Njia bora ya kumuacha mwanamke

Gluk

JF-Expert Member
Mar 23, 2017
1,856
2,953
Ikiwa ni siku nyingne tena tunakutana kwenye jukwaa letu pendwa la MMU.
Leo naomba ushauri kidogo juu ya hili swala,

Kuna bidada mmoja tulifanya nae biashara fulani, baadae tukaendelea kuwasiliana kama marafiki wa kawaida.Ila yule binti anajifanya mlokole sana tena sana, baada ya muda fulani nikamrushia ndoano bidada akajaa mazimamazima..

Ila baadae ikatokea hali ya kutokumpenda tena na sikuwahi kugegedana nae japo anaonyesha dalili zote za kuhitaji mchezo, Nikaanza visa vya hapa na pale ila naona ndo kwanza spidi ya kunipenda inazidi maana inafikia hatua kosa nafanya mm harafu yeye ananiomba msamaha mimi.

Kutoka moyoni huyu binti sina hisia nae tena na sihitaji kumgegeda sabab mm siwezi lala na mwanamke nisiyehitaji kuwa nae. Huyu binti anapiga simu kwa siku zaidi ya mara kumi japo mm simpigii wala kumtumia SMS.

Naombeni mnishauri njia bora ya kumuacha bila kumuachia maumivu yoyote maana muda mwingine namuonea huruma jinsi anavyohangaika juu yangu ili hali mimi sina malengo nae na sihitaji kumpotezea muda wala malengo yake..

Asanteni sana
 
Mwambie samaki uliemnasa kwenye ndoano cye uliemtaka na unaona bora arudi zake kwenye maji akaendelee na maisha yake.
 
Kwa nini ulimtongoza sasa kama hukuwa na hisia nae? We unajua mwanamke akipenda Kapenda kweli..

JIFUNZE KUHESHIMU HISIA ZA WANAWAKE MKUU..USICHEZE NA HISIA ZAKE..WATU KAMA NYIE NDIO MNATUFANYA WANAUME WENGINE TUONEKANE WABAYA
Mwanzo nilikuw na hisia nae ila ghafla tu imetokea hali ya kutokujiskia kuwa nae kabsa
 
Back
Top Bottom