Mada inahusika.
Fanyeni survey kote nchini uone namna ya baadhi ya wana CCM walivyojengeka kiburi linapokuja suala la haki na chaguzi huru. Ndivyo walivyo mara zote na kote si Bara wala Zanzibar.
Kupitia kunufaika na Dola kwa njia mbali mbnali wanajiona wana haki zaidi ya watanzania wengine.
Mentality hii imejengeka kwenye maeneo yote.
Hebu tazama kwa mfano Kwenye zoezi la uandikishaji, uchukuaji fomu, urejeshaji na kupiga kura wao kwa kutumia UCCM wanahitaji wasiulizwe na wafanye vile wanavyoona ndivyo. Si Polisi wala Usalama hawawasumbui na wanakosa ujasiri wa kuwaelekeza taratibu kwa hofu.
Kupitia utamaduni huo na kudekezwa siku yoyote sheria na haki ikitumika wanakosa furaha na kuhisi kuhujumiwa na hapo huanza mizengwe ya kuwaandama maofisa, Polisi, wakurugenzi na wengine wanaosimamia taratibu.
Kama kuna Jambo ambalo CCM Taifa imewakosea Watanzania ni kutengeneza Vijana waliolelewa kwenye upendeleo na kujazwa kwenye ajira za Umma. Hawa katu hawawezi kutenda haki.
CCM imetengeneza New generation ya siasa za vyama vingi kwa upendeleo kiasi cha kuiona HAKI na Kufuata taratibu kama nakama kwao na nje ya upendeleo na dhulma hawawezi kuishi.
Hii ni hatari kwa mustkabali wa Taifa.
Kwa mfano fuatilieni hali ya furaha waliyokuwa nayo wana CCM wakati wakurugenzi walipowakimbia wapinzani kwenye ofisi za umma na kushindwa kupokea fomu zao kwenye uchaguzi wa mitaa mwaka 2019.
Waoneni wanapofurahi hata kwenye Zoezi la kurejesha fomu kwenye uchaguzi mkuu huu wa 2020 na kufurahia figisu zinazowapa wapinzani huko majimboni.
Waoneni wanavyodiriki kutumia nafasi zao kuwakosesha haki za msingi watanzania wenzao kwa kutumia vyeo vyao wazi wazi.
Ni jambo la kawaida CCM kutumia nyenzo zote za Dola na Umma kujinufaisha kisiasa na wala hakuna Mipaka kwenye chaguzi ingawa wanapinga.
Kwa mfano huko Zanzibar imezoeleka kutumiwa vikosi vya SMZ kwenye shughuli za CCM kuanzia mikutano, mapokezi, maandamano n.k.
Huku Bara nako siasa hizi zimeanza kuota mizizi.
CCM wanaogopa haki na usawa na kwao wao bila upendeleo na dhuluma wanakosa furaha za chaguzi.
Tumieni uchaguzi mkuu huu wa 2020 kuwapima na kujiridhisha.
Kishada
Fanyeni survey kote nchini uone namna ya baadhi ya wana CCM walivyojengeka kiburi linapokuja suala la haki na chaguzi huru. Ndivyo walivyo mara zote na kote si Bara wala Zanzibar.
Kupitia kunufaika na Dola kwa njia mbali mbnali wanajiona wana haki zaidi ya watanzania wengine.
Mentality hii imejengeka kwenye maeneo yote.
Hebu tazama kwa mfano Kwenye zoezi la uandikishaji, uchukuaji fomu, urejeshaji na kupiga kura wao kwa kutumia UCCM wanahitaji wasiulizwe na wafanye vile wanavyoona ndivyo. Si Polisi wala Usalama hawawasumbui na wanakosa ujasiri wa kuwaelekeza taratibu kwa hofu.
Kupitia utamaduni huo na kudekezwa siku yoyote sheria na haki ikitumika wanakosa furaha na kuhisi kuhujumiwa na hapo huanza mizengwe ya kuwaandama maofisa, Polisi, wakurugenzi na wengine wanaosimamia taratibu.
Kama kuna Jambo ambalo CCM Taifa imewakosea Watanzania ni kutengeneza Vijana waliolelewa kwenye upendeleo na kujazwa kwenye ajira za Umma. Hawa katu hawawezi kutenda haki.
CCM imetengeneza New generation ya siasa za vyama vingi kwa upendeleo kiasi cha kuiona HAKI na Kufuata taratibu kama nakama kwao na nje ya upendeleo na dhulma hawawezi kuishi.
Hii ni hatari kwa mustkabali wa Taifa.
Kwa mfano fuatilieni hali ya furaha waliyokuwa nayo wana CCM wakati wakurugenzi walipowakimbia wapinzani kwenye ofisi za umma na kushindwa kupokea fomu zao kwenye uchaguzi wa mitaa mwaka 2019.
Waoneni wanapofurahi hata kwenye Zoezi la kurejesha fomu kwenye uchaguzi mkuu huu wa 2020 na kufurahia figisu zinazowapa wapinzani huko majimboni.
Waoneni wanavyodiriki kutumia nafasi zao kuwakosesha haki za msingi watanzania wenzao kwa kutumia vyeo vyao wazi wazi.
Ni jambo la kawaida CCM kutumia nyenzo zote za Dola na Umma kujinufaisha kisiasa na wala hakuna Mipaka kwenye chaguzi ingawa wanapinga.
Kwa mfano huko Zanzibar imezoeleka kutumiwa vikosi vya SMZ kwenye shughuli za CCM kuanzia mikutano, mapokezi, maandamano n.k.
Huku Bara nako siasa hizi zimeanza kuota mizizi.
CCM wanaogopa haki na usawa na kwao wao bila upendeleo na dhuluma wanakosa furaha za chaguzi.
Tumieni uchaguzi mkuu huu wa 2020 kuwapima na kujiridhisha.
Kishada