NJAA YAJA: Dear Mr. President, On a Serious Note...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Ndugu zangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba itakapofika kiangazi mwaka huu, Taifa letu linaweza kujikuta kwenye upungufu mkubwa wa chakula ambao siyo tu unatishia maisha ya watu wetu bali pia unashusha hadhi na utu wa mwanadamu. Hakuna kitu kinachomdhalilisha mwanadamu na kuweza kumfanya awe mtu kama njaa.

Ni njaa ndiyo inayoweza kumfanya mtu aukane urithi wake wa kwanza kama alivyofanya Esau na ni njaa ambayo ilikuwa inatumika tangu enzi za kale kama silaha ya mwisho ya vita ambayo inalazimisha watu kusalimu amri.

Tanzania tutakabiliwa na njaa ambayo chanzo chake si ukame. Mara nyingi (kama siyo zote) njaa husababishwa na ukame na vita. Hata hivyo njaa ambayo naweza kuiangalia toka mbali na inayosogelea kama simba anyatiaye haitokani na mambo hayo bali makubwa mawili.

a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.

b. Mvua ya masika.
Hata hivyo naamini kwa upande wa Tanzania kitakachosababisha njaa sana ni hii mvua ambayo imeharibu mashamba na mazao ya watu kiasi kwamba baadhi ya maeneo ambayo kwa kawaida yana chakula cha kutosha yanaweza kujikuta yanahamia mwaka huu. Kama mpunga wa Kyela utakuwa umeathirika kama Dr. Mwakyembe alivyosema kwenye mahojiano yake nami kuna uwezekano kuwa Mwaka huu bei ya Mchele nayo itapanda na hivyo kufanya nafaka hiyo ianze kuwa adimu na kupatikana kwa wachache.

Maeneo ambayo mchele ndiyo chakula kikuu na pia zao la biashara watajikuta wanakabiliwa na upungufu wa fedha za kununulia hata vitu vingine na hivyo kusubiri chakula cha misaada.

Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?
 
Yeah niliona juzi IMF walitoa tahadhari especially nchi za Africa kuwa chakula kitapanda maradufu. Nafikiri wananchi waelimishe mapema ili mwenye kagunia kake ka mpunga akaifadhi vizuri maana hii itakuwa ni tatizo la dunia na sio taifa tunaweza kukosa mtu wa kumlilia kutusaidia kama tulivyozoea
 
najua watu wanapenda habari za ufisadi na kashfa lakini kama kuna kitu muhimu cha kujiandaa nacho ni hili suala la njaa. Najua wengi tumeshiba huku tuliko na hatuna wasiwasi tunakoromea mafisadi na kumkoma nyani giledi kutoka katika comfort of our cozy rooms and comfortable lifestyles.

Hata hivyo kwa mamilioni ya ndugu zetu njaa inadhalilisha na kutweza kwelikweli. Je mtu mmoja mmoja, jamii, na taifa lijiandae vipi au tusubiri hadi wapite na kuomba omba tena? Tukizingatia kuwa mwaka huu hatutakuwa peke yetu katika kuomba omba huko.
 
M.M.M, hapo umesema sawa kabisa.... Kuhusu effect ya haya mimi niliyakuta mwishoni mwa March 08 nilipoenda na Mama kufanya manunuzi nikakuta Mchele wa Kyela umepanda from 900/1000 mpaka 1300/1600 na hii ilikuwa ni pale Sokoni Kisutu. So kukujibu ni kwamba ndio bei zimeeanza kupanda Mkulu.

Hili la kupanda bei za chakula duniani ni sawa lakini kwa haraka inaelekea sisi litautgusa vibaya sababu kuna thread tayari nilichangia nadhani leo asubuhi kuhusu Wassira kupiga marufuku uagizaji wa matunda na mbogamboga... Mtiririko wa hoja humu jamvini umenipelekea kuamini kwamba sisi kama nchi "Hatuna mpango endelevu wa kilimo"... niligusia kuhusu tofauti ya wakulima na vipaumbele kati ya mazao ya bishara na chakula etc.....
 
