Nje au Nyumbani

Papa

New Member
Oct 10, 2007
2
0
Watanzania wamekuwa wakimbilia nje kuhangaika na maisha maruri lakini kumbuka maisha mazuri yako nyumbani kwako- kwani wengi wao wanaokimbilia nje hawana kisomo kilicho makini na huishia mitaani na kujikuta kwenye matatizo makubwa mno

Nawaambeni watanzania wenzangu kuwa makini kabla huja amua kukimbilia nje

Mimi nimeishi nje ya nchi kwa takiribani miaka 16 sasa na sijaona kuliko kuzuri zaidi ya Tanzania nimetembea nchi zaidi ya 12

Bongo bado bomba Nyumbani ni nyumbani tuu


Papa kula nao
 
Mheshimiwa, nakuomba ueleze kwa kina ni jinsi gani ulikwenda nje ya Tanzania na ni nchi zipi ulipitia au kuishi na ni mafanikio gani umepata.

Pili, unakosea unapojumisha kwamba wote wanaokwenda nje ya nchi wanakimbia nchi yao na kwamba hawana elimu ya kutosha, kwa hili natofauitana nawe na naona - "you have lost the plot".

Kuhusu "point" yako ingine kwamba watu wawe makini wanapokimbilia nje ya nchi, hii pia wewe hauko makini kwa kuzingatia hujaeleza ni umakini gani wewe uliufanza kabla ya kwenda nje ya nchi na ni vipi umekuwa makini kwa miaka 16 nje ya nchi.

Pia unasema katika nchi ulizotembelea hujaona kilicho kizuri kama vile vya nyumbani Tanzania, hapa nakuomba uwe "very serious" na kauli hii.

Sikatai kwamba kuna baadhi ya mambo ya kupamba Tanzania hasa Dar-es-Salaam, ili ionekane kwamba hio ndio Tanzania lakini watu wamekosa hata miundo mbinu mizuri ya hata kulela mazao yao kwenye masoko kwa muda unaotakiwa. Angalia "blog" ya Maggid Mjengwa utaelewa namaanisha nini.

Mwisho, hakuna anaekataa kwamba Tanzania alikozaliwa ni nyumbani kwake ila kutokana na utofauti wa mambo mazuri na mabaya kwa pande zote mbili bado mtu ambae anaruhusiwa kuishi majuu kihalali, ana uchaguzi kwamba ni wakti gani aje nyumbani iwe likizo tu au kuhamia kabisa.

Naomba kutoa hoja.
 
papa at 2:34pm said:

Maoni kuhusu Biashara E-Africa

Mimi ni mtanzania naishi South Africa nataka kujua kuna biashara gani naweza wekeza E-Africa

Nipe maoni na mifano ilio hai

Kula nao Papa

After exactly 10 minutes he has managed to travel to Tanzania Mhhh Mhhhh.................
papa 2:44pm said:

Nje au Nyumbani

Watanzania wamekuwa wakimbilia nje kuhangaika na maisha maruri lakini kumbuka maisha mazuri yako nyumbani kwako- kwani wengi wao wanaokimbilia nje hawana kisomo kilicho makini na huishia mitaani na kujikuta kwenye matatizo makubwa mno

Nawaambeni watanzania wenzangu kuwa makini kabla huja amua kukimbilia nje

Mimi nimeishi nje ya nchi kwa takiribani miaka 16 sasa na sijaona kuliko kuzuri zaidi ya Tanzania nimetembea nchi zaidi ya 12

Bongo bado bomba Nyumbani ni nyumbani tuu

Papa kula nao

Karibu JF.
 
..nyumbani maisha huwa nafuu[kwa maana ya kupata support ya ndugu na jamaa pale unapokwama]na hivyo kuvumilika zaidi ya nje!

..nyumbani mtu huwa huru zaidi kuvinjari maeneo mbalimbali bila kuogopa kutengwa au kubaguliwa!

..nyumbani kuna umasikini pia!

..nyumbani watu wengi hawana mwamko wa maendeleo ya kweli[bali maneno]!

..nyumbani tunajidanganya sana tukifikiri mabaya tunayofanya yatapotea kama moshi wa moto!kumbe hubakia kama historia!

..nyumbani ni kwako,unakaribishwa uje tembelea,tena na tena!

..sasa hiyo inategemea!kama umejilipua je?
 
Papa message yako iko too General, na si sahihi kabisa; kama ulienda kwa staili ya ujanja ujanja ulitegemea nini?
Kumbuka dunia ya sasa ni kama kijiji, unaweza izunguka kadri unavyotaka, ILA TU inabidi iwe ni kwa shuguli mbadala au kusoma na vitu kama hivyo, sio kubahatisha;
 
Watanzania wamekuwa wakimbilia nje kuhangaika na maisha maruri lakini kumbuka maisha mazuri yako nyumbani kwako- kwani wengi wao wanaokimbilia nje hawana kisomo kilicho makini na huishia mitaani na kujikuta kwenye matatizo makubwa mno

Nawaambeni watanzania wenzangu kuwa makini kabla huja amua kukimbilia nje

Mimi nimeishi nje ya nchi kwa takiribani miaka 16 sasa na sijaona kuliko kuzuri zaidi ya Tanzania nimetembea nchi zaidi ya 12

Bongo bado bomba Nyumbani ni nyumbani tuu


Papa kula nao

Kuna kipengele katika katiba ya Tanzania kinachosema kwamba "Mtanzania yuko huru kwenda mahali popote pale duniani ili mradi havunji sheria." Watanzania wengi walio nje wametumia kifungu hiki na hawakuvunja sheria yoyote.

Hii dhana yako ya kwamba "wamekimbilia nje" ni ya mwaka 47 sasa hivi tuko 2007 na mambo yote ni utandawazi (globalization). Mtu anayekimbia kwao ni muhalifu ambaye anaogopa kukamatwa kwa makosa aliyoyafanya. Watanzania wengi walio nje si wahalifu na ni wachapa kazi wazuri tu na baadhi ya nchi wanataka Watanzania zaidi wenye utaalamu wenye soko katika nchi.

Watanzania wenye elimu ya juu katika fani mbali mbali wamegundua kwamba kuna nchi nyingi hapa duniani ambazo zinahitaji utaalamu wao na mishahara ni mizuri kabisa inayokuwezesha kulipa gharama zako muhimu za kila mwezi na pia kuweka akiba au kuinvest baadhi ya mapato yako.

Pia Watanzania walio nje huwa wanakuja Tanzania kwa likizo na pia wana ndugu zao, jamaa na marafiki ambao huwapa habari zote zinazojiri ndani ya Tanzania, hawahitaji msaada wako kujua kama Bongo ni bomba au la. Kama mambo ni bomba inakuwaje Watanzania katika kona mbali mbali wameanza kuwazomea viongozi? tabia ambayo hatujawahi kuiona tangu tupate uhuru karibu miaka 46 iliyopita. Je kulikoni?

Waswahili wanasema, "bahati ya mwenzio usiilalie mlango wa wazi" hizo nchi 12 ulizopitia wewe labda hazihitaji fani uliyosomea hivyo ukawa unapiga lami tu, baadhi wameishi nchi moja tu na wanapeta kama kazi na matunda ya elimu yao wanayaona na wana vyeo vikubwa tu lakini wengi wao hawapendi kupiga tarumbeta ili kujisifia mafanikio yao.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom