kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,298
- 12,600
Hakuna ubishi sasa hivi mafisadi yamebanwa kwenye kona mbaya, yanalalamika kwa kuzibiwa vichochoro vyao vya kupiga madili.
Bila shaka kwa miaka 10 ya Rais Magufuli madarakani yatakuwa yamedhoofu kwa njaa, kiu na kuishi kama mashetani, wanatamani miaka 10 ya Rais magufuli ipite haraka kama upepo.
Hofu yangu mimi ni baada ya miaka 10 ya Mh. Magufuli kumalizika kwa mujibu wa katiba yetu. Je, nini kitafuata ili kuendeleza moto aliouwasha JPM dhidi ya ubadhilifu nchini baada ya yeye kumaliza muda wake Ili juhudi za JPM zisipotee bure kama vile zilivyopotea zile za Mwl. Julius K. Nyerere (rip) baada ya kung'atuka urais 1985 watu wakakimbilia kulinyonga Azimio lake la Arusha na kuunda Azimio la Zanzibar?
Ni heri JPM atengeneze polepole utaratibu, chombo na mfumo ambao utakuwa na uwezo wa kupambana wenyewe na ufisadi na uvivu kabla hajamaliza kipindi chake badala ya kutegemea juhudi na ufundi wa mtu binafsi.
JPM anaifahamu vilivyo mianya iliyoko kwenye katiba na sheria zetu ambayo ni rahisi kutumiwa na watawala wenye nia mbaya, afanye kazi ya kuiziba polepole wakati anaelekea mwaka 2025, vingine majizi haya ambayo yatawekwa na njaa na hasira za miaka 10 ya JPM siku yakibahatika kuikamata Ikulu tena hakiyamungu taifa litakujajuta.
Bila shaka kwa miaka 10 ya Rais Magufuli madarakani yatakuwa yamedhoofu kwa njaa, kiu na kuishi kama mashetani, wanatamani miaka 10 ya Rais magufuli ipite haraka kama upepo.
Hofu yangu mimi ni baada ya miaka 10 ya Mh. Magufuli kumalizika kwa mujibu wa katiba yetu. Je, nini kitafuata ili kuendeleza moto aliouwasha JPM dhidi ya ubadhilifu nchini baada ya yeye kumaliza muda wake Ili juhudi za JPM zisipotee bure kama vile zilivyopotea zile za Mwl. Julius K. Nyerere (rip) baada ya kung'atuka urais 1985 watu wakakimbilia kulinyonga Azimio lake la Arusha na kuunda Azimio la Zanzibar?
Ni heri JPM atengeneze polepole utaratibu, chombo na mfumo ambao utakuwa na uwezo wa kupambana wenyewe na ufisadi na uvivu kabla hajamaliza kipindi chake badala ya kutegemea juhudi na ufundi wa mtu binafsi.
JPM anaifahamu vilivyo mianya iliyoko kwenye katiba na sheria zetu ambayo ni rahisi kutumiwa na watawala wenye nia mbaya, afanye kazi ya kuiziba polepole wakati anaelekea mwaka 2025, vingine majizi haya ambayo yatawekwa na njaa na hasira za miaka 10 ya JPM siku yakibahatika kuikamata Ikulu tena hakiyamungu taifa litakujajuta.