling anakuwa amekufa kwenye Maua kama hivyo yani..,
 
Tatizo ni Bunge na TRA.

TRA kuanzisha EFD Machines ni jambo zuri sana kwenye kukusanya mapato, ila walikurupuka sana. Zile mashine zinakadiria kodi kwa "MAUZO" ambayo mfanyabiashara anafanya, na sio kwamba zinakadiria kwa "FAIDA" mfanyabiashara anayopata.
Kusema na ule ukweli hata parcentage za kodi ziko juu sana

Halafu huduma za Jamii ziko chini sana
 
Kipindi kilichopita Wafanyabiashara wamepita kwenye njia Nyembamba sana..,
Yani Mtaji unakata unaushuhudia na Macho yako yani usipostuka mapema frem inabaki na leseni ya biashara na Tax payer certificate!
Unasubiri Giza totoro unarudi zako kufuta Jina na kubandua Matangazo, Sterling anakuwa amekufa kwenye Maua kama hivyo yani..,
Acha nimesikia Benki moja ya walala Hoi imesitisha mikopo Kwa wajasiliamali, Lawama, unachukua fedha baada ya muda inakata yote. Wamebaki na wafanyakazi Tu.
 
Tra wajipange upya na wakae na wafanyabiashara waangalie namna boravya kodi,maana kofi ndio injini ya uchumi,wafanye zaiara nchi jirani kama Malawi na Zambia,hawana bandari,lakini wafanyabiashara wetu wanakimbilia kuwekeza huko!Ni hatari kweli.
 
Tatizo ni Bunge na TRA.

TRA kuanzisha EFD Machines ni jambo zuri sana kwenye kukusanya mapato, ila walikurupuka sana. Na sio kwamba hawafahamu au hawana uwelewa, bali wanajitia wazimu.

Zile mashine za EFD zinakadiria kodi kwa "MAUZO" ambayo mfanyabiashara anafanya, na sio kwamba zinakadiria kwa "FAIDA" mfanyabiashara anayopata.

Kodi huwezi ukatoza kwa mauzo mfanyabiashara anayofanya, kodi inatozwa kutokana na faida anayopata mfanyabiashara baada ya kutoa "GHARAMA ZA KUENDESHA BIASHARA".

Mfano,

Mfanyabiashara anaendesha biashara yake kwa Sh 100,000/= kwa mwezi (Gharama Za Umeme, Posho Kwa Vibarua, Fremu, Kununua Bidhaa, Usafiri), halafu kwa huo mwezi anauza Sh 150,000/=.

Wewe unaenda kumtoza kodi ya Sh 150,000/= ambayo inajumuisha mpaka gharama za kuendesha biashara hio. Badala uangalie gharama aliotumia ya Sh 100,000/= na uitoe kwenye mauzo yake ya Sh 150,000/= ndio umtoze kodi.
VAT haimuhusu mfanyabiashara ni jambo ambalo mfanyabiashara aongeze bei ya bidhaa
 
Daaah ni noma sana lakini watakuwepo tu wanaokwepa,,hivi hapa EA ni nchi zipi ambazo investment inaeza kuwa afadhali kdg maana APA kwetu ni ghasia ase
Uganda ni namba moja halafu kuna Bunia Kongo

Huko Kongo kuna swahiba kaenda siku Magu alipoingia 2016 sasa hivi anapeleka anapeleka Semi mbili za Mahogany na Red Wood China na Falme za kiarabu kila mwezi

Kaongeza na mke wa pili wa Kinyankole
 
Uganda ni namba moja halafu kuna Bunia Kongo

Huko Kongo kuna swahiba kaenda siku Magu alipoingia 2016 sasa hivi anapeleka anapeleka Semi mbili za Mahogany na Red Wood China na Falme za kiarabu kila mwezi

Kaongeza na mke wa pili wa Kinyankole
nimependa msisitizo wako eti kuongeza mke wa pili,hii n kwamba matunda yanaonekana au sio
 
Back
Top Bottom