Jinsi ya kuondoa au kupunguza mafuta tumboni kwa wanawake (Vitambi vya kike)

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Jamani kuna ndugu yangu anateseka sana na kitambi amejaribu kunywa whisky za aina yote akiamini atapunguza kitambi jawabu -ve...kwenu wapendwa...afya bora kwa kila mtanzania...
Apunguze kula vyakula vya wanga kwa wingi...

Asubuhi - breakfast nyepesi (matunda + mboga na wanga kidogo kama mkate wa brown)

Lunch - Wanga kidogo + Maharage + Mboga za Majani kwa wingi

Dinner - Mboga za Majani + Matunda (Dinner iliwe walau Masaa 2 kabla ya kuingia kulala).

Anywe walau Lita 1 ya maji kwa siku.

Apate walau Masaa nane ya usingizi.

Afanye mazoezi ya viungo ikiwamo situps walau mara 3 kwa wiki.

ASINYWE POMBE.

Mifano ya Chakula ni "mifano tu" awe mbunifu kulingana na taste yake...ili mradi aepuke milo mizito kama Ugali, Wali, Mihogo, Vitumbua mara 3 kwa siku.
Pole kwa Kitambi...

Ushauri wangu

1. Afunge...alau kwa wiki mara 2
2. kama anauwezo afunge swaumu kwa mwezi mara 15, afunge na kula kesho yake...na Ulaji wa vyakula Kitaalamu.

3.Awe na muda kufikiria matatizo yanayowakabili watanzania wengi ambao hawana elimu, tiba hafifu,mlo haba na mengineyo, namna kuondoa utawala mbovu vitamfanya apungue kitambi kwa kushughulishwa matatizo hayo.

4. Pombe zote aache.(naomba kutofautiana nao na wadau hapo Juu)
5. Apate Belt za kufunga Tumboni kupunguza ufumukaj wa tumbo.
6. Mazoezi hapaswi kuyaacha. Kila zoezi litakalopelekea kupunguza mwili asiache.

Kikubwa Uvivu(Kujiachia) na kulala Hovyo, Ulevi ndizo sababu kadhaa za Kufumuka matumbo.
Kuna jamaa alikuwa na tatizo kama hilo, ilikuwa kazi kukata kucha za miguu mpaka mtu amkate. Alivyoenda kwa wataalamu, akaambiwa kwa wiki mbili ale mboga mboga na matunda tu, akitaka sharubati basi iwe ya chungwa ama zabibu na vizuri iwe fresh. Baada ya wiki mbili alikuwa kaambiwa ale wanga mchana tu kwa wiki tatu na aliambiwa apunguze kama atashindwa kuacha kwa wiki hizo tatu nyama, ale samaki na kuku tena kwa uchache mno. Ila vizuri aliambiwa ale maharagwe ya soya na mihogo kiasi mchana, kwa wingi matunda na mboga mboga. Baada ya miezi miwili usingeweza kujua ni yule.

Mwingine alikuwa mhindi, huyu yeye alikuwa mnene ile ya kutisha. Ushauri wote aliopewa haukupunguza unene wake kabisa. Alihangaika sana kwa hilo manake alikuwa anapata shida na huo unene. Siku moja akaenda kwa daktari akamueleza yote jinsi alivyohangaika kupunguza unene imeshindikana. Daktari akamchukua vipimo, halafu akamwambia kuwa kwa unene ule ana tatizo kubwa sana linaloweza kumsababishia moyo usimame ghafla kufanya kazi, sababu hata moyo wake una tatizo kaligundua. Akampa dawa akamwambia kuwa baada ya mwezi arudi bila kukosa huenda kama dawa hazitofanya kazi watamfanyia uperesheni na itahitajika haraka kuokoa maisha. Jamaa akatokwa jasho vibaya mno, akaenda kutumia dawa, baada ya mwezi aliporudi hospitali alikuwa kwisha kabisa kwa kuogopa kifo. Daktari akamwambia nilikutisha ili upone, na dawa nilizokupa ni Aspirin, hivyo sasa fuata ushauri wa chakula usinenepe tena. Kilichotokea kumbe jamaa alikonda kwa kuogopa kifo, baada ya mwaka unene ukarudi kama kawaida.

Chukua ushauri wa kwanza.
Wana JF,

Hili suala la mtu kutafuta ushauri wa jinsi ya kuondoa kitambi liliishaongelewa hapa kama sikosei miezi mitatu minne iliyopita. Kuna ushauri ulitolewa na jamaa yangu mmoja akaamua kuufuata kwa makini. Huwezi kuamini ndani ya siku 45 alibadilika kupita kiasi. Inawezekana nisiandike vile vile kama yule mshauri wa awali lakini huyu jamaa yangu alizingatia yafuatayo;

1. Awali alikuwa hali breakfast. Baada ya ushauri alianza kula breakfast.

2. Alikuwa anakula chakula kingi mchana na usiku. Alibadili na kuanza kula chakula kidogo mchana na usiku anakula chakula kidogo kabisa au siku nyingine hali.

3. Aliongeza kasi ya kunywa maji na kwa siku angalau alikuwa anakunywa lita 3 za maji

4. Alianza kwenye kwenye gym kila jioni ambako alipata nafasi ya ku-burn idle calories halafu kama nilivyosema hapo namba 3 akawa hali chakula kingi usiku.Kwenye gym machine alikuwa ana cover si chini ya kilomita 5 kila siku na alikuwa anakwenda kwenye gym 4 times a week.(He should spend at least 30 minutes in gym room exercising hard)

5. Alikuwa anaepuka kula vyakula vyenye jamii ya nyama usiku.

6. Alipunguza kasi ya kunywa bia.

This is a practical experience na nina imani huyo aliyeuliza akifuata haya maelekezo anaweza kufanikiwa kama jamaa yangu alivyofanikiwa.

Tiba
CHANZO CHA VITAMBI, UZITO NA UNENE KUPITA KIASI NA NAMNA UWEZAVYO KUDHIBITI TATIZO HILI BILA DAWA:


Mfumo mkuu wa fahamu katika ubongo hutambua kushuka kwa kiasi cha nguvu kinachopatikana kwa ajili ya matumizi yake.

Hisia za kiu au njaa pia hutokea kunapotokea kupungua kwa nguvu mwilini.

Ili kuiamsha nguvu toka katika mafuta yaliyohifadhiwa, kunahitajika mwingilio maalumu wa ki-homoni. Zoezi hili huchukuwa muda mrefu zaidi (na pengine mazoezi zaidi kwa mishipa huhitajika) kuliko udharura wa uhitaji wa nguvu unavyohitajika na ubongo.

Sehemu ya mbele ya ubongo hupata nguvu ama kutoka katika nguvu inayozarishwa kwa nguvu za maji au kutoka katika sukari kwenye mzunguko wa damu. Nguvu zitokanazo na maji huhitajiwa kwa dharura zaidi siyo katika kuzarisha nguvu tu, bali hata katika mifumo yake ya usafirishaji ambayo hutegemea maji zaidi.

Kwa hiyo hisia za kiu na njaa huja kwa pamoja kuonesha mahitaji ya ubongo. Hatuzitambui hisia za kiu, na tunazichukulia hisia zote kuwa ni hitaji la kula. Tunakula chakula hata wakati mwili unapotakiwa upokee maji. Watu waliopunguza uzito wao kwa kunywa maji kabla ya kula, wamefanikiwa kuzitofautisha hisia hizi mbili. Hawakula kuzidi ya kipimo kuituliza kiu ya mwili kwa maji.

Hata hivyo, watu wengi sana kote duniani huwa hawafuatilii lolote kuhusu uzito wao. Uzito uliozidi ni ugonjwa na ni hatua ya kwanza katika kuporomoka kwa mwili wa binadamu. Kila mmoja anapaswa kujua kama uzito alionao unafaa kwa mwili wake au la.


Kwanini watu wanakula sana?

Ubongo wa binadamu una ukubwa kama 1/50 ya uzito wa mwili. Inasemwa, ubongo una seli neva kama tilioni 9 (kama chipu za kompyuta). Inasemwa, zaidi ya asilimia 85 ya seli za ubongo, ni maji.

Asilimia 20 ya damu yote mwilini imeelekezwa na inapatikana kwa ajili ya ubongo. Hii inamaanisha ubongo unahitajika kuchukua kila unachokihitaji kwa ajili ya kazi zake toka katika mzunguko wa damu.

Ubongo ni moja kati ya ogani pekee za mwili ambazo hufanya kazi muda wote hata katika usingizi mzito, huzishughurikia taarifa zote toka katika maeneo mbalimbali ya mwili na zile zinazouingia toka katika mazingira, jamii na hata zile toka mazingira ya ki-usumaku.

Katika kushughurikia kazi zote hizo, ubongo hutumia kiasi kikubwa sana cha nguvu. Wakati huo huo ubongo hutumia nguvu katika kutengeneza mahitaji ya mwanzo na jumbe kemikali (chemical messengers) ambazo zimetengenezwa toka seli za ubongo na ambazo zinatakiwa kusafirishwa kwenda miishio ya neva kuzunguka mwili.

Mfumo wa usafirishaji mwilini hutumia pia kiasi kikubwa cha nguvu. Kiasi hiki kikubwa cha matumizi makubwa ya nguvu yanayofanywa na ubongo ndiyo sababu ya ubongo kutengewa asilimia 20 ya mzunguko wa damu.

Seli za ubongo huhifadhi nguvu zake katika mifumo miwili. Stoo yake ya kwanza inaitwa Adenosine Triphosphate (ATP), na ya pili inaitwa Guanosine Triphosphate (GTP).

Baadhi ya maswali maalumu hujibiwa na nguvu zilizohifadhiwa toka stoo ya kwanza (ATP) ambayo inapatikana katika maeneo mbalimbali ya seli hasa katika kuta zake. Kwenye ukuta wa seli (cell membranes) ndiko ambako taarifa huingilia na ndiko ambako majibu huanzishwa.

Kuna mfumo wa mgawo wa 'nguvu' ambao hufanya kazi muda wote katika seli. Siyo madokezo yote ya maswali yanaweza kufanikiwa kupata majibu toka katika stoo ya nguvu ya kwanza (ATP).

Kuna vikwazo katika uelekezwaji wa nguvu kwa baadhi ya maswali. Ubongo unakokotoa na kukielewa kipi ni cha mhimu na kipi si cha mhimu katika bajeti yake ya nguvu.

Wakati inapopungukiwa nguvu stoo ya kwanza, baadhi ya madokezo hayapati majibu. Kupunguwa huku kwa nguvu toka stoo ya kwanza kwa baadhi ya seli za ubongo, kunatokea kujionesha kama hali ya uchovu katika baadhi ya kazi zinazosimamiwa na seli hizo.

Vivyo hivyo, matendo hayo hutokea pia kwa stoo ya pili ya nguvu (GTP). Katika baadhi ya matendo maalumu ya dharura, baadhi ya nguvu toka stoo ya pili inaweza kuelekezwa kuiongezea nguvu stoo ya kwanza kwa madokezo maalumu kushughurikiwa.

Hifadhi ya nguvu katika maghala ya nguvu za ubongo, inaonekana kutegemea zaidi upatikanaji wa sukari mwilini. Muda wote ubongo unachukuwa sukari toka katika damu ili kuyajaza maghala yake (ATP na GTP).

Hivi karibuni imegundurika kuwa, mwili unao uwezo wa kutengeneza nguvu kwa kutumia maji (hydroelectric energy), wakati maji peke yake yanapoingia kupitia kuta za seli na kuwasha pampu maalumu za majenereta ya kuzarishia nguvu yaitwayo kwa kitaalamu, 'cation pumps', ni kama vile bwawa la umeme linapojengwa karibu na mto mkubwa.

Kwa hiyo ubongo hutumia mifumo miwili kwa ajili ya mahitaji yake ya nguvu, wa kwanza ni ule wa kiumetaboli wa chakula na kuunda sukari,na wa pili unahusisha matumizi ya maji kuzariha nguvu umeme zitokanazo na maji (hydroelectric energy).

Inajionesha wazi sasa kwamba ubongo unategemea zaidi nguvu zitokanazo na umeme wa maji hasa katika mifumo yake ya usafirishaji kwenye neva zake kwenda sehemu mbalimbali za mwili.

Ili kuhimili mahitaji ya ubongo, mwili umekuza mfumo maalumu ili kutunza kiasi cha kawaida cha sukari katika mzunguko wa damu. Hufanya hivyo kwa njia mbili, ya kwanza ni ile ya kusisimua ulaji wa vyakula vyenye protini na wanga ambavyo vitabadilishwa kuwa sukari ikijumuisha pia sukari yenyewe katika mlo, njia ya pili ni ya kubadili wanga na protini toka katika hifadhi ya mwili na kuwa sukari. Njia hii ya pili huitwa kitaalamu kama 'Gluconeogenesis', yaani utengenezwaji wa sukari toka katika malighafi zilizohifadhiwa. Utengenezaji wa aina hii wa sukari hufanyika katika Ini.

Utegemezi wa sukari kwa kazi nyingi zifanywazo na ubongo, kumepelekea mapenzi kwa vyakula vyenye radha ya utamu. Mwili umekuza mfumo kanuni maalumu, uunganikaji wa kazi na ogani zingine hasa Ini wakati radha ya utamu inaposikika katika ulimi.

Inapotokea hakuna sukari ya kutosha katika mzunguko, Ini huanza kuitengeneza na kuijaza kwenye usawa wa damu. Mwanzoni litaanza na wanga uliokuwa umehifadhiwa ukifuatiwa na protini na kiasi kidogo cha mafuta. Ubadilikaji wa mafuta kuwa sukari huchukuwa muda mrefu zaidi.

Mwili unahitaji kubaki bila chakula kwa muda fulani kabla kiasi kikubwa cha umetaboli wa mafuta hakijaanzishwa.

Protini hupatikana kiurahisi zaidi na umetaboli wake ni mrahisi zaidi kuliko mafuta. Dipositi za mafuta zimetengenezwa kutokana na yuniti nyingi mbalimbali za asidi mafuta ambazo zimeungana pamoja. Asidi mafuta za mtu ndizo huvunjwa (humeng'enywa) kwa ajili ya thamani yake kwa nguvu ya mwili.

Kila gramu 1 ya mafuta hutoa kalori 9 za nishati, kila gramu 1 ya protini au sukari hutoa kalori 4 za nishati. Hii ndiyo sababu mafuta yanapotumika kuzarisha nguvu, mtu hajisikii sana njaa.

Kwa watoto, stoo za mafuta zina rangi ya kahawia na zina mzunguko zaidi wa damu. Kwenye mafuta ya rangi ya kahawia, mafuta yanameng'enywa moja kwa moja na nguvu hutengenezwa. Baada ya miaka kadhaa baadaye, stoo za mafuta huwa na mizunguko michache ya damu na uwezekano mdogo wa kuvifikia vimeng'enya vinavyozihamasisha asidi mafuta kwa mabadiliko yake kwenye ini na mishipa.

Wakati mwili unapokuwa legelege, mishipa hushambuliwa kirahisi zaidi na protini yake humeng'enywa na kufanywa sukari. Ingawa, ikiwa mishipa inashuhulishwa, itaanza kumeng'enya baadhi ya mafuta yake yaliyohifadhiwa na kuyatumia kama chaguo la chanzo chake cha nguvu katika kufanya kazi na kuutunza au kuuongeza ujazo wake.

Ili kufanya hivyo, mishipa hukiamsha kimeng'enya chake cha mafuta, homoni iitwayo kwa kitaalamu 'lipase'.

Imedhihirika katika majaribio ya kujirudia huko nchini Sweden kwamba kimeng'enya hiki cha kuchoma mafuta huamka baada ya mwendo wa miguu wa saa moja MFULULIZO, na huendelea kumeng'enya mafuta kwa muda wa masaa 12.

Kwa hiyo ikiwa mtu atatembea kwa muda wa saa moja mara mbili kwa siku, atakuwa amekiamsha kimeng'enya (enzyme) hiki kufanya kazi kwa masaa 24 (siku nzima)!.

Kuendelea kutembea zaidi, ndivyo kimeng'enya hiki kinavyoendelea kujitokeza zaidi, kwa hiyo fungu lolote la mpango wa mlo lazima liegemee zaidi upande wa mahitaji ya mishipa kwa ajili ya matokeo ya muda mrefu ya moja kwa moja ya kifiziolojia katika kumeng'enywa kwa mafuta.

Ni kimeng'enya hiki hiki (lipase) kwenye mzunguko wa damu ambacho huisafisha mishipa dhidi ya mabaki ya mafuta, cholesteroli na dipositi zake.


Hivi ndivyo ilivyo rahisi kupunguza uzito na unene bila nguvu wala gharama yeyote!. Anza leo, tembea saa moja kutoka kituo A mpaka kituo B bila kupumzika KWA SAA MOJA, ITABIDI UWE NA SAA KABISA MKONONI asubuhi na jioni, baada ya wiki mbili pima tena uzito wako kuona namna ulivyofanikiwa kwa muda huo na muda gani uwekeze tena kumaliza tatizo hili linalosumbuwa watu wengi kote duniani.

Kumbuka pia kunywa maji kila nusu saa kabla ya kula.

Kazi zinazofanywa kwa kukaa (maofisini) katika maisha yetu ya kisasa, ni kipindi cha mabadiliko ya kiutamaduni. Fiziolojia ya miili yetu bado haijabadilishwa vya kutosha kuwezesha matumizi yasiyo ya kawaida ya mwili wa binadamu. Mwili bado unahitaji kushughulishwa kwa mishipa ili kuhimili hali ya kawaida ya kazi zake.

Ikiwa mwili unaendesha kazi zake katika hali yake ya kawaida, utaelewa ni muda gani wa kula na kwa kiasi gani bila kuizidisha hifadhi ya mafuta. Kila sehemu ya mwili itatumia kiasi chake cha nguvu iliyotengewa kwa ufanisi na kazi zinazoendeshwa vizuri zaidi. Hivi ndivyo mwili ulivyosanifiwa.

Ingawa, ikiwa ubongo umetumika zaidi (wakati wa mfadhaiko kwa mfano) na mwili haujatumika kwa uwiano huo huo kuusambazia ubongo mahitaji yake ya sukari, mtu mwenye uelewa mdogo ataangukia kwenye kula zaidi mara nyingi na kwa kiasi kikubwa.

Inashangaza zaidi inapotokea tunashindwa kuzielewa ishara za mwili unapoyahitaji maji kwa ajili ya mahitaji yake ya kusambaziwa nguvu, na badala ya kunywa maji, tunakimbilia kula zaidi.

Katika mfadhaiko (stress), mwili unakuwa umepungukiwa maji (dehydrated).

Sababu ya kwanini inatokea kuongezeka uzito ni rahisi. Tunakula ili kuusambazia ubongo mahitaji yake ya nguvu kwa ajili ya kazi zake masaa 24.

Kama ilivyofafanuliwa, mwili una vyanzo vitatu vya nguvu: Sukari, Mafuta na Maji/chumvi.

Hata hivyo, wakati chakula kimeliwa, ni karibu asilimia 20 tu za chakula ndizo hutumika na ubongo, sehemu inayobaki huhifadhiwa taratibu ikiwa shughuli za mishipa (mazoezi) hazitumiki kutumia kiasi chake cha chakula iliyotengewa.

Maji yanapotumika kama chanzo cha nguvu, stoo hii ya kuhifadhia sehemu iliyobaki ya chakula, haitokei, maji yanayozidi hutolewa nje kupitia mfumo wa mkojo.

Wakati mwingine utakaposikia njaa kati ya chakula cha asubuhi, cha mchana au cha jioni, badala ya kukimbilia kula chakula, chukua maji kunywa nusu yake kisha tafuna chumvi na umalizie maji yaliyokuwa yamebaki na kisha usubiri kwa muda wa dakika 20 na uone kama utaendelea kujisikia njaa. Zaidi ya asilimia 90 ya njaa yako itakuwa imepotea, hii ilikuwa ni namna ya ubongo wako kukuambia kuwa unahitaji maji.

Ubongo hauwezi kutuma ishara tofauti za njaa na kiu, ishara zote hutumwa kwa pamoja, hatuzitambui ishara za kutaka kunywa maji na badala yake tunakimbilia kula hata wakati mwili unahitaji maji.

Kujuwa zaidi namna ya kuyanywa maji kama tiba, waweza kunitumia sms tu katika namba 0769779533.

Kumbuka pia kuwa hii ni elimu tu na siyo kumuondoa daktari wako au chaguo lako la kutumia dawa, ni programu iliyopendekezwa kwa manufaa yako.
 
Jamani kuna ndugu yangu anateseka sana na kitambi amejaribu kunywa whisky za aina yote akiamini atapunguza kitambi jawabu -ve...kwenu wapendwa...afya bora kwa kila mtanzania...

Sasa mama si ungepeleka jukwaa la afya? make katumbo kanene na siasa wapi na wapi?
 
Mwambie aachane na whisky. Apunguze kula nyama na atembee angalau kilomita 8 kila asubuhi. Na asiache pushups.
 
one step;
Mwambie aachane na whisky. Apunguze kula nyama na atembee angalau kilomita 8 kila asubuhi. Na asiache pushups

thanks
 
Sasa mama si ungepeleka jukwaa la afya? make katumbo kanene na siasa wapi na wapi?

Ni kweli mkuu rwagubiri ila wengine mpaka waende jukww la AFYA UJUE NDUGU ZAO WAKO MAUTIUTI...at least huku mtu akiona anatoa mawazo yake na msaada unaoitajika ni wa haraka si mpaka mtu aende afya...samahani kwa kukukwaza...ubarikiwe.
 
Jamani kuna ndugu yangu anateseka sana na kitambi amejaribu kunywa whisky za aina yote akiamini atapunguza kitambi jawabu -ve...kwenu wapendwa...afya bora kwa kila mtanzania...


Apunguze kula vyakula vya wanga kwa wingi...

Asubuhi - breakfast nyepesi (matunda + mboga na wanga kidogo kama mkate wa brown)

Lunch - Wanga kidogo + Maharage + Mboga za Majani kwa wingi

Dinner - Mboga za Majani + Matunda (Dinner iliwe walau Masaa 2 kabla ya kuingia kulala).

Anywe walau Lita 1 ya maji kwa siku.

Apate walau Masaa nane ya usingizi.

Afanye mazoezi ya viungo ikiwamo situps walau mara 3 kwa wiki.

ASINYWE POMBE.

Mifano ya Chakula ni "mifano tu" awe mbunifu kulingana na taste yake...ili mradi aepuke milo mizito kama Ugali, Wali, Mihogo, Vitumbua mara 3 kwa siku.
 
Apunguze kula vyakula vya wanga kwa wingi...

Asubuhi - breakfast nyepesi (matunda + mboga na wanga kidogo kama mkate wa brown)

Lunch - Wanga kidogo + Maharage + Mboga za Majani kwa wingi

Dinner - Mboga za Majani + Matunda (Dinner iliwe walau Masaa 2 kabla ya kuingia kulala).

Anywe walau Lita 1 ya maji kwa siku.

Apate walau Masaa nane ya usingizi.

Afanye mazoezi ya viungo ikiwamo situps walau mara 3 kwa wiki.

ASINYWE POMBE.

Mifano ya Chakula ni "mifano tu" awe mbunifu kulingana na taste yake...ili mradi aepuke milo mizito kama Ugali, Wali, Mihogo, Vitumbua mara 3 kwa siku.

Sahihi kabisa, msisitizo ni kwamba huu ndio uwe mfumo wake wa maisha asitarajie makubwa - ni kupungua kilo 5 kwa mwaka, taratibu ndio mwendo.
 
Pombe anaweza kunywa in moderation. Ama chupa mbili za bia kwa siku au glasi moja ya mvinyo mwekundu kwa siku.
 
Jamani kuna ndugu yangu anateseka sana na kitambi amejaribu kunywa whisky za aina yote akiamini atapunguza kitambi jawabu -ve...kwenu wapendwa...afya bora kwa kila mtanzania...

...sema tu ni bwana yako,mwambie apunguze kula na afanye mazoezi!
 
Pole kwa Kitambi...

Ushauri wangu

1. Afunge...alau kwa wiki mara 2
2. kama anauwezo afunge swaumu kwa mwezi mara 15, afunge na kula kesho yake...na Ulaji wa vyakula Kitaalamu.

3.Awe na muda kufikiria matatizo yanayowakabili watanzania wengi ambao hawana elimu, tiba hafifu,mlo haba na mengineyo, namna kuondoa utawala mbovu vitamfanya apungue kitambi kwa kushughulishwa matatizo hayo.

4. Pombe zote aache.(naomba kutofautiana nao na wadau hapo Juu)
5. Apate Belt za kufunga Tumboni kupunguza ufumukaj wa tumbo.
6. Mazoezi hapaswi kuyaacha. Kila zoezi litakalopelekea kupunguza mwili asiache.

Kikubwa Uvivu(Kujiachia) na kulala Hovyo, Ulevi ndizo sababu kadhaa za Kufumuka matumbo.
 
Kuna jamaa alikuwa na tatizo kama hilo, ilikuwa kazi kukata kucha za miguu mpaka mtu amkate. Alivyoenda kwa wataalamu, akaambiwa kwa wiki mbili ale mboga mboga na matunda tu, akitaka sharubati basi iwe ya chungwa ama zabibu na vizuri iwe fresh.

Baada ya wiki mbili alikuwa kaambiwa ale wanga mchana tu kwa wiki tatu na aliambiwa apunguze kama atashindwa kuacha kwa wiki hizo tatu nyama, ale samaki na kuku tena kwa uchache mno. Ila vizuri aliambiwa ale maharagwe ya soya na mihogo kiasi mchana, kwa wingi matunda na mboga mboga. Baada ya miezi miwili usingeweza kujua ni yule.

Mwingine alikuwa mhindi, huyu yeye alikuwa mnene ile ya kutisha. Ushauri wote aliopewa haukupunguza unene wake kabisa. Alihangaika sana kwa hilo manake alikuwa anapata shida na huo unene.

Siku moja akaenda kwa daktari akamueleza yote jinsi alivyohangaika kupunguza unene imeshindikana. Daktari akamchukua vipimo, halafu akamwambia kuwa kwa unene ule ana tatizo kubwa sana linaloweza kumsababishia moyo usimame ghafla kufanya kazi, sababu hata moyo wake una tatizo kaligundua.

Akampa dawa akamwambia kuwa baada ya mwezi arudi bila kukosa huenda kama dawa hazitofanya kazi watamfanyia uperesheni na itahitajika haraka kuokoa maisha. Jamaa akatokwa jasho vibaya mno, akaenda kutumia dawa, baada ya mwezi aliporudi hospitali alikuwa kwisha kabisa kwa kuogopa kifo.

Daktari akamwambia nilikutisha ili upone, na dawa nilizokupa ni Aspirin, hivyo sasa fuata ushauri wa chakula usinenepe tena. Kilichotokea kumbe jamaa alikonda kwa kuogopa kifo, baada ya mwaka unene ukarudi kama kawaida.

Chukua ushauri wa kwanza.
 
Mimi nafikiri huyo bwana anatakiwa afanye mazoezi kidogo halafu awe nakiasi kwenye kula .Halafu aache pombe badala yake anywe maji mengi kila siku.
 
Mwambie awe anapiga sit ups 100 jumatatu jumatano na ijumaa
__________________
Nyani ngabu umesomea usheikh yahaya nini?
 
Mpe glass mbili za aloe vera kila siku ikipita mwezi atakuwa flat kama Shamsi Vuai Nahodha, akiongezea sit ups basi atakuwa na six pack kama Pinda.
 
Bongo tambarare..

watu wanajadili namna ya kupunguza miili yao wakati wengine hata uhakika wa huo mlo wa mchana haupo?
 
Watu wengi Tz sahivi wanatatizo kubwa la kua na uzito wa ziada (overweight) na hiyo inasababishwa na mambo mengi kubwa likiwa ni kutokuwajibika kwa Wizara ya Afya (kutotoa elimu ya afya kwa watz), utamaduni wetu (kufikiri kua kula nyama, bia na vyakula vyenye mafuta mengi kila siku ni ufahari au ishara ya maisha bora,kutojali mazoezi pengine kutokua na maeneo ya wazi ya kufanyia mazoezi(maana si wote wanaoweza kumudu gym za kulipia),

Kupenda kutumia usafiri wa gari hata maeneo ya karibu ambayo unaweza kutembea kwa miguu, kutumia lift badala ya ngazi hata kama ni kushuka floor mbili tu chini. Listi ni ndefu ila kujibu swali lako mwambie ajalibu kuepuka hayo madogo madogo kwanza halafu afuate ushauri uliokwisha kutolewa hapo juu na wadau wengine.
 
Hey people, vitambi vingine ni vya urithi... Sasa wadau mngefuatilia kwanza kwa Mama Mia, je huyu jamaa (..mume wake??) ana historia gani...!!!! Mi sina utaalamu, but ni mtazmo tu.. ha..haaa...haaaaa!!!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom