Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 209
- 351
NJIA PANDA YA VWASU (Simulizi ya Huba)
DAVID NGOCHO SAMSON
0629077792
01
Naikumbuka vema ile siku. Alinipigia simu, nami nikaipokea kwa bashasha na furaha tele. Huyu alikuwa mpenzi wangu, mwanamke aliyenipa raha mara nyingi.
'Mambo vipi mpenzi? Uliona email niliyokutumia? Nilikujulisha kuwa narejea nchini, kwa bahati mbaya sijapata tena nafasi ya kucheki kama ulijibu. Kuna mambo fulani fulani yalitokeza na kukatisha mawasiliano. Ajabu napowaza kukupandia hewani, unaniwahi na hii call. I miss you babe!' niliongea kwa sauti ya furaha.
Kawaida, mimi hutabasamu kabla hata ya kusikia sauti ya Hellen, yaani ile nikiona kwenye kioo cha simu yangu jina 'Hellen', basi moyo wangu hufukuta kwa fukuto la furaha, hata kama ningekuwa na huzuni, mie huisahau mara moja hadi pale nitakapomaliza mazungumzo.
Kwa nini sijasevu jina la Hellen kwa mbwembwe za 'my love', au 'Honey' au 'laaziz' unajiuliza eh?! Utafahamu hapo baadaye, lakini yeye Hellen anajua kwa nini jina lake nimelisevu kavu. Sasa basi, naweza kusema, ingawa tupo kwenye mahusiano kwa karibia miezi minne sasa, lakini ukiniona navyotabasamu kumuona Hellen, basi unaweza kukokotoa na kupata jawabu la uongo. Ndiyo, la uongo.
Utajua tu kwamba huyu jamaa, ndiyo kwanza kamuona huyu binti na amemzimikia kinoma. Kawaida pumbazo langu la kwanza nilipokutana na Hellen mara ya kwanza miezi mitatu iliyopita, basi limekuwa likibaki hivyo hivyo hata sasa baada ya miezi hii yote napomuona tena. Aisee! Huyu binti kajua kunishika. Mie zuzu wallah.
Basi, nilipomaliza kumweleza maneno hayo, nilisubiri kwa hamu niisikie sauti ya mpenzi wangu, ambayo kuisikia pekee, hunipatia burudani nafsini mwangu.
'Niliiona Derrick, na nimeshaijibu. Uko wapi?' Hellen Alizungumza kwa sauti tulivu. Sauti ambayo sikuizoea. Haikuwa na ule uchangamfu wa siku zote. Najua haikuwa nao, japo alijaribu kuongea kwa kuniigizia. Namjua mpenzi wangu bwana huwezi kunidanganya kitu. 'Hellen wangu ana shida gani jamani!'. Nilijiuliza. Ah, sikuvumilia kubaki najiuliza tu, nikaamua kuondoa hilo dukuduku moyoni mwangu.
'Vipi dear, mbona umepoa hivyo mpenzi? Kunani tena darling. Eh mamii, are you sick mpenzi?' nililazimika kuhoji, ile furaha yangu ikiyeyuka kama donge la barafu kwenye joto kali. Aisee, sio siri, niambie habari gani sijui, lakini habari za huzuni hunibeba sana mimi. Nadhani, huu ni udhaifu kwangu mimi mtoto wa kiume, kuwa na hisia nzito sana.
Ni mwepesi sana wa furaha na huzuni vile vile. Ndio maana najaribu kusoma soma masuala ya kisaikolojia, kunisaidia kuwatambua matapeli mapema. Si unafahamu matapeli wanacheza sana na hisia! Naam, matapeli buana wakikujua wewe' ni mtu unayepata huzuni ukielezwa tukio la kuhuzunisha, matapeli ni wepesi sana kupita humo, wakakulisha habari ya msiba, ukajikuta unachangia nauli ya kwenda msibani kwa kuwaonea huruma, kutokana na matatizo chungu nzima watakayokuorodheshea.
Huzuni iliyokuwa moyoni mwangu, kusikia tu ukosefu wa uchangamfu kwenye sauti ya Hellen, ungedhani nimepashwa habari za msiba.
'Siku hazilingani mpenzi, hata hivyo kiafya niko poa tu sema nimekumiss. Kama tunaweza kuonana itakuwa poa sana. Nahitaji tuongee!' Hellen alizungumza kwa utulivu ule ule.
'Ok dear, nipo Changanyikeni now. Nije au uje?' nilimtupia swali japo ilikuwa wazi kwamba alinihitaji niende. Kikawaida akihitaji kuja kwangu, yeye huja baada ya kujibiwa message yake ya neno moja ambayo ni mimi tu naielewa 'Hr301'. Hiki ni kifupisho cha moja ya kozi ambazo zilitukutanisha mimi na Hellen miezi mitatu iliyopita. Usijali. Nitakuelezea. Najua unataka ujue ilikuwa vipi.
Kwa kawaida, vyuoni kozi huwa zinakuwa na majina ya vifupisho. Mfano hiyo Hr inasimama badala ya kozi ya 'human rights' (Haki za binadamu …) na hiyo 301, Sina hakika lakini nahisi ilimaanisha mwaka wa masomo. Maana kulikuwa pia hr101 iliyofundishwa mwaka wa kwanza, hr 201 ilifundishwa mwaka wa pili. So nahisi kabisa hiyo ndio ilikuwa maana yake, yaani mwaka wa tatu.
Hellen yeye amesoma kozi ya Archaeology, na mimi nilisomea kozi ya Political Science and Public Administration. Kwa hiyo, tulikuwa kozi mbili tofauti kabisaa na ndiyo maana tulikuja kufahamiana mwaka wa tatu. Ajabu ni kuwa, kwenye semester ya pili ya mwaka wa Mwisho wa masomo yetu, mimi niliamua kuongezea kozi hii ya human rights, kama kozi ya ziada tu. Haikuwa lazima kuisoma, kumbe naye, aliamua kufanya hivyo tusijue kama ndio kitu kingetukutanisha.
Mimi ni mtu mmoja ambaye, napenda kubeba majukumu yangu kwa mikono miwili, tena kwa umakini wa kiwango cha juu kabisa. Na hii naweza kukudhihirishia kwa mambo ninayoamua kufanya, ni lazima nione yamekamilika, ndio naweza kurelax. Sasa basi, kwenye hiyo kozi, nikajikuta nimepangwa semina moja na Hellen. Halafu tena, tukapewa group assignment (kazi ya kikundi) watu kumi, mimi na yeye tukiwa miongoni mwa wanakikundi.
Shida ikawa moja, wadau wote niliopangwa nao, ama walikuwa wapuuziaji wa mambo au walikuwa na mishe nyingine muhimu kuliko shule. Watu hawa, tulipokubaliana muda wa kukutana kwa ajili ya kujadiliana na kutafuta majibu ya kazi tuliyopewa, hawakuonekana. Nikajikuta peke yangu eneo la tukio. Bahati mbaya sana ilikuwa kwenye kikao hicho ndio tukabidhiane mawasiliano kwa ajili ya kupeana taratibu na yanayojiri mengine.
Kitu nilichokuja kubaini baadaye, ni kwamba wale wanakikundi wenzangu, kila mmoja kwa wakati wake, alikuwa anajidanganya kwamba ni yeye pekee hajahudhuria kwenye majadiliano, na hivyo kujitia moyo kwamba hakuna kitakachoharibika. Lo! Walijidanganya sana. Baada ya hali kuwa hivyo, basi nikalivalia njuga suala hilo mimi mwenyewe, nikaanza kuandika kazi ile mimi mwenyewe kwa juhudi kubwa. Uzuri ni kwamba, kwa mfumo wa zile semina za chuoni, kwenye uwasilishaji hoja, angeweza kuteuliwa mmoja akatoa wasilisho lote kwa niaba ya kundi lote, huku wale wengine wakisaidiana naye kujibu hoja ambazo zingeibuliwa kwenye mjadala wa pamoja. Hivyo, nikaamua kuwa jeshi la mtu mmoja.
Hali hii haikuwa ya kwanza kuwahi kutokea, nilikwishakutana na visa vya namna hii mara kadhaa, sema hii ilitia fora. Awali nilikuwa nakutana na watu wachache au wengi, wakakosekana baadhi. Lakini hii ilikuwa mara ya kwanza wote kukosekana. Sikujali. Kwanza kabisa, mimi najijua, napenda sana kufanya uwasilishaji, hivyo hata kama ingekuwaje, tuseme kwa mfano angelichaguliwa muwasilishaji mwingine, bado ningelijiandaa kama vile mimi ndio muwasilishaji mkuu. Ndiyo. Kila mtu na ulevi wake bwana, na mimi wangu ulikuwa huu wa kupigiwa makofi na kupewa sifa kwa uwasilishaji bora na wahadhiri au ma-tutor. So kusema kweli, nilijiandaa vema kwa nondo za uhakika.
Siku ya uwasilishaji, mimi nilienda kwenye semina kama kawaida kwa muda uliopangwa. Kumbe bwana, wale jamaa zangu, kwa kutaka angalau wapate point mbili za kujitetea nazo ikitokea wametakiwa kutoa hoja, waliwahi nusu saa kabla ili wakutane na wahusika wengine, wadandie points. Hali ikawa ngumu pale wote tisa walipojikuta hakuna hata mmoja aliyehudhuria kwenye majadiliano. Kimbembe kikawakumba. Wakaanza kuhaminika. Wajadiliane, waandike, wawasilishe, na bado kazi hiyo ilihitaji kukusanywa ikiwa imechapwa!. Niliwakuta jamaa wameloa jasho wakihangaika.
Ilikuwa dakika tano hivi kabla ya muda wa wasilisho kufanyika. Dah walikuwa wamejikatia tamaa vibaya sana. Mwanaume nikaingia kwa mbwembwe na kabrasha zangu kwenye begi utadhani waziri wa fedha anaenda kusoma bajeti bungeni.
'Oya waungwana, muda wa kuingia kwenye semina huu. Vipi bado mnagaagaa na upwa?' Nikawauliza.
'Hivi si tupo wote wewe?' Aliniuliza jamaa mmoja anaitwa Stanley.
'Yeah man, twendeni tukawasilishe wazee!' niliwaambia.
'Vipi mwanangu uliandaa wasilisho?' akaniuliza tena.
'Haya ndio mambo niliyofuata hapa mlimani. Hebu njoeni hapa wadau, tuwekane sawa kabisa.' nilitamka kwa sauti kubwa yenye mamlaka. Najua kwa wakati huo walikuwa tayari kunisikiliza kwa hamu zote, si nimekuja kuokoa chombo kisiende mrama? Basi wakanisogelea wakiwa watulivu kama vifaranga walionyeshewa. Nikawaangalia nyuso zao zilivyotia huruma, basi nikacheka sana kimoyomoyo.
'Waungwana, tumefeli sana kwenye kipengele cha uungwana, fikiria wote mlikimbia majadiliano na kuniachia mzigo wote nibebe mimi?' nilivyotamka hivyo nikaona nyuso zao zikipata nuru ya tumaini jipya. Kwa sababu walau walipata uhakika kwamba kutakuwa na kazi ya kakabidhiwa kwa profesa.
'Sasa. Hapa nimeshaandaa nondo, nina uhakika wa asilimia mia wa kuwapatieni A ya bure. Lakini mnatakiwa mfahamu kuwa, nimetumia muda na gharama. Hapa tunafanya changisho, ndio unapata fursa ya kusaini jina lako kwenye wasilisho. Kila mmoja anachanga buku mbili. Tufanye fasta, naona bado dakika tatu tuingie kwenye semina.' niliongea kwa kujiamini sana nikiwa nimevalia sura ya kazi. Hakuna aliyebisha. Nikazikusanya buku mbili mbili, tukazama darasani.
Kama kawaida yangu, kumbuka nimekueleza huu ndio ulevi wangu. Muda wa wasilisho ulipofika, nilikabidhi nakala ya wasilisho kwa msimamizi wa semina yetu. Profesa Nkungu, halafu nikaanza mbwembwe zangu za uwasilishaji hoja. Huu ndio uwanja naofanyaga mambo yangu, basi nikawa nipo namwaga sera zangu huku nikishuhudia zinavyowaingia wadau. Nikamuona profesa anatikisa kichwa juu chini kukubaliana na hoja zangu. Nilipoweka kituo baada ya wasilisho, chumba kizima walikuwa wanapiga makofi. Kwangu ilikuwa burudani kabisa. Wale jamaa zangu hawakuamini. Niliwapatia alama A Kama nilivyowaahidi. Profesa akasifia sana kundi letu.
Basi, tulivyotoka kwenye semina, nikiwa naondoka mdogo mdogo kuelekea kwenye vimbweta nikaperuzi peruzi notes zangu. Nikasikia sauti nyuma yangu. 'Derrick'. Ilikuwa sauti laini, sauti ya kike. Ikanilazimu kusimama na halafu nikageuka nyuma, maana chuoni kuna watu wengi na wakina Derrick sikuwa mimi pekee.
'Naomba nisubiri tafadhali' yule msichana alitamka. Nikakumbuka Ni miongoni mwa wale wanakikundi niliowatoza shilingi elfu mbili mbili.
'Mimi?' niliuliza kwa kutojiamini.
'Ndio, wewe si Derrick?' akatamka kwa ulizo.
'Ndio, lakini kwenye chuo kinachosajili maelfu ya wanafunzi huwezi kudhani utakuwa mtu pekee mwenye jina kama lako, sivyo? Nilimweleza.
'Sawa, upo sahihi nadhani.' alitamka yule mrembo.
'Haina kudhani hiyo, ndio uhalisia wa mambo' nikamuhakikishia.
'Kuna hoja unashindwa kujibu kweli?' mrembo huyu aliniuliza.
'Ah hayo masihara sasa. Of course kila hoja inaweza kujibiwa. Kwa kukubaliwa au kupingwa' nilimwambia halafu nikaongezea.
'Pale palikuwa na Helen, Mwajuma, Aisha na Doris, wewe utakuwa nani kati yao?' niliuliza nikiwa nimetaja majina ya wasichana ambao walikuwa sehemu ya kundi langu la wasilisho.
'Tabiri!' alinambia akiwa anatabasamu.
'Haha, mie si Sheikh Yahya bwana. Lakini kwa vile umenipa cheo hicho, wacha nijaribu, kwani nikikosea kuna hukumu?' akatikisa kichwa kulia na kushoto kumaanisha hakuna hukumu. Nami nikaamua kwenda na jina la kwanza.
'Hellen' nikatamka bila kupepesa jicho.
'Nilijua unafahamu, sema Unataka kuniigizia tu!'
'Haha' nikajichekea zangu. Sikufahamu jina lake, lakini sikuona kwa nini nisitumie lift hii niliyokua napewa bure, ya kufahamu nisichofahamu.
'Enhe nambie Hellen, wewe na wenzio mna tabia mbaya sana. Mbona mkaniachia kazi peke yangu' sikuwa na hoja na kulikuwa kumepita ukimya wa sekunde kadhaa kati yetu, hivyo nikaona niongee kauli hiyo kufufua mjadala. Huwa sipendi nikiwa na mtu kuwe na ukimya kati yetu, hasa kama ni jinsia ya kike. Kuepuka kutongoza, basi mimi huanza kuleta simulizi za kutunga za uongo na kweli ili kuepuka ukimya. Mara nyingi, nautafsiri ukimya kama mlango wa kuruhusu mwenzako aingie moyoni mwako na kuibua hisia za mapenzi.
Sio kwamba sipendi kutongoza. La hasha! Ni kwamba, ili kudumisha nidhamu binafsi, sipendi niwe kwenye mahusiano na msichana tunayeonana kila mara. Yaani darasani, kwenye semina, canteen na maeneo ya chuoni. Ndiyo maana niliamua kuwa na mahusiano na msichana ambaye anasoma chuo kishiriki cha chuo kikuu Cha Dar es salaam, kampasi ya Duce - Chang'ombe. Anaitwa Welu.
Hii Ina maana kwamba, tulikuwa tunaonana wikend tu na mara moja moja kati kati ya wiki. Kwangu mimi, hiyo ni heshima. Kuna kumisiana na kutarajiana kunakoamsha penzi na kulifanya liwe kileleni muda wote. Pia inaepusha migongano na migogoro midogo midogo inayoyumbisha penzi kama vile wivu pale unapomuona mwenzio anazungumza na mtu wa jinsia yako, halafu ukajikuta unaanzisha zogo. Inakuwa utoto, maana mara kadhaa nimeshuhudia washkaji wanatandikwa mbele ya mademu zao kwa sababu hizo za wivu. Kukaa unaumia moyoni kwa sababu unajikuta umejipachika ukachero wa kumfuatilia mwenzio nyendo zake, kama vile yeye ni mtoto asiyejua anachofanya.
Mara unaanzisha zogo na shemeji pasipokujua, au mrembo wako anazungumza masuala tofauti, unahisi Ni mapenzi unajitosa umuoneshe umwamba huyo jamaa, halafu unatoka hapo umevimbwa midomo au umepasuliwa komwe. Hayo ndio mambo naepuka kwa kuwakwepa warembo wa kuonana kila mara. Shida kubwa ni kwamba, hujijui kama una wivu,na hata unapofuatilia mambo yake, unakuwa pia hujui kwamba ndio umeanza upelelezi. Unajikuta mtumwa wa mpenzio bila kujua. Ah, hayo mie siyataki kabisa.
'Dah, ungejua ungenipa pole mwenzio!' Hellen aliongea kwa unyonge. Ah, kama nilivyokueleza awali, nina wepesi sana wa kubebwa kihisia. Ndio maana, kusema kweli, sipendi kusikiliza simulizi za huzuni, najikuta tu navutwa makini, na hali hiyo huniondolea mudi ya furaha. Mimi napenda habari za furaha, hizo tu, basi. Sasa, ajabu ni kuwa mtu akinijia na simulizi ya huzuni najikuta namsikiliza huku nikibebwa kihisia utadhani suala husika linanihusu.
'Oh Pole sana Hellen.' nilitamka huku nikiingiza mkono kwenye mfuko wa suruali yangu na kuchomoa wallet.
'Naamini sijakutendea haki kuchukua buku mbili zako, bila kujali ulikuwa na madhila gani. Tafadhali nisamehe.' niliongea huku nachomoa elfu mbili kwenye wallet na kumkabidhi Hellen.
'What?? Noo Derrick, Noo! Actually nimekufuata kutaka kukushukuru kwa jinsi ulivyookoa jahazi. Mimi napenda sana kushiriki kwenye discussion. Siku ile nilipata dharura, kulikuwa na kikao cha harusi na mimi nilikuwa nahusika kwa sehemu kubwa, so nikakosa namna ya kuomba udhuru, hivyo nikalazimika kukosa.'
'Ah, that's better now. Unajua hakuna kitu kinachoumiza kama kuwa-taken advantage of (kuchukuliwa poa) kwa sababu ya matatizo yako. Kwa hiyo, ulivyoanza kwa kusema nikupe pole, nikajua itakuwa tu ulikumbwa na matatizo. Haha, kwa hiyo anaolewa dada au unapata wifi?' nikauliza kwa utani. Nikaona kama Hellen alishituliwa na swali langu, au kuna namna swali hilo lilimuondolea Hali ya kujisikia amani (comfortability).
'Haha, forget about that. Derrick, I love your way of doing things. ( Sahau kuhusu hilo, napenda sana unavyokunyanyasa mambo yako) Jinsi ulivyoshushasha nondo mle ndani najisikia kukutoa out, lakini shida ni moja tu. Natakiwa tena kwenye kikao cha wajasiriamali mjini. So, please accept this as my gesture of appreciation (tafadhali pokea hii kama shukrani na hongera yangu) .' Hellen aliongea huku akinikabidhi noti ya shilling elfu kumi. Wow! Nikabaki nashangaa. Nikawa sina neno la kusema. Hata kusema asante nikasahau.
'Do you mind if I had your phone number?' (naweza kupata namba yako?) Hellen aliniuliza akiniangalia kwa jicho fulani hivi! Sauti hiyo ikanitoa kwenye pumbazo la muda nilikokuwa nimetopea.
'Hellen' nikatamka nikiwa nimekumbatia viganja vyake kwenye viganja vyangu.
'Asante sana, lakini neno tu la shukrani linatosha. Huna haja ya kulipia. You are a nice person. Please keep the money, ok. I appreciate your appreciation.' (Wewe ni mtu poa sana. Hata hivyo, siwezi kupokea fedha yako. Jua tu, nimekubali kunibali kwako) niliongea kwa sauti tulivu. Sauti ya kunong'ona. Huenda kuna namna sauti hii iliamsha kitu ndani yake.
'My numbers are ….. ' nikaanza kumtajia namba zangu, lakini nikasikia sauti yake ikisema
'Wait a minute' (subiri kwanza) nikalazimika kutulia wakati akichomoa simu yake kwenye mkoba. Ilikuwa tablet moja amazing. Well, mimi nilikuwa na kismart changu cha tekno, fresh tu!
'Ok, nitajie' alitamka tena Hellen.
'07174117..' nikamtajia na yeye akaziandika kwenye simu yake. Sekunde kadhaa mbele nikasikia kimeo changu kinaita.
'That's my number' akatamka. Halafu akaniambia
'Sasa, mie niwahi bwana!' Ni kama sikusikia, lakini nilimsikia, sema tu kuna namna huyu dada Hellen alikuwa ananipumbaza kwa sauti yake tamu. Nikiwa nimeganda sijui cha kusema, nikashitukia Hellen amenibusu shavuni halafu yule ananipungia mkono akiwa anaondoka. Nikabaki nimeduwaa. Napopata akili ya nini hasa kimetokea, Hellen alikuwa keshapotea kwenye upeo wa macho yangu. Kama vile bwege, nikabaki napunga hewani mikono yangu.
David Ngocho Samson
2020
DAVID NGOCHO SAMSON
0629077792
01
Naikumbuka vema ile siku. Alinipigia simu, nami nikaipokea kwa bashasha na furaha tele. Huyu alikuwa mpenzi wangu, mwanamke aliyenipa raha mara nyingi.
'Mambo vipi mpenzi? Uliona email niliyokutumia? Nilikujulisha kuwa narejea nchini, kwa bahati mbaya sijapata tena nafasi ya kucheki kama ulijibu. Kuna mambo fulani fulani yalitokeza na kukatisha mawasiliano. Ajabu napowaza kukupandia hewani, unaniwahi na hii call. I miss you babe!' niliongea kwa sauti ya furaha.
Kawaida, mimi hutabasamu kabla hata ya kusikia sauti ya Hellen, yaani ile nikiona kwenye kioo cha simu yangu jina 'Hellen', basi moyo wangu hufukuta kwa fukuto la furaha, hata kama ningekuwa na huzuni, mie huisahau mara moja hadi pale nitakapomaliza mazungumzo.
Kwa nini sijasevu jina la Hellen kwa mbwembwe za 'my love', au 'Honey' au 'laaziz' unajiuliza eh?! Utafahamu hapo baadaye, lakini yeye Hellen anajua kwa nini jina lake nimelisevu kavu. Sasa basi, naweza kusema, ingawa tupo kwenye mahusiano kwa karibia miezi minne sasa, lakini ukiniona navyotabasamu kumuona Hellen, basi unaweza kukokotoa na kupata jawabu la uongo. Ndiyo, la uongo.
Utajua tu kwamba huyu jamaa, ndiyo kwanza kamuona huyu binti na amemzimikia kinoma. Kawaida pumbazo langu la kwanza nilipokutana na Hellen mara ya kwanza miezi mitatu iliyopita, basi limekuwa likibaki hivyo hivyo hata sasa baada ya miezi hii yote napomuona tena. Aisee! Huyu binti kajua kunishika. Mie zuzu wallah.
Basi, nilipomaliza kumweleza maneno hayo, nilisubiri kwa hamu niisikie sauti ya mpenzi wangu, ambayo kuisikia pekee, hunipatia burudani nafsini mwangu.
'Niliiona Derrick, na nimeshaijibu. Uko wapi?' Hellen Alizungumza kwa sauti tulivu. Sauti ambayo sikuizoea. Haikuwa na ule uchangamfu wa siku zote. Najua haikuwa nao, japo alijaribu kuongea kwa kuniigizia. Namjua mpenzi wangu bwana huwezi kunidanganya kitu. 'Hellen wangu ana shida gani jamani!'. Nilijiuliza. Ah, sikuvumilia kubaki najiuliza tu, nikaamua kuondoa hilo dukuduku moyoni mwangu.
'Vipi dear, mbona umepoa hivyo mpenzi? Kunani tena darling. Eh mamii, are you sick mpenzi?' nililazimika kuhoji, ile furaha yangu ikiyeyuka kama donge la barafu kwenye joto kali. Aisee, sio siri, niambie habari gani sijui, lakini habari za huzuni hunibeba sana mimi. Nadhani, huu ni udhaifu kwangu mimi mtoto wa kiume, kuwa na hisia nzito sana.
Ni mwepesi sana wa furaha na huzuni vile vile. Ndio maana najaribu kusoma soma masuala ya kisaikolojia, kunisaidia kuwatambua matapeli mapema. Si unafahamu matapeli wanacheza sana na hisia! Naam, matapeli buana wakikujua wewe' ni mtu unayepata huzuni ukielezwa tukio la kuhuzunisha, matapeli ni wepesi sana kupita humo, wakakulisha habari ya msiba, ukajikuta unachangia nauli ya kwenda msibani kwa kuwaonea huruma, kutokana na matatizo chungu nzima watakayokuorodheshea.
Huzuni iliyokuwa moyoni mwangu, kusikia tu ukosefu wa uchangamfu kwenye sauti ya Hellen, ungedhani nimepashwa habari za msiba.
'Siku hazilingani mpenzi, hata hivyo kiafya niko poa tu sema nimekumiss. Kama tunaweza kuonana itakuwa poa sana. Nahitaji tuongee!' Hellen alizungumza kwa utulivu ule ule.
'Ok dear, nipo Changanyikeni now. Nije au uje?' nilimtupia swali japo ilikuwa wazi kwamba alinihitaji niende. Kikawaida akihitaji kuja kwangu, yeye huja baada ya kujibiwa message yake ya neno moja ambayo ni mimi tu naielewa 'Hr301'. Hiki ni kifupisho cha moja ya kozi ambazo zilitukutanisha mimi na Hellen miezi mitatu iliyopita. Usijali. Nitakuelezea. Najua unataka ujue ilikuwa vipi.
Kwa kawaida, vyuoni kozi huwa zinakuwa na majina ya vifupisho. Mfano hiyo Hr inasimama badala ya kozi ya 'human rights' (Haki za binadamu …) na hiyo 301, Sina hakika lakini nahisi ilimaanisha mwaka wa masomo. Maana kulikuwa pia hr101 iliyofundishwa mwaka wa kwanza, hr 201 ilifundishwa mwaka wa pili. So nahisi kabisa hiyo ndio ilikuwa maana yake, yaani mwaka wa tatu.
Hellen yeye amesoma kozi ya Archaeology, na mimi nilisomea kozi ya Political Science and Public Administration. Kwa hiyo, tulikuwa kozi mbili tofauti kabisaa na ndiyo maana tulikuja kufahamiana mwaka wa tatu. Ajabu ni kuwa, kwenye semester ya pili ya mwaka wa Mwisho wa masomo yetu, mimi niliamua kuongezea kozi hii ya human rights, kama kozi ya ziada tu. Haikuwa lazima kuisoma, kumbe naye, aliamua kufanya hivyo tusijue kama ndio kitu kingetukutanisha.
Mimi ni mtu mmoja ambaye, napenda kubeba majukumu yangu kwa mikono miwili, tena kwa umakini wa kiwango cha juu kabisa. Na hii naweza kukudhihirishia kwa mambo ninayoamua kufanya, ni lazima nione yamekamilika, ndio naweza kurelax. Sasa basi, kwenye hiyo kozi, nikajikuta nimepangwa semina moja na Hellen. Halafu tena, tukapewa group assignment (kazi ya kikundi) watu kumi, mimi na yeye tukiwa miongoni mwa wanakikundi.
Shida ikawa moja, wadau wote niliopangwa nao, ama walikuwa wapuuziaji wa mambo au walikuwa na mishe nyingine muhimu kuliko shule. Watu hawa, tulipokubaliana muda wa kukutana kwa ajili ya kujadiliana na kutafuta majibu ya kazi tuliyopewa, hawakuonekana. Nikajikuta peke yangu eneo la tukio. Bahati mbaya sana ilikuwa kwenye kikao hicho ndio tukabidhiane mawasiliano kwa ajili ya kupeana taratibu na yanayojiri mengine.
Kitu nilichokuja kubaini baadaye, ni kwamba wale wanakikundi wenzangu, kila mmoja kwa wakati wake, alikuwa anajidanganya kwamba ni yeye pekee hajahudhuria kwenye majadiliano, na hivyo kujitia moyo kwamba hakuna kitakachoharibika. Lo! Walijidanganya sana. Baada ya hali kuwa hivyo, basi nikalivalia njuga suala hilo mimi mwenyewe, nikaanza kuandika kazi ile mimi mwenyewe kwa juhudi kubwa. Uzuri ni kwamba, kwa mfumo wa zile semina za chuoni, kwenye uwasilishaji hoja, angeweza kuteuliwa mmoja akatoa wasilisho lote kwa niaba ya kundi lote, huku wale wengine wakisaidiana naye kujibu hoja ambazo zingeibuliwa kwenye mjadala wa pamoja. Hivyo, nikaamua kuwa jeshi la mtu mmoja.
Hali hii haikuwa ya kwanza kuwahi kutokea, nilikwishakutana na visa vya namna hii mara kadhaa, sema hii ilitia fora. Awali nilikuwa nakutana na watu wachache au wengi, wakakosekana baadhi. Lakini hii ilikuwa mara ya kwanza wote kukosekana. Sikujali. Kwanza kabisa, mimi najijua, napenda sana kufanya uwasilishaji, hivyo hata kama ingekuwaje, tuseme kwa mfano angelichaguliwa muwasilishaji mwingine, bado ningelijiandaa kama vile mimi ndio muwasilishaji mkuu. Ndiyo. Kila mtu na ulevi wake bwana, na mimi wangu ulikuwa huu wa kupigiwa makofi na kupewa sifa kwa uwasilishaji bora na wahadhiri au ma-tutor. So kusema kweli, nilijiandaa vema kwa nondo za uhakika.
Siku ya uwasilishaji, mimi nilienda kwenye semina kama kawaida kwa muda uliopangwa. Kumbe bwana, wale jamaa zangu, kwa kutaka angalau wapate point mbili za kujitetea nazo ikitokea wametakiwa kutoa hoja, waliwahi nusu saa kabla ili wakutane na wahusika wengine, wadandie points. Hali ikawa ngumu pale wote tisa walipojikuta hakuna hata mmoja aliyehudhuria kwenye majadiliano. Kimbembe kikawakumba. Wakaanza kuhaminika. Wajadiliane, waandike, wawasilishe, na bado kazi hiyo ilihitaji kukusanywa ikiwa imechapwa!. Niliwakuta jamaa wameloa jasho wakihangaika.
Ilikuwa dakika tano hivi kabla ya muda wa wasilisho kufanyika. Dah walikuwa wamejikatia tamaa vibaya sana. Mwanaume nikaingia kwa mbwembwe na kabrasha zangu kwenye begi utadhani waziri wa fedha anaenda kusoma bajeti bungeni.
'Oya waungwana, muda wa kuingia kwenye semina huu. Vipi bado mnagaagaa na upwa?' Nikawauliza.
'Hivi si tupo wote wewe?' Aliniuliza jamaa mmoja anaitwa Stanley.
'Yeah man, twendeni tukawasilishe wazee!' niliwaambia.
'Vipi mwanangu uliandaa wasilisho?' akaniuliza tena.
'Haya ndio mambo niliyofuata hapa mlimani. Hebu njoeni hapa wadau, tuwekane sawa kabisa.' nilitamka kwa sauti kubwa yenye mamlaka. Najua kwa wakati huo walikuwa tayari kunisikiliza kwa hamu zote, si nimekuja kuokoa chombo kisiende mrama? Basi wakanisogelea wakiwa watulivu kama vifaranga walionyeshewa. Nikawaangalia nyuso zao zilivyotia huruma, basi nikacheka sana kimoyomoyo.
'Waungwana, tumefeli sana kwenye kipengele cha uungwana, fikiria wote mlikimbia majadiliano na kuniachia mzigo wote nibebe mimi?' nilivyotamka hivyo nikaona nyuso zao zikipata nuru ya tumaini jipya. Kwa sababu walau walipata uhakika kwamba kutakuwa na kazi ya kakabidhiwa kwa profesa.
'Sasa. Hapa nimeshaandaa nondo, nina uhakika wa asilimia mia wa kuwapatieni A ya bure. Lakini mnatakiwa mfahamu kuwa, nimetumia muda na gharama. Hapa tunafanya changisho, ndio unapata fursa ya kusaini jina lako kwenye wasilisho. Kila mmoja anachanga buku mbili. Tufanye fasta, naona bado dakika tatu tuingie kwenye semina.' niliongea kwa kujiamini sana nikiwa nimevalia sura ya kazi. Hakuna aliyebisha. Nikazikusanya buku mbili mbili, tukazama darasani.
Kama kawaida yangu, kumbuka nimekueleza huu ndio ulevi wangu. Muda wa wasilisho ulipofika, nilikabidhi nakala ya wasilisho kwa msimamizi wa semina yetu. Profesa Nkungu, halafu nikaanza mbwembwe zangu za uwasilishaji hoja. Huu ndio uwanja naofanyaga mambo yangu, basi nikawa nipo namwaga sera zangu huku nikishuhudia zinavyowaingia wadau. Nikamuona profesa anatikisa kichwa juu chini kukubaliana na hoja zangu. Nilipoweka kituo baada ya wasilisho, chumba kizima walikuwa wanapiga makofi. Kwangu ilikuwa burudani kabisa. Wale jamaa zangu hawakuamini. Niliwapatia alama A Kama nilivyowaahidi. Profesa akasifia sana kundi letu.
Basi, tulivyotoka kwenye semina, nikiwa naondoka mdogo mdogo kuelekea kwenye vimbweta nikaperuzi peruzi notes zangu. Nikasikia sauti nyuma yangu. 'Derrick'. Ilikuwa sauti laini, sauti ya kike. Ikanilazimu kusimama na halafu nikageuka nyuma, maana chuoni kuna watu wengi na wakina Derrick sikuwa mimi pekee.
'Naomba nisubiri tafadhali' yule msichana alitamka. Nikakumbuka Ni miongoni mwa wale wanakikundi niliowatoza shilingi elfu mbili mbili.
'Mimi?' niliuliza kwa kutojiamini.
'Ndio, wewe si Derrick?' akatamka kwa ulizo.
'Ndio, lakini kwenye chuo kinachosajili maelfu ya wanafunzi huwezi kudhani utakuwa mtu pekee mwenye jina kama lako, sivyo? Nilimweleza.
'Sawa, upo sahihi nadhani.' alitamka yule mrembo.
'Haina kudhani hiyo, ndio uhalisia wa mambo' nikamuhakikishia.
'Kuna hoja unashindwa kujibu kweli?' mrembo huyu aliniuliza.
'Ah hayo masihara sasa. Of course kila hoja inaweza kujibiwa. Kwa kukubaliwa au kupingwa' nilimwambia halafu nikaongezea.
'Pale palikuwa na Helen, Mwajuma, Aisha na Doris, wewe utakuwa nani kati yao?' niliuliza nikiwa nimetaja majina ya wasichana ambao walikuwa sehemu ya kundi langu la wasilisho.
'Tabiri!' alinambia akiwa anatabasamu.
'Haha, mie si Sheikh Yahya bwana. Lakini kwa vile umenipa cheo hicho, wacha nijaribu, kwani nikikosea kuna hukumu?' akatikisa kichwa kulia na kushoto kumaanisha hakuna hukumu. Nami nikaamua kwenda na jina la kwanza.
'Hellen' nikatamka bila kupepesa jicho.
'Nilijua unafahamu, sema Unataka kuniigizia tu!'
'Haha' nikajichekea zangu. Sikufahamu jina lake, lakini sikuona kwa nini nisitumie lift hii niliyokua napewa bure, ya kufahamu nisichofahamu.
'Enhe nambie Hellen, wewe na wenzio mna tabia mbaya sana. Mbona mkaniachia kazi peke yangu' sikuwa na hoja na kulikuwa kumepita ukimya wa sekunde kadhaa kati yetu, hivyo nikaona niongee kauli hiyo kufufua mjadala. Huwa sipendi nikiwa na mtu kuwe na ukimya kati yetu, hasa kama ni jinsia ya kike. Kuepuka kutongoza, basi mimi huanza kuleta simulizi za kutunga za uongo na kweli ili kuepuka ukimya. Mara nyingi, nautafsiri ukimya kama mlango wa kuruhusu mwenzako aingie moyoni mwako na kuibua hisia za mapenzi.
Sio kwamba sipendi kutongoza. La hasha! Ni kwamba, ili kudumisha nidhamu binafsi, sipendi niwe kwenye mahusiano na msichana tunayeonana kila mara. Yaani darasani, kwenye semina, canteen na maeneo ya chuoni. Ndiyo maana niliamua kuwa na mahusiano na msichana ambaye anasoma chuo kishiriki cha chuo kikuu Cha Dar es salaam, kampasi ya Duce - Chang'ombe. Anaitwa Welu.
Hii Ina maana kwamba, tulikuwa tunaonana wikend tu na mara moja moja kati kati ya wiki. Kwangu mimi, hiyo ni heshima. Kuna kumisiana na kutarajiana kunakoamsha penzi na kulifanya liwe kileleni muda wote. Pia inaepusha migongano na migogoro midogo midogo inayoyumbisha penzi kama vile wivu pale unapomuona mwenzio anazungumza na mtu wa jinsia yako, halafu ukajikuta unaanzisha zogo. Inakuwa utoto, maana mara kadhaa nimeshuhudia washkaji wanatandikwa mbele ya mademu zao kwa sababu hizo za wivu. Kukaa unaumia moyoni kwa sababu unajikuta umejipachika ukachero wa kumfuatilia mwenzio nyendo zake, kama vile yeye ni mtoto asiyejua anachofanya.
Mara unaanzisha zogo na shemeji pasipokujua, au mrembo wako anazungumza masuala tofauti, unahisi Ni mapenzi unajitosa umuoneshe umwamba huyo jamaa, halafu unatoka hapo umevimbwa midomo au umepasuliwa komwe. Hayo ndio mambo naepuka kwa kuwakwepa warembo wa kuonana kila mara. Shida kubwa ni kwamba, hujijui kama una wivu,na hata unapofuatilia mambo yake, unakuwa pia hujui kwamba ndio umeanza upelelezi. Unajikuta mtumwa wa mpenzio bila kujua. Ah, hayo mie siyataki kabisa.
'Dah, ungejua ungenipa pole mwenzio!' Hellen aliongea kwa unyonge. Ah, kama nilivyokueleza awali, nina wepesi sana wa kubebwa kihisia. Ndio maana, kusema kweli, sipendi kusikiliza simulizi za huzuni, najikuta tu navutwa makini, na hali hiyo huniondolea mudi ya furaha. Mimi napenda habari za furaha, hizo tu, basi. Sasa, ajabu ni kuwa mtu akinijia na simulizi ya huzuni najikuta namsikiliza huku nikibebwa kihisia utadhani suala husika linanihusu.
'Oh Pole sana Hellen.' nilitamka huku nikiingiza mkono kwenye mfuko wa suruali yangu na kuchomoa wallet.
'Naamini sijakutendea haki kuchukua buku mbili zako, bila kujali ulikuwa na madhila gani. Tafadhali nisamehe.' niliongea huku nachomoa elfu mbili kwenye wallet na kumkabidhi Hellen.
'What?? Noo Derrick, Noo! Actually nimekufuata kutaka kukushukuru kwa jinsi ulivyookoa jahazi. Mimi napenda sana kushiriki kwenye discussion. Siku ile nilipata dharura, kulikuwa na kikao cha harusi na mimi nilikuwa nahusika kwa sehemu kubwa, so nikakosa namna ya kuomba udhuru, hivyo nikalazimika kukosa.'
'Ah, that's better now. Unajua hakuna kitu kinachoumiza kama kuwa-taken advantage of (kuchukuliwa poa) kwa sababu ya matatizo yako. Kwa hiyo, ulivyoanza kwa kusema nikupe pole, nikajua itakuwa tu ulikumbwa na matatizo. Haha, kwa hiyo anaolewa dada au unapata wifi?' nikauliza kwa utani. Nikaona kama Hellen alishituliwa na swali langu, au kuna namna swali hilo lilimuondolea Hali ya kujisikia amani (comfortability).
'Haha, forget about that. Derrick, I love your way of doing things. ( Sahau kuhusu hilo, napenda sana unavyokunyanyasa mambo yako) Jinsi ulivyoshushasha nondo mle ndani najisikia kukutoa out, lakini shida ni moja tu. Natakiwa tena kwenye kikao cha wajasiriamali mjini. So, please accept this as my gesture of appreciation (tafadhali pokea hii kama shukrani na hongera yangu) .' Hellen aliongea huku akinikabidhi noti ya shilling elfu kumi. Wow! Nikabaki nashangaa. Nikawa sina neno la kusema. Hata kusema asante nikasahau.
'Do you mind if I had your phone number?' (naweza kupata namba yako?) Hellen aliniuliza akiniangalia kwa jicho fulani hivi! Sauti hiyo ikanitoa kwenye pumbazo la muda nilikokuwa nimetopea.
'Hellen' nikatamka nikiwa nimekumbatia viganja vyake kwenye viganja vyangu.
'Asante sana, lakini neno tu la shukrani linatosha. Huna haja ya kulipia. You are a nice person. Please keep the money, ok. I appreciate your appreciation.' (Wewe ni mtu poa sana. Hata hivyo, siwezi kupokea fedha yako. Jua tu, nimekubali kunibali kwako) niliongea kwa sauti tulivu. Sauti ya kunong'ona. Huenda kuna namna sauti hii iliamsha kitu ndani yake.
'My numbers are ….. ' nikaanza kumtajia namba zangu, lakini nikasikia sauti yake ikisema
'Wait a minute' (subiri kwanza) nikalazimika kutulia wakati akichomoa simu yake kwenye mkoba. Ilikuwa tablet moja amazing. Well, mimi nilikuwa na kismart changu cha tekno, fresh tu!
'Ok, nitajie' alitamka tena Hellen.
'07174117..' nikamtajia na yeye akaziandika kwenye simu yake. Sekunde kadhaa mbele nikasikia kimeo changu kinaita.
'That's my number' akatamka. Halafu akaniambia
'Sasa, mie niwahi bwana!' Ni kama sikusikia, lakini nilimsikia, sema tu kuna namna huyu dada Hellen alikuwa ananipumbaza kwa sauti yake tamu. Nikiwa nimeganda sijui cha kusema, nikashitukia Hellen amenibusu shavuni halafu yule ananipungia mkono akiwa anaondoka. Nikabaki nimeduwaa. Napopata akili ya nini hasa kimetokea, Hellen alikuwa keshapotea kwenye upeo wa macho yangu. Kama vile bwege, nikabaki napunga hewani mikono yangu.
David Ngocho Samson
2020