Njaa inanukia, mvua zimegoma. Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi

Acheni njia primitive za kupambana na matatizo.

Kumzuia mkulima kuuza mazao yake mahali popote anapoona panampa manufaa eti kwa sababu kuna dalili ya njaa, ni njia primitive za kupambana na tatizo la njaa.

Kuna wakati kumewahi kuwa na upungufu mkubwa wa cement nchini, umewahi kusikia serikali ikipiga marufuku viwanda kuuza cement nje ya Tanzania? Kwa nini iwe tofauti kwa mkulima?

Kama Serikali itakuwa imeona kuna dalili ya uwepo wa njaa, ikanunue mazao toka kwa wakulima, ikashindane na wanunuzi wengine, ikayatunze mazao hayo kwenye maghali yake, na siyo vinginevyo.

Halafu, siyo kweli kuwa siyo kawaida kutokuwepo mvua kipindi hiki huko Nyanda za Juu. Labda umezaliwa miaka ya karibuni, na hivyo hujawa na uzoevu wa kutosha wa hali ya hewa ya maeneo ya huko.

Ni mara nyingi tu, maeneo ya Nyanda za Juu kukosa mvua kipindi hiki. Na ukizungumza na wakulima wa huko, hata miaka ya nyuma, utawasikia, 'mwaka huu mvua zimechelewa lakini Christmas lazima zitanyesha, na ikiwa hivyo kutakuwa na mazao mengi mwaka huu'.

Kwa uzoefu wangu, maeneo ya Nyanda za Juu, kukiwa na upungufu wa mvua, huwa wanapata mavuno mengi na mazuri zaidi. Tatizo la Nyanda za juu, mara nyingi ni mazao yao kama mahindi kuoza kutokana na mvua kunyesha kipindi kirefu, maharage kuungua kutokana na mvua kuzidi. Nyanda za juu, kwa wastani mahindi hukomaa ndani ya miezi 3. Hivyo mavuno mazuri ni ya mazao yanayopandwa mwezi Januari au mwishoni kabisa mwa December, ambayo hukomaa mwezi March, na hukauka mwezi April mpaka May. Hata kama mvua zikiwahi, ukipanda mwezi December, mazao hayo huharibiwa na mvua maana yataanza kukauka kipindi ambacho mvua bado zinanyesha.

Kama tutafika mwezi Januari 2022 bila ya mvua, hapo kweli Nyanda za juu wataanza kuwa na hofu ya kupata mavuno mazuri. Sasa hivi tatizo kubwa la mikoa hiyo ni bei ya mbolea, mfuko mmoja umefika shilingi 120,000. Huwezi kununua mbolea kwa bei hiyo, ukaitumie kwenye kilimo cha mahindi, upate faida. Sasa hivi nimeambiwa wakulima wameanza kutafuta mbegu zao za asili ili wasitumie mbolea, maana za kisasa haziwezi kumudu bila mbolea. Kitakachotokea ni mavuno kidogo
Mbaya zaidi hii mbinu yao ya kiprimitive badala ya kuondoa tatizo la njaa inaleta njaa.
 
Habari za mida..

Kuna dalili za njaa mwaka ujao kutokana na Hali ya ukame inayoendelea Nchini kwa sasa.

Sio jambo la kawaida kwa mwezi huu wa disemba mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutokuwa na mvua.Sehemu nilipo wananchi bado hawajaotesha Mazao kwa sababu mvua hazipo.

Hali ya hewa ni jua,joto,upepo na manyunyu tuu huku nzi wakitamalaki.

Chonde chonde Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi maana hivi tunavyoongea bei za Mazao zimeanza kupanda.Hata wale wa mahindi waliokuwa wanalia saizi wanauza kwa bei ya Kati ya 45,000-55,000 kwa gunia huku mikoani.

Ili kunusuru chakula kilichopo,nashauri serikali ipige marufuku exports ya Mazao yote ