Njaa Somalia: Je, Tanzania itoe msaada kwa hawa wenzetu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
article-2019268-0D2BCEDF00000578-452_634x464.jpg
Desperate: Seven-month-old Mihag Gedi Farah weighs just 7lbs and was hours from death after arriving at a field hospital in Dadaab, Kenya


Ukiondoa Kenya na baadhi ya nchi za karibu ambazo zimejikuta na wakimbizi wa Somalia hasa kutokana na baa la njaa ni nchi chache za Kiafrika zimejitokeza kutoa misaada - as a matter of fact sijaona bado ni nchi gani. Tumekuwa na haraka kweli tunapoona nchi za magharibi zinakuja kutuondolea madikteta wetu na kuwakemea mara moja - ooh tuachieni Afrika tutatue matatizo yetu. Hatuchelewi kupeleka ujumbe Libya, Ivory Coast n.k ili kujionesha kuwa tunaweza kutatua matatizo yetu na kusaidiana wenyewe.

Then comes Somalia. Ukiondoa matatizo mengine ya nyuma hakuna tatizo ambalo linagusa nafsi ya mwanadamu na utu wake kama njaa. Vita haikaribii njaa kwa madhara yake. Lakini inashangaza, hatujasikia viongozi wa Afrika wakimobilize watu wao kusaidia chakula huko! Hata sisi Tanzania hatujasema tunatoa japo msaada wa fedha au chakula - si kwamba hatuna uwezo. Lakini hadi hivi sasa ni hawa hawa wazungu tusiotaka watusaidie kwenye madudu yetu mengine wamekuwa tena wa kwanza na kwa nguvu zaidi kutoa misaada ya chakula.

Tatizo letu ni nini hasa? Wakati Somalia wanakufa njaa, sisi tulikuwa na mashindano ya kula sana pale Morogoro; wakati Somalia wanakufa njaa sisi tunaendelea na mizunguko ya Fiesta! Ooh sina tatizo na sherehe hizo au watu kufurahia lakini can we be a little bit responsible nation miaka 50 baada ya uhuru wetu? I'll share you a short story, hotuba ya Nyerere.

Our friends in Kenya are being prosecutedfor alleged offences arising from their efforts to oppose the Lennox-Boyd constitution. Our National Executive sent a cheque of Shs. 5000/- to those friends to help towards legal defence expenses and also called upon the country to fast and pray on the 27 May, and stop smoking for two days- 27 and 28 May

At the same time our Nyasaland brothers appealed to us for financial help to enable them to send a delegation to the United Kingdom to put their case for constitutional reforms. TANU has already sent to Nyasaland African Congress sufficient money to pay for a return ticked for once delegate.

Imperialists agents are complaining again. Not because they know that is is a sacrifice for our poor membership to give this very little financial help to our brethren in need; but because they do not like what all thi smeans: for it means African solidarity on a wider scale. If the Africans of Africa unite imperialism must go.

We pray for the safety and success of our brethren in Keany and Nyasaland, and in fact wherever they may be engaged in this struggle to add to the world's sum total of freedom and human dignity by restoring that freedom and dignity to this great continent of ours- AFRICA - Sauti ya TANU, 20 Juni, 1958

Najiuliza; were we in a better position to help our brothers in Kenya and Nyasaland (now Malawi) then than now? Kama matatizo ya uhuru tuliyaona yanatuhusu hivyo, je matatizo ya chakula hayatugusi hivyo? Najiuliza, kuna kiongozi yeyote Tanzania anayeweza kutoa wazo hili na kulisimamia simply kwa ajili ya utu wa mwanadamu? Si kwamba katiba yetu inasema "kila mtu (haisemi kila Mtanzania) anastahili haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake"?

Nauliza: Makanisa, na Misikiti yetu wako wapi kutekeleza wito wao wa kusimama na wale wenye njaa na shida? Nauliza, makundi ya vijana ma wanaharakati wetu, wako wapi?

Kwa upande wangu, I'll do something, the only little thing I know I can do. Siwezi kuangalia macho ya huyo mtoto na kuendelea kula kama kawaida. NI DHAMBI dhidi ya uanadamu wake.
 
