RICHEST
Member
- Jun 23, 2011
- 25
- 16
Kuna watu wengi wanaamini nchi ili iende unahitaji utoze kodi.Si kweli.Korea ya Kaskazini inaenendeshwa bila kodi kwa miaka mingi sasa .Na ni marufuku kulipa kodi ya mapato korea.Wanachofanya wao wanaamini serikali haziwezi kuendesha nchi kwa kujiamini kama haina vitega uchumi vyake vya maana ambako itapata mapato yake ya uhakika.Sababu ukitegemea private sector wana matatizo waweza kupeleka puta.Au wakafunga biashara kukukomoa ukubaliane nao.Ndio maana Korea Kaskazini hadi leo ina kiburi cha ajabu haiigopi hata marekani inao uwezo wake kama serikali wa kujiamini.
Hivyo serikali ya korea kaskazini hutegemea mapato toka mashirika yao ya umma yaliyozagaa kila kona na ya kila sekta.Na ukiharibu uendeshaji wa shirika ukiwa meneja au mtumishi wanakunyonga.Nasikia na Nyerere alipoanzisha mashirika ya Umma alishauriwa hivyo na Abdulahman Babu akiwa waziri wake wa mipango ili aelekee huko pa kuifikisha serikali ijitegemme isitegemee kodi.Na Nyerere alitangaza Siasa ya kujitegemea ambayo ilikuwa ni kwa ajili ya kujitegemea mtu binafsi lakini pia kwa ajili ya serikali isiwe tegemezi .Lakini viongozi wengi wanasikiliza propaganda za kilevi za nchi za magharibi kuwa nchi haiwezi endeshwa bila kodi na serikali isiwe na vitega uchumi ili makampuni yao yaje yapeleke serikali puta.Hivi kama huna kitega uchumi uwe mtu binafsi au serikali hutakujwa usumbuliwe mbeleni kimaisha au kiserikali?
Katika jambo ambalo kwa moyo wangu wote naamini Marehemu Mwalimu Nyerere hajatendewa haki na serikali zilizomfuata ni kuua mashirika ya umma.Alianzisha misingi ya kusaidia serikali ifikie mahali ije ijitegemee isitegemee mapato ya kukimbiza machinga na virungu barabarani eti hawalipi kodi. Hivi siku walipa kodi wakubwa wakiamua kufunga biashara zao na kuondoka zao kama ilivyotokea Zimbabwe
Nafikiri suala la serikali ya Tanzania kuwa na mashirika ya umma lifikiriwe upya kwa usalama wa serikali yenyewe.
Na mimi nangoja kwa hamu Siku TRA watakapoambiwa hawana kazi maana yake hawa jamaa kiboko kabla hata biashara hujafungua mlango wa duka na hata kabla hujauza hata kibaba kimoja cha unga wameshakukadiria kodi unayotakiwa kulipa serikali.Siku wakiondoka nitacheza CHAN CHAN ngoma ya kihindi na kupiga fataki hewani kusherekea.
Hivyo serikali ya korea kaskazini hutegemea mapato toka mashirika yao ya umma yaliyozagaa kila kona na ya kila sekta.Na ukiharibu uendeshaji wa shirika ukiwa meneja au mtumishi wanakunyonga.Nasikia na Nyerere alipoanzisha mashirika ya Umma alishauriwa hivyo na Abdulahman Babu akiwa waziri wake wa mipango ili aelekee huko pa kuifikisha serikali ijitegemme isitegemee kodi.Na Nyerere alitangaza Siasa ya kujitegemea ambayo ilikuwa ni kwa ajili ya kujitegemea mtu binafsi lakini pia kwa ajili ya serikali isiwe tegemezi .Lakini viongozi wengi wanasikiliza propaganda za kilevi za nchi za magharibi kuwa nchi haiwezi endeshwa bila kodi na serikali isiwe na vitega uchumi ili makampuni yao yaje yapeleke serikali puta.Hivi kama huna kitega uchumi uwe mtu binafsi au serikali hutakujwa usumbuliwe mbeleni kimaisha au kiserikali?
Katika jambo ambalo kwa moyo wangu wote naamini Marehemu Mwalimu Nyerere hajatendewa haki na serikali zilizomfuata ni kuua mashirika ya umma.Alianzisha misingi ya kusaidia serikali ifikie mahali ije ijitegemee isitegemee mapato ya kukimbiza machinga na virungu barabarani eti hawalipi kodi. Hivi siku walipa kodi wakubwa wakiamua kufunga biashara zao na kuondoka zao kama ilivyotokea Zimbabwe
Nafikiri suala la serikali ya Tanzania kuwa na mashirika ya umma lifikiriwe upya kwa usalama wa serikali yenyewe.
Na mimi nangoja kwa hamu Siku TRA watakapoambiwa hawana kazi maana yake hawa jamaa kiboko kabla hata biashara hujafungua mlango wa duka na hata kabla hujauza hata kibaba kimoja cha unga wameshakukadiria kodi unayotakiwa kulipa serikali.Siku wakiondoka nitacheza CHAN CHAN ngoma ya kihindi na kupiga fataki hewani kusherekea.