Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
Mahakama ya Wilaya ya Ludewa imemhukumu kifungo cha miaka 5 jela John Chale(60) mkazi wa kata ya Ilela wilayani Ludewa mkoani Njombe kwa kosa la kumfanyia vitendo vya kishirikina mtoto wa mdogo wake Videana Chale(18) na kupelekea kupata ukichaa.
Akisomewa hukumu hiyo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya Ludewa Isaac Ayengo imeelezwa kuwa binti huyo alipatwa na kichaa ambapo wazazi wake walimpeleka kwa mganga wa kienyeji ndipo walipoambiwa kuwa amerogwa na mshtakiwa huyo.
Lakini hawakuishia hapo walimpeleka kanisani nako ikagundulika hivyo pia ndipo walipoamua kumuuliza mshtakiwa huyo kwakuwa amekuwa na tabia ya vitendo vya kishirikina na anamiliki nyoka ndani ya nyumba yake ambaye kwa macho ya kawaida amekuwa akionekana kama jiwe.
Aidha mshtakiwa huyo alikiri kutenda kosa hilo ndipo baba mzazi wa mtoto huyo Hekima Chale akaamua kupeleka jambo hilo katika vyombo vya sheria ambako mtuhumiwa huyo alikana lakini baada ya kufanyika upelelezi na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili mahakama ilijilidhisha kuwa yeye ndio ametenda kosa hilo.
Mwendesha mashtaka wa serikali aliiomba Mahakama kumpatia mshitakiwa adhabu kali ili iwe fundisho kwake na jamii kwa ujumla kwani vitendo vya kishirikina vinasababisha migogoro ya familia na jamii kwa ujumla na kupelekea mauaji na baada ya hoja hizo Mahakama imeamuru mshitakiwa kutumikia kifungo cha Miaka 5 gerezani.
Source: Issa Michuzi
Akisomewa hukumu hiyo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya Ludewa Isaac Ayengo imeelezwa kuwa binti huyo alipatwa na kichaa ambapo wazazi wake walimpeleka kwa mganga wa kienyeji ndipo walipoambiwa kuwa amerogwa na mshtakiwa huyo.
Lakini hawakuishia hapo walimpeleka kanisani nako ikagundulika hivyo pia ndipo walipoamua kumuuliza mshtakiwa huyo kwakuwa amekuwa na tabia ya vitendo vya kishirikina na anamiliki nyoka ndani ya nyumba yake ambaye kwa macho ya kawaida amekuwa akionekana kama jiwe.
Aidha mshtakiwa huyo alikiri kutenda kosa hilo ndipo baba mzazi wa mtoto huyo Hekima Chale akaamua kupeleka jambo hilo katika vyombo vya sheria ambako mtuhumiwa huyo alikana lakini baada ya kufanyika upelelezi na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili mahakama ilijilidhisha kuwa yeye ndio ametenda kosa hilo.
Mwendesha mashtaka wa serikali aliiomba Mahakama kumpatia mshitakiwa adhabu kali ili iwe fundisho kwake na jamii kwa ujumla kwani vitendo vya kishirikina vinasababisha migogoro ya familia na jamii kwa ujumla na kupelekea mauaji na baada ya hoja hizo Mahakama imeamuru mshitakiwa kutumikia kifungo cha Miaka 5 gerezani.
Source: Issa Michuzi