Mosi, hiyo picha inatisha. Ungeweka angalizo kama 'viewer discretion is advised' ingekuwa bomba.

Pili, niseme nini tena. Unauliza mbona Waafrika hatusimami kusaidia Waafrika wenzetu....hahaaa....ningesema lakini nishasema sana hadi nimechoka.
 
Mosi, hiyo picha inatisha. Ungeweka angalizo kama 'viewer discretion is advised' ingekuwa bomba.

Pili, niseme nini tena. Unauliza mbona Waafrika hatusimami kusaidia Waafrika wenzetu....hahaaa....ningesema lakini nishasema sana hadi nimechoka.

Mzee, ndio maana nimeweka hiyo picha.. kati ya mtu kushtuka na huyo mtoto kutuangalia nadhani, yeye anatakiwa asione picha za sisi tulioshiba, atashtuka. Wouldn't you agree?
 
  • Thanks
Reactions: ral
Mkjj hujui kwamba sisi ni masikini hahahaha!!!!! sisi ni watu wa kusaidiwa bana si kusaidia afteralll kwani Marekani, Uingereza wamegoma kusaidia hahahahah!!

Nacheka lakini kwa uchungu, kuna watu wanaweza kuwa wanamshangaa JK kwenye hili wakati hili ni jukumu la kila mmoja kama mwananchi, people can mobilize themselves in small groups wakachangia chochote walicho nacho na kuchannel thru say RED CROSS.
 
Mzee, ndio maana nimeweka hiyo picha.. kati ya mtu kushtuka na huyo mtoto kutuangalia nadhani, yeye anatakiwa asione picha za sisi tulioshiba, atashtuka. Wouldn't you agree?

Mkuu hiyo picha, is it a kid au mzee? It's really shocking! 7 months????? Unaweza fikiri mzee wa miaka 70 akiwa anaishia kwa ngoma!!!!!!
 
Wanasema a picture worth 1000 words, nashukuru kwasababu nimeliongelea kwa hoja ya 'Je ile kauli mbinu ya matatizo ya Afrika yanahitaji suluhu ya Afrika' inayotumiwa na AU ina maana!

Tunalaani uvamizi wa nchi za magharibi kwa mapovu midomoni tukitetea Libya, Ivory coast n.k. vema! Je hili la njaa halihitaji AU.

Sisi ni wanafiki nasema bila kuuma maneno. Kwanini tulumbane kwenye mablog, magazeti ,warsha na semina kuhusu neo-colonialism wakati wakoloni hao hao sasa ndio wapo Somalia wakigawa chakula. Sisi tupo wapi kwenye matatizo kama haya.

Je ina maana watoto wanaokufa kwa vita ni bora kuliko wanokufa kwa njaa?
Je miaka 30 bado tunamsubiri Harry Belafonte na akina Lionel Rich waje kuimba ili kusaidia wenzetu.

Kuna 'moral authority gani kwa mawaziri wa mambo ya nje kama akina Mh Membe kukimbia huku na huko ili kumuokoa Gaddhafi ili hali watu wanakufa Somalia na wao wapo Dodoma.

Wale wanaowapa Alshaabab silaha wako wapi kuwapa chakula. Wale waliokuwa wanapigania Sudan kusini ijitenge wapo wapi kusaidia Somalia?

Kwanini hatulalamikii uvamizi wa mgharibi nchini Somalia tunabaki tukilumbana dhidi ya Ghadaffi na Bagbo.
 
Wanasema a picture worth 1000 words, nashukuru kwasababu nimeliongelea kwa hoja ya 'Je ile kauli mbinu ya matatizo ya Afrika yanahitaji suluhu ya Afrika' inayotumiwa na AU ina maana!

Tunalaani uvamizi wa nchi za magharibi kwa mapovu midomoni tukitetea Libya, Ivory coast n.k. vema! Je hili la njaa halihitaji AU.

