Njelu Kasaka: Hakuna aliye salama ndani na nje ya CCM

Massivve

JF-Expert Member
Jun 4, 2015
274
368
kasaka-300x151.jpg


MWANASIASA mkongwe ambaye alipata kuwa mwenyekiti wa kundi la wabunge waliohitaji muundo wa Serikali tatu (G55) wakati wa utawala wa awamu ya pili, Njelu Kasaka, amesema hakuna mtu aliye salama ndani au nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kauli hiyo aliitoa wakati wa mkutano mkuu wa kidemokrasia uliofanyika jana jijini Arusha ambako alikuwa mgeni mwalikwa.

Pasipo kutaja jina la mtu, Kasaka alitumia kauli hiyo kwa kugusia matukio ya kisiasa yaliyojiri katika siku za hivi karibuni.

Moja ya matuko hayo ni lile lililotokea katikati ya wiki hii kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kukabiliana na changamoto ya kutishiwa bastola na mtu anayeaminika kuwa askari kanzu.

“Ingekuwa wakati CCM ilipokuwa imeshika hatamu, suala hili la RC wa Dar es Salaam tayari CCM ingekuwa imeishakaa na kumuelekeza Rais cha kufanya juu ya mkuu huyo wa mkoa,” alisema Kasaka.

Alisema siku hizi hali haiko hivyo ndiyo maana hata Katibu Mkuu wa CCM mwaka 2015 kabla ya uchaguzi mkuu, alitaka kodi kero zifutwe, lakini ndio kwanza zikaongezwa.

“Ni kwa kuwa CCM ya sasa haina nguvu hizo tena, wapinzani wakiungana na kuondoa tofauti zao wanaweza kuiondoa CCM madarakani,” alisema.

Kasaka ambaye amepata kuwa mbunge, waziri na mkuu wa mkoa, alijitoa ndani ya CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mbali na Kasaka, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema wamiliki wa vyombo vya habari na waandishi wa habari hapa nchini sio maadui wa Rais Dk. John Magufuli bali adui yake ni yeye mwenyewe.

Alimtaka Rais Magufuli badala ya kukasirikia vyombo vya habari ambavyo vinafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha umma wa Watanzania, yeye binafsi ajitafakari na awe na akiba ya maneno pale anapozungumza.

“Sijui kilichomkasirisha Rais ni kitu gani, mimi binafsi nashangaa, anasema kalamu za waandishi ndizo zitasababisha mauaji ya halaiki kama ilivyotokea katika nchi za jirani, sio kweli, badala ya kurudia rudia kutamka mauaji ya kimbari ya Rwanda, sisi tunamwambia aache na aweke akiba ya maneno.

“Kama kiongozi wetu awe makini, awe mnyenyekevu na ajue hawezi kujua kila kitu, atuunganishe Watanzania, kwa sababu kile kilichotokea huko anakotolea kama somo ni matokeo ya utawala mbovu, ni itikadi ya jamii moja kujiona bora kuliko jamii zingine na ni matokeo ya wananchi kukosa matumaini,” alisema Zitto.

Pia alitumia fursa hiyo kuendelea kulaani kitendo kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam cha kuvamia Clouds Media huku akiwa na askari.

“Adui wa Rais Magufuli ni John Pombe Joseph Magufuli, ni kutokana na kuacha kutumia mifumo katika kutawala, matokeo yake viwanda havipanuki, ajira haziongezeki. Akirudi na kutumia mifumo atafanya vizuri.

“Serikali haitakiwi kuhangaika na watu wadogo wadogo waliowekeza mitaji yao na kuajiri wafanyakazi, wala haitakiwi kuwafilisi, bali inapaswa kuangalia, kujadili na kuziba mianya yote ya ukwepaji kodi unaofanyika katika nchi yetu,” alisema.

Akizungumzia dhana ya ujamaa, Zitto alisema tangu ujamaa ulipotupwa miaka 25 iliyopita pengo kati ya walionacho na wasio nacho limeongezeka na kiwango cha umasikini, hasa vijijini kinakua kwa kasi hali inayohatarisha umoja wa wananchi.

Kwa mujibu wa Zitto, hali hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na sera mbovu za CCM na Serikali yake na hakiwezi kukwepa lawama na shutuma kwani ndio chama kinachotawala hivi sasa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), alisema kuwa amepata maono mapya, kwamba ameona viongozi mbalimbali wa dini; masheikh na maaskofu wakichomwa moto kutokana na kutenda dhambi ya woga.
Lema alisema hayo wakati alipokuwa akitoa salamu za Chadema na kusisitiza umuhimu wa vyama vyote vya upinzani kuungana na kwenda kuwaelimisha wananchi madhara ya hofu na woga unaowakabili.

“Nimepata maono, nimeona viongozi wa dini, mashekhe na maaskofu wakichomwa moto wa jehanamu, nikamuuliza Mungu kwanini, mbona hawa wanachomwa moto, akanijibu kwa sababu ya dhambi ya woga,” alisema Lema.

Source:Gazeti la Mtanzania
 
Hakika hili ni neno na kila mmoja amkumbushe kila mmoja wetu ili ujumbe huu mzuri umfikie rais na marais waliopita tuizuie Tanzania yetu isiende inakoenda kwan imeshafika Uganda......
 
kasaka-300x151.jpg


MWANASIASA mkongwe ambaye alipata kuwa mwenyekiti wa kundi la wabunge waliohitaji muundo wa Serikali tatu (G55) wakati wa utawala wa awamu ya pili, Njelu Kasaka, amesema hakuna mtu aliye salama ndani au nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kauli hiyo aliitoa wakati wa mkutano mkuu wa kidemokrasia uliofanyika jana jijini Arusha ambako alikuwa mgeni mwalikwa.

Pasipo kutaja jina la mtu, Kasaka alitumia kauli hiyo kwa kugusia matukio ya kisiasa yaliyojiri katika siku za hivi karibuni.

Moja ya matuko hayo ni lile lililotokea katikati ya wiki hii kwa aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kukabiliana na changamoto ya kutishiwa bastola na mtu anayeaminika kuwa askari kanzu.

“Ingekuwa wakati CCM ilipokuwa imeshika hatamu, suala hili la RC wa Dar es Salaam tayari CCM ingekuwa imeishakaa na kumuelekeza Rais cha kufanya juu ya mkuu huyo wa mkoa,” alisema Kasaka.

Alisema siku hizi hali haiko hivyo ndiyo maana hata Katibu Mkuu wa CCM mwaka 2015 kabla ya uchaguzi mkuu, alitaka kodi kero zifutwe, lakini ndio kwanza zikaongezwa.

“Ni kwa kuwa CCM ya sasa haina nguvu hizo tena, wapinzani wakiungana na kuondoa tofauti zao wanaweza kuiondoa CCM madarakani,” alisema.

Kasaka ambaye amepata kuwa mbunge, waziri na mkuu wa mkoa, alijitoa ndani ya CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mbali na Kasaka, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema wamiliki wa vyombo vya habari na waandishi wa habari hapa nchini sio maadui wa Rais Dk. John Magufuli bali adui yake ni yeye mwenyewe.

Alimtaka Rais Magufuli badala ya kukasirikia vyombo vya habari ambavyo vinafanya kazi kubwa ya kuuhabarisha umma wa Watanzania, yeye binafsi ajitafakari na awe na akiba ya maneno pale anapozungumza.

“Sijui kilichomkasirisha Rais ni kitu gani, mimi binafsi nashangaa, anasema kalamu za waandishi ndizo zitasababisha mauaji ya halaiki kama ilivyotokea katika nchi za jirani, sio kweli, badala ya kurudia rudia kutamka mauaji ya kimbari ya Rwanda, sisi tunamwambia aache na aweke akiba ya maneno.

“Kama kiongozi wetu awe makini, awe mnyenyekevu na ajue hawezi kujua kila kitu, atuunganishe Watanzania, kwa sababu kile kilichotokea huko anakotolea kama somo ni matokeo ya utawala mbovu, ni itikadi ya jamii moja kujiona bora kuliko jamii zingine na ni matokeo ya wananchi kukosa matumaini,” alisema Zitto.

Pia alitumia fursa hiyo kuendelea kulaani kitendo kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam cha kuvamia Clouds Media huku akiwa na askari.

“Adui wa Rais Magufuli ni John Pombe Joseph Magufuli, ni kutokana na kuacha kutumia mifumo katika kutawala, matokeo yake viwanda havipanuki, ajira haziongezeki. Akirudi na kutumia mifumo atafanya vizuri.

“Serikali haitakiwi kuhangaika na watu wadogo wadogo waliowekeza mitaji yao na kuajiri wafanyakazi, wala haitakiwi kuwafilisi, bali inapaswa kuangalia, kujadili na kuziba mianya yote ya ukwepaji kodi unaofanyika katika nchi yetu,” alisema.

Akizungumzia dhana ya ujamaa, Zitto alisema tangu ujamaa ulipotupwa miaka 25 iliyopita pengo kati ya walionacho na wasio nacho limeongezeka na kiwango cha umasikini, hasa vijijini kinakua kwa kasi hali inayohatarisha umoja wa wananchi.

Kwa mujibu wa Zitto, hali hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na sera mbovu za CCM na Serikali yake na hakiwezi kukwepa lawama na shutuma kwani ndio chama kinachotawala hivi sasa.
Naye Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), alisema kuwa amepata maono mapya, kwamba ameona viongozi mbalimbali wa dini; masheikh na maaskofu wakichomwa moto kutokana na kutenda dhambi ya woga.
Lema alisema hayo wakati alipokuwa akitoa salamu za Chadema na kusisitiza umuhimu wa vyama vyote vya upinzani kuungana na kwenda kuwaelimisha wananchi madhara ya hofu na woga unaowakabili.

“Nimepata maono, nimeona viongozi wa dini, mashekhe na maaskofu wakichomwa moto wa jehanamu, nikamuuliza Mungu kwanini, mbona hawa wanachomwa moto, akanijibu kwa sababu ya dhambi ya woga,” alisema Lema.

Source:Gazeti la Mtanzania
Ufu 21:8 "woga ni dhambi....."
 
Watanzania wanatishwa wasidai haki zao kisa yaliyotokea Rwanda?.
Kama kiongozi kama kweli una huruma na watu wako,nchi yako basi TENDENI HAKI NA HAMTAONA MTU ANAWANYOSHEA KIDOLE.
Tofauti na hapo nitaamini kuwa hamuipendi nchi na watu wake
 
It is very true.

Kama imewezekana kwa Mheshimiwa mbunge wa CCM Nape Nnauye siku moja tu baada ya kuvuliwa uwaziri, akatolewa bastola na wanausalama wa nchi hii na kumwamuru arudi kwenye gari yake na haruhusiwi kufanya kikao kile na wale wanahabari ambacho dhumuni kuu lake lilikuwa kuwashukuru wanahabari kwa ushirikiano waliompa katika kipi
ndi alichohudumu kama Waziri wa Habari na Sanaa.

Sasa kama jambo hilo la kuinyeshwa bastola Mheshimiwa Mbunge wa CCM limefanywa hadharani mbele ya camera lukuki za wanahabari.

So what do you expect kwa sisi walala hoi wa mitaani?

Maana yake ni kuwa kwa kila mtanzania ambaye atataka kuikosoa serikali hii ya awamu ya 5, atakuwa anaishi katika mashaka makubwa.....

Ninachokiona kwa serikali hii ya awamu ya 5 ni ukiukwaji wa wazi wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibata ya 18 ambayo inatoa Uhuru kwa kila mwananchi kuweza kuwa na Uhuru wa kutoa maoni yake.
 
nimeupenda huu msemo `Adui wa Rais Magufuli n Joseph Pombe Magufuli'hahaha anaambili huyu adui make katiba inadai kuwa rais hashauriwi na mtu yoyote so sio raihc kushaurika kwan katiba inamruhusu kutopokea ushaur wa m2 yoyote! tatizo haya maneno kuntu ktk media platform wanaosoma asilimia wao husoma magazet ya udaku hasa wanawake na watu wa vjjn hawajui kuingia ktk mitandao kulingana na nature ya watanzania,ushaur wangu viongoz wa upinzan puuzen kaul ya rais ya kuto fanya mikutano mpaka 2020 il muende kumsemelea kwa raia huko vjjn lkn msipofanya hvyo wezenu wana2mia kaul ya elimu bure kuwa rubun wanavjj kwan mambo ya bombardier na flyover hata hawayajui huku kwe2!
 
Ni kweli aliye salama na ambaye anaweza kufanya chochote bila kukemewa ni Daudi bashite peke yake
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ufu 21:8 "woga ni dhambi....."
haswa.Watu wengi wanasubiri wakaungue tu kuliko kuwa wakweli.Na mimi nasikitika juu ya viongozi wa dini,Lakini baadhi Yao kama Gwajima na Kakobe moto wa namna hiyo hawata ungua.Wote kwa nyakati tofauti wametishiwa kufutiwa makanisa yao kwa sababu ya kuisema serikali inapo kosea
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom