Nje ya muungano Zanzibar haiwezi kushikamana

MLETAHOJA

Member
Apr 5, 2012
75
28
Pamoja na ukweli kuwa Wazanzibar wana matatizo ya msingi ambayo yameshindwa kupatiwa ufumbuzi kwa muda mrefu, na kwamba baadhi ya matatizo hayo yanatokana na muungano, kuna uwezekano mkubwa wa Zanzibar kushindwa kushikamana iwapo dai lao la kutaka kujitenga na Muungano litaafikiwa. Wanazo tofauti kubwa ndani ya vyama vyao vya siasa na visiwa vyao vya Unguja na Pemba ambazo hazijapatiwa suluhisho la kweli na la kudumu. Ndoa ya Cuf na CCM inaimarishwa na kuwepo kwa Bara inayoonekana kama adui wa pamoja (common enemy) wa pande hizo mbili (Cuf na CCM kwa upande mmoja na Unguja na Pemba kwa upande mwingine.) Nje ya muungano hiki kinachounganisha umoja wao sasa hakitakuwepo. Wananchi wa kawaida wanaweza kudhani mslahi yao yatapewa kipaumbele wakati huo lakini wasikumbuke kuwa hao wanaowasukuma kuelekea Zanzibar huru wana matarajio ya kujinyakulia fursa za kujineemesha binafsi ama na jamaa zao wa karibu fursa ambazo kwa sasa zinaminywa na kuwepo kwa muungano na hivyo wakajikuta wamehadaiwa kama baadhi yao walivyohadaiwa katika mashirikiano ya vyama vya CUF na CCM. Mimi kama mtanzania mpenda amani, ningemshauri Raisi Kikwete kwa kuwa ameonyesha nia ya kurejesha utulivu Zanzibar kwa hatua zake mbalimbali alizozichukua hadi sasa (ikiwa ni pamoja na kuruhusu mjadala wa katiba) aikamilishe nia hiyo kwa kuwapa watanzania fursa ya kuujadili muungano. Hapa tulipofika sasa hatuna uchaguzi ila kuujadili muungano. Tukiendelea na kujifanya hatuoni haja ya kuujadili muungano tutafika hatua mbaya zaidi. Tutatoka kwenye kubaguana kisiasa (angalao hilo ni historia kwa sasa huko Zanzibar) na kuingia kwenye kubaguana kiudini (hili linaendelea kwa kasi kwa sasa) na kuishia kwenye ubara na Uzanzibara (hili lilitabiriwa kutokea na kuna kila dalili za kuwezekana kutokea). Lakini pia tukiruhusu muungano uvunjike katika mazingira haya ya jazba tutashuhudia miungano mingine ya CUF na CCM na Unguja na Pemba ikisambaratika na kulazimika kuwa na kambi za wakimbizi Unguja, Mombasa ama Dar es Salaam. Kwa hekima yako Raisi Kikwete waweza kulinusuru hili lisitokee. Mungu ibariki Tanzania.
 
Mkuu umeona mbali kama mwewe waache hao wa znz wenye maono kama ya kuku wafurahie kujitenga
 
Yazanzibar waachiwe wenyewe Wazanzibar, kama Zanzibar wakijitoa kwenye Muungano, alafu wao wasiposhikana itatuhusu nini sisi Watanganyika?.

Kenya, Somalia, Burundi, Congo hawajashikana je sisi ugali wetu hatuli, fatilia maana ya msemo huu MCHUMA JANGA HULA NA WAKWAO.
 
Eti kisiwa kilikuwa Bara Arabia kikasukumwa na upepo hadi pwani ya Afrika Mashariki
Eti waarabu walipokuja ktk biashara ya utumwa walizaa na manyani wa porini huko Kigoma, Tabora, Mpwapwa, Kilosa, Bagamoyo na watumwa wanawake wa ziada waliwekwa Pemba km hasusa ya vijana (Shababy) toka Arabia waje osha nyota zao walipozaliwa watoto hao (waarabu koko) hawakuruhusiwa kwenda chafua damu huko ila wakae Unguja na Pemba
Kuna ahadi kuwa iko siku watasaidiwa na wajomba zao akiwemo Sultani aliyefurushwa na Karume
Kwa hiyo waangalieni waarabu hao hakuna Mbantu halisi kwani wana msemo PUNDA hapandi MUSCAT au Punda hawezi kuzaa na Farasi ila Farasi ndio ana haki ya kujamiiana na Punda
Kwa hiyo bila kibano hao watu sio wazuri wapewe kibano na kisiwa wasipewe watarudisha Utwana na Ubwana walla tatizo sio DINI
 
Yazanzibar waachiwe wenyewe Wazanzibar, kama Zanzibar wakijitoa kwenye Muungano, alafu wao wasiposhikana itatuhusu nini sisi Watanganyika?.

Kenya, Somalia, Burundi, Congo hawajashikana je sisi ugali wetu hatuli, fatilia maana ya msemo huu MCHUMA JANGA HULA NA WAKWAO.

Pamoja na muungano kunikera lazima nikiri pia kuwa Zanzibar matters, angalia Kenya na Somalia. Zanzibar ikiwa on fire, sisi ndo tutateseka na huo moshi.
 
Kwamba hawatokuwa na mshikamano, watabaguana, watasalitiana hizo zote ni non of our business(sisi Wabara) waacheni tu wajitenge, hivi kwanini tunawabembeleza?
 
Nje ya muungano hakuna sisi wanzanzibar wala sisi wa-bara bali kuna unguja na pemba,wanzanzibar wakitaka kuvunja muungano kwa ulevi hasa wa madaraka hawatakaa salama,ikumbuke muungano ndio unawaowafanya wajiite sisi wazanzibar--mwl jk nyerere

My vice:
Mtoto akililia wembe mpe,wacha watafute wanachokitaka! Hilo kundi la UHARISHO linawapotosha sana hao wala urojo.
 
Wa-Unguja hate watu wa Pemba na watu wa Pemba hate watu wa Unguja, but they both hate Tanganyika. Wakishaondoa 'common' enemy watarudi pale pale, Unguja & Pemba. Mungu tupe uzima.
 
zanzibar ni kisiwa likicho karibu na kenya na Tanganyika(Tanzania Bara) hivyo watu wa asili wa visiwa hivyo wametoka bara, wapo wanyamwezi, wanyakyusa( Mwakanjuki) and the like, wangoni Ukoo wa Hassan Nassoro Moyo, Jumbe Mngoni, Mwinyi anatoka Mkuranga, Karume-wamanyema, Wapemba wengi wa asili ya kiarabu, Muscat Oman na walikuja kwa ajili ya biashara na kupata nafasi ya kupumua baada ya kubanwa kama mjusi na waarabu wenzao, ndio kuzaa na dada zetu wakatokea waarabu koko, baada ya waarabu muscat oman kukosa wake, dada zetu wengine wamekuwa wakienda huko kuolewa na kufanyishwa kazi. Na agenda nyingine ni ile ya watu wengine kupenda kufaidika kupitia mgongo wa wengine sasa wapuuzi wachache bila kuelewa malengo ya wapiga propaganda hizi za uchumi na dinia , wanarukia bila kuelewa wakisha jitenga tu hao waarabu watangangania migongo yao ka ruba, au watawafukuza kwa kudai wao si wanzanibari, bali wanzanzibara. Miongoni mwao ni hao hao wanao ongea kwenye hiyo mihadhara ni mijitu majinga kweli kweli kisa kashata na harua wanazo pewa, kama kweli wao ni wapenda haki kweli au dini ya kiislamu ni ya wapenda haki jee utumwa wawanzanzibar ulifanywa na nani? kama sio waarabu. kama ni suala la haki na uislamu mbona Assad wa Syria anaua watoto na wanawake tena waislamu wenzie? na kama wana sema kuhusu haki na demokrasia mbona Assad na ukoo wake tu ndio wawe viongozi. au huo ndio uislamu.
 
Back
Top Bottom