Sisi ni wanafiki nasema bila kuuma maneno. Kwanini tulumbane kwenye mablog, magazeti ,warsha na semina kuhusu neo-colonialism wakati wakoloni hao hao sasa ndio wapo Somalia wakigawa chakula. Sisi tupo wapi kwenye matatizo kama haya.

Je ina maana watoto wanaokufa kwa vita ni bora kuliko wanokufa kwa njaa?
Je miaka 30 bado tunamsubiri Harry Belafonte na akina Lionel Rich waje kuimba ili kusaidia wenzetu.

Kuna 'moral authority gani kwa mawaziri wa mambo ya nje kama akina Mh Membe kukimbia huku na huko ili kumuokoa Gaddhafi ili hali watu wanakufa Somalia na wao wapo Dodoma.

Wale wanaowapa Alshaabab silaha wako wapi kuwapa chakula. Wale waliokuwa wanapigania Sudan kusini ijitenge wapo wapi kusaidia Somalia?

Kwanini hatulalamikii uvamizi wa mgharibi nchini Somalia tunabaki tukilumbana dhidi ya Ghadaffi na Bagbo.

Mkuu kama wiki tatu zilizopita nilikuwa naangalia historia ya utumwa marekani niliguswa sana na namna watumwa walivyokuwa mistreated mfano hawakuruhusiwa kufanya mikutano au kutembea usiku. Watumwa hata wale walionunua uhuru wao waliweza kukamatwa na kuuzwa tena. Kunyang'anya mali ya mtumwa au kuua mtumwa ilikuwa si dhambi wala kosa kisheria. This was in the 17th century, sasa cha ajabu in the 21st century watawala kama Mugabe they are doing the same to their country men just because they have different political beliefs. Weusi kwa weusi, watu wanapotea, wengine kuwa detained hata zaidi ya miezi sita bila kufunguliwa mashtaka, ZANU PF akimuumiza sometimes hata kumuua MDC hakuna kesi wala ufuatiliaji, this is done miaka hii ya 2000.

Kwa hiyo kama ulivyoongelea kwenye hoja yako sisi kweli ni wanafiki na tunakuwa driven na maslahi binafsi zaidi kuliko ya the entire human race?????
 
Kwa hiyo kama ulivyoongelea kwenye hoja yako sisi kweli ni wanafiki na tunakuwa driven na maslahi binafsi zaidi kuliko ya the entire human race?????
Mwanakijiji:Nauliza: Makanisa, na Misikiti yetu wako wapi kutekeleza wito wao wa kusimama na wale wenye njaa na shida?
Mwezi mtukufu wa Ramadhani unaanza katika siku mbili au tatu zijazo, nitafurahi nikiona zile tende zinazogawiwa na watu kwenye TV sasa zinafungashwa kupelekwa Somalia.
Nitafuahi nikisikia Jumamosi na Jumapili huko makanisani wanachanga pesa kuwasaidia Somalia.

Kama viongozi wa dini wanasimamia amani ya dunia, basi watueleze amani ni vita peke yake au zaidi ya hapo? Mzazi wa huyo mtoto ana amani gani hapo alipo na huyo mtoto ana amani gani tunayoambiwa tuwape wenzetu.

AU ina askari wa kulinda amani, amani ipi kwa familia hiyo hapo kwenye picha?
 
kwa kweli hali ni ya kutisha, na inabidi kuchukua hatua za haraka kuwaokoa wenzetu.
 
Mzee Mwanakijiji,

Hivi kweli unategemea sisi kujifunga mikanda tuende kumsaidia jirani aliye na njaa? Ikiwa kulisha watoto ndani na kuhakikisha wana afya bora na mahitaji ya lazima tunaona kana kwamba ni anasa, na ni mkao wa kula umbakishie Baba lile paja kubwa na matonge mengine, Baba ambaye hajui watoto wameamkaje, wamekula nini au wamevaa nini, leo ndio tuone kibanzi kwa jirani?