Ndugu zangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba itakapofika kiangazi mwaka huu, Taifa letu linaweza kujikuta kwenye upungufu mkubwa wa chakula ambao siyo tu unatishia maisha ya watu wetu bali pia unashusha hadhi na utu wa mwanadamu. Hakuna kitu kinachomdhalilisha mwanadamu na kuweza kumfanya awe mtu kama njaa.

Ni njaa ndiyo inayoweza kumfanya mtu aukane urithi wake wa kwanza kama alivyofanya Esau na ni njaa ambayo ilikuwa inatumika tangu enzi za kale kama silaha ya mwisho ya vita ambayo inalazimisha watu kusalimu amri.

Tanzania tutakabiliwa na njaa ambayo chanzo chake si ukame. Mara nyingi (kama siyo zote) njaa husababishwa na ukame na vita. Hata hivyo njaa ambayo naweza kuiangalia toka mbali na inayosogelea kama simba anyatiaye haitokani na mambo hayo bali makubwa mawili.

a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.

b. Mvua ya masika.
Hata hivyo naamini kwa upande wa Tanzania kitakachosababisha njaa sana ni hii mvua ambayo imeharibu mashamba na mazao ya watu kiasi kwamba baadhi ya maeneo ambayo kwa kawaida yana chakula cha kutosha yanaweza kujikuta yanahamia mwaka huu. Kama mpunga wa Kyela utakuwa umeathirika kama Dr. Mwakyembe alivyosema kwenye mahojiano yake nami kuna uwezekano kuwa Mwaka huu bei ya Mchele nayo itapanda na hivyo kufanya nafaka hiyo ianze kuwa adimu na kupatikana kwa wachache.

Maeneo ambayo mchele ndiyo chakula kikuu na pia zao la biashara watajikuta wanakabiliwa na upungufu wa fedha za kununulia hata vitu vingine na hivyo kusubiri chakula cha misaada.

Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?

Sababu nyingine ni mzee bush na kijana wake Gordon brown wamekwiba raslimali zetu kwa kigezo cha mashirika ya huko kuwekeza kumbe wanapora.Ambapo zingeongeza pato la Taifa.
 
Why tuwe na njaa? Sielewi kabisa...

Ngabu,

ninatafuta ile story ilikuwa kwenye wire (AP) jana kuwa nchi za magharibi zinategemea kuwa ukosefu wa chakula au bei juu ya vyakula itapelekea kuanguka kwa regimes wasizozipenda.

Sitaki kuamini kwenye conspiracies but sikujua hiyo story ya AP ilikuwa inalenga kwenye nini?!?!?!
 
Ngabu,

ninatafuta ile story ilikuwa kwenye wire (AP) jana kuwa nchi za magharibi zinategemea kuwa ukosefu wa chakula au bei juu ya vyakula itapelekea kuanguka kwa regimes wasizozipenda.

Sitaki kuamini kwenye conspiracies but sikujua hiyo story ya AP ilikuwa inalenga kwenye nini?!?!?!

Kwani hii itakuwa mara kwanza kuwepo kwa ukosefu wa chakula? Kama imefikia hatua ya hadi kukosa chakula ndipo regimes zianguke basi bana....mi nanyoosha mikono....bora niendelee kuwa na msosi na kuyaacha mafisadi kama yalivyo. Sitaki kufa njaa miye....
 
Jamani ni kweli huko DSM bei za misosi zimekuwa hazishikiki. Embu chekini hii habari

Ni vizuri kwa waliokuwepo TZ waanze kujitayarisha kwa kujiwekea akiba. Naomba hizi mvau zisije haribu mashamba ya wakulima wa Pamba kule Kanda ya Ziwa, maana bei za mwaka huu zitakuwa alahamdulilah na kuwawezesha kuweza angalau kuondoka kwenye poverty line.

Bei ya vyakula sasa yatisha

2008-04-14 09:22:43
Na Lucy Lyatuu


Bei ya vyakula jijini Dar es Salaam imepanda maradufu kutokana na kuongezeka kwa gharama za mafuta ya petroli na dizeli pamoja na barabara kuharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Uchunguzi uliofanywa na Nipashe jana jijini Dar es Salaam kwenye baadhi ya masoko, ulibaini kuwa bidhaa nyingi zimepanda na kusababisha wananchi wenye kipato cha chini kuwa katika hali ngumu.

Katika soko la Kisutu, Kariakoo, Mwananyamala na Tandale, bei ya mchele imepanda kutoka wastani wa Sh. 1,000 kwa kilo hadi kufikia Sh. 1,500 ambapo maharage (soya) kwa kilo yaliuzwa Sh. 1,700 badala ya Sh. 900.

Aidha, karanga kwa kilo ziliuzwa Sh. 1,500 badala ya 1,000, choroko Sh. 1,500 badala ya Sh. 1,200, unga wa sembe Sh. 800 badala ya Sh. 550 kwa kilo, viazi viliuzwa Sh. 800 badala ya 500 na vitunguu Sh. 800 badala ya 500.

Aidha, gunia la viazi kwa sasa linauzwa Sh. 27,000 badala ya Sh. 22,000, nyanya boksi moja Sh. 35,000 badala ya Sh. 20,000 wakati vitunguu nusu gunia vinauzwa Sh. 60,000 tofauti na Sh. 45,000
.

Akizungumza kutoka soko la Kariakoo jijini, Bw. Joseph Moses, alisema ni kweli mazao ya chakula yamepanda na sio mara ya kwanza kwani katika msimu wa mvua barabara nyingi zinakuwa hazipitiki na mafuta kutumika kwa wingi.

``Miundombinu ya barabara iliyopo ni mibovu huko vijijini kunakotoka chakula, ndio sababu kuu ya kupanda kwa bei ya mazao kutoka kwa wakulima mashambani kwani ufikishaji wake sokoni unakuwa mgumu,`` alisema.

Aliongeza kuwa chanzo kikuu cha kumfikishia mlaji wa mwisho bidhaa kinatokana na usafiri na hivyo kupanda kwa bei ya mafuta, petroli na dizeli, nako kumechangia ongezeko la bei ya bidhaa sokoni.

Naye Bw. Makengwaa Idrisa, Mfanyabiashara wa Kisutu alisema tatizo kuu linalowakabili wafanyabiashara ni kupanda kwa mafuta kila mara.

Alitoa ushauri kwa ngazi zinazohusika kufuatilia au kutafuta suluhisho la bei hizo ili kwamba kudhibiti bei holela ya bidhaa sokoni.

Kwa upande wake, Bw. John Anthony, Mfanyabiashara wa Tandale alisema ni kweli bidhaa nyingi sokoni zimepanda kutokana na mpaka wa Tanzania na Kenya kufunguliwa.

``Wakati Kenya wakiwa kwenye mgogoro wafanyabiashara walielekeza nguvu nyingi kuleta bidhaa zao jijini Dar es Salaam, lakini baada ya kumalizika kwa ugomvi sasa wanaingia kwa wingi nchini humo hali inayofanya bidhaa kupungua Dar na kukosekana ushindani, hali ambayo inapandisha bei,`` alisema Bw. John.

Naye Bw. Jabir Richard mfanyabiashara wa Mwananyamala, alisema bidha zimepanda na kwamba bado zinaweza kuendelea kupanda kutokana na kupanda kwa gharama za mafuta na pia kumalizika kwenye maghala.

Alisema ni kawaida wakulima kuuza vyakula kwa bei ya juu hasa kipindi hiki ambacho wanasubiri mavuno, hali ambayo hufanya wale wasafirishaji nao kupandisha gharama zao.

SOURCE: Nipashe
 
Hii sasa kali, njaa dunia nzima. Nadhani Serikali yetu inapaswa kuimarisha kitengo cha SGR (strategic grain reserve) ipewe hata vile vihenge vya Kihesa Iringa, vilivyotelekezwa baada ya mafisadi kuua NMC. Fedha zilizorudishwa za EPA (kama zipo) zitumike kuimarisha kitengo hiki.

Kilimo cha nafaka kipewe kipaumbele zaidi tuachane na jatrofa. Hii ni pamoja na kupeleka watalaam katika bonde la mto Kilombero, bonde la Usangu nk (hakuna mafuruko maeneo hayo). pamoja na mbinu nyingine. Hakuna sababu ya Tanzania kulia njaa.
 
Kwani hii itakuwa mara kwanza kuwepo kwa ukosefu wa chakula? Kama imefikia hatua ya hadi kukosa chakula ndipo regimes zianguke basi bana....mi nanyoosha mikono....bora niendelee kuwa na msosi na kuyaacha mafisadi kama yalivyo. Sitaki kufa njaa miye....

Inaonekana for now hii ndio the only option. Wakati haya yote yakitokea, mkuu wa kaya yuko bize akizunguka dunia. What a shame!
 
hili tatizo la njaa huenda likaja kuwa kubwa zaidi huko mbeleni kutoka na nafaka kuwa zitatakiwa kwa wingi kutengeneza biofuel, ili kureplace petrol, nahofia kwamba ili biofuel ya kutosha iweze kutengenezwa, nafaka kama vile mahindi na mpunga zitatakiwa sana, kwa hiyo competetion kubwa itakuwepo,baina ya nafaka kwa ajili ya chakula na nafaka kwa ajili ya kuzalisha hiyo biofuel!.

Watanzania tunatakiwa kujiandaa vya kutosha kuhusiana na hali hii. kilimo cha nafaka kitiliwe mkazo sana badala ya kutegemewa uagizaji wa mpunga kutoka nje
 
On top of all that has been pointed out, there is China on the east and the Ethanol hoopla on the west.

In the east China's 1.3 billion plus population is now changing it's lifestyle, consuming more than it ever did and moving from the ageless habit of almost complete vegetarinism into eating meat.

One argument for vegetarianism is that it takes more grains to feed animals for human consumption than it would take to feed human directly.Thus if it will take one ton of corn to directly feed a village for a month, it may very well take four to five tons of corn to feed cows for human consumption lasting a month, eating meat is a very uneconomic use of resources.

In the west the big ethanol debate, which is looked upon as a lucrative opportunity for farmers, especially in middle American farming states such as Iowa, fueled by already record high oil prices, speculations,the need to move away from oil dependency especially due to oil geopolitics and the need for an alternate and environmentally friendly fuel is raising the price of corn and the demand for other substitute grains, hence raising the price level of all grains by proxy.

So on top of the usual vagaries of weather, we have all these global factors to deal with.

I'm all for an all nutrients/minerals/proteins/energy pill, sorta like the one-a-day of food.

Eating is such a messy process anyway.
 
You are not suggesting that we should stop eating now my dear Pundit!.. LOL.. well tufanye nini kujiandaa, mimi sipendi maisha ya kubahatisha as if everything is in "God's hand"
 
Sie tuna cha kufanya tena? Si tunasubiri "international pressure" kama alivyojisemea PM Pinda?

Futurology is risky business, but I would bet on whoever can come up with a system to engineer the body to produce less waste and use 95% plus of our intake, then move to cheap ndonge (vitamins/proteins/minerals energy, then we will all eat cardboard (disguised as special biscuits) for roughage) and patent the whole bizz to be the first trillionaire.

I know there will be a nostalgic feeling about food, taste and smell, but it will be so expensive only the super rich will afford to eat.

I must be sounding like one of A.C. Clarke's doomsday prediction, but 200 years from now, the soil polluted, the temperature sky high, rivers full of toxins, the ozone hole almost not a hole anymore who is to say this won't become a reality?

What am I trying to do forecasting 200 years while we don't know from where will the next budget come.
 
Back
Top Bottom