Njia wanayoweza kutumia wadada kupata waume wa kuwaoa kwa haraka

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,173
39,931
Ulimwengu umebadilika sana, yale mambo ya kizamani ya kwamba, mwanaume ndio anatakiwa aanze kumtongoza mwanadada/mwanamke yalishapitwa na wakati. Kwa takwimu zilizopo duniani, wanawake ni wengi kuliko wanaume; sasa usipotumia ujuzi wa kuzaliwa, utajikuta unazeeka mwenyewe bila mwenza. Ndio maana nyakati hizi, tunaona wengine wanatembea na mabango barabarani.

Njia rahisi kwa mwanadada kufanikisha lengo la kupata mwenza, inabidi aibu aweke pembeni; kama kuna mtu umemkubali, iwe kazini, chuoni, sokoni, kanisani n.k jitahidi uonane naye 'physically' na muwe wawili tu, na umfungukie jinsi unavyojihisi kuwa naye na unatamani awe mumeo.

Kwa asilimia kubwa si wanaume huwa ni dhaifu kwa mwanamke, hapo lazima jibu liwe Yes. Kama itakuwa ni ngumu kuonana naye, tafuta namba yake ya simu, na umpigie kwa muda unaoona kwake hatokuwa na majukumu mengi na ujaribu kumfungukia; hapo matatizo ya kutembea na bango barabarani yatapungua.

images
 
Back
Top Bottom