Ni aibu kuwa leo hii tunaambiwa na Serikali iko mbioni kutathmini athari za kukosekana umeme! Now wenzetu wanakufa njaa, tuko mguu pande tunatalii dunia mzima kubembeleza watu wachangie bakuli letu ilhali tunauwezo wa kujikimu wenyewe na hiyo misaada inapaswa kwenda Somalia na Djibuti na hata Kenya!

Ni uroho, ulafi, ubinafsi total selfishness! As huyu msukuma wako would say...MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO!
 
article-2019268-0D2BCEDF00000578-452_634x464.jpg
Desperate: Seven-month-old Mihag Gedi Farah weighs just 7lbs and was hours from death after arriving at a field hospital in Dadaab, Kenya
Hii ni AIBU KWA ALSHABAB waliotayari kutawala mafuvu ya vichwa.
Hii ni AIBU KWA MAJIRANI WA SOMALIA waliotayari kula na kumwaga huku wanafumbia macho hali hii.
Hii ni AIBU KWA TANZANIA kutokana na historia yake ya ukombozi wa Afrika.
Hii ni AIBU KWA VIONGOZI WA AFRIKA, bara lenye kila utajiri lakini watoto wa Waafrika wamefikia hali hii.
Hii ni AIBU KWA ULIMWENGU WOTE kwa sababu 1001.
HII NI AIBU YANGU MIMI NA WEWE.
Mwanakijiji, Maxence, Wana JF wote, ninashauri tupitishe bakuli ndani ya JF.
 
The question is what do we do?

MMJJ hongera sana kwa kutujuza juu ya hawa ndugu zetu, wangeweza kuikimbia hiyo njaa lakini watapita wapi ? Visa,PP,rushwa nk.ni vikwazo na vitu vya kuongeza machungu. hata wale ambao wanaweza toroka na kufanikiwa kufika hata mbeya ambako neno 'njaa' maana yake ni kukosekana kwa wali au ugali. AU wangekaa na kutafakari upya namna ya kuhakikisha nchi zenye ahueni ya chakula zifungue mipaka na kuondoa vikwazo ili watu waweze kusafiri au kusafirisha chakula,nafikiri umesikia serikali yetu ikipiga marufuku mahindi kusafirishwa kwenda nje ?????!!!!!!
 
Tuanze leo mkakati wa kuwafikia hao watoto,ni aibu na nidhambi kuona chakula kinazagaa jikoni kwangu,huku watoto wakifa kwa kukosa hicho ambacho wanangu wanaonja na kukiacha...Something must be done now,through JF we can do something for these innocent kids.
 
Kwenye masoko yetu ya chakula bado 'supply' ni kubwa kuliko 'demand' lakini bado watawala wetu kwa kuogopa vivuri vyao na ubinafsi wa kiafrika wako radhi kuona inzi wanafaidi vyakula vilivyooza kwa kukosa soko na kuwaumiza wafanyabiashara wetu kuliko vyakula hivyo kupelekwe kwenye mahitaji makubwa na ya kweli ya chakula kama somalia...Inahuzunisha sana
 
Mwezi mtukufu wa Ramadhani unaanza katika siku mbili au tatu zijazo, nitafurahi nikiona zile tende zinazogawiwa na watu kwenye TV sasa zinafungashwa kupelekwa Somalia.
Nitafuahi nikisikia Jumamosi na Jumapili huko makanisani wanachanga pesa kuwasaidia Somalia.

Kama viongozi wa dini wanasimamia amani ya dunia, basi watueleze amani ni vita peke yake au zaidi ya hapo? Mzazi wa huyo mtoto ana amani gani hapo alipo na huyo mtoto ana amani gani tunayoambiwa tuwape wenzetu.

AU ina askari wa kulinda amani, amani ipi kwa familia hiyo hapo kwenye picha?

Makanisa yapo bize kupanga na kutekeleza miradi ya kujiongezea kipato. KANISA LA SASA LIMEPOTEZA DIRA HALINA HATA MWELEKEO LILILOACHIWA NA BWANA WETU YESU KRISTO.Kanisa liko bize na miradi huku likisubiri kubatiza watoto na kuzika wafu,ndo injili pekee ambayo kanisa la sasa linaiweza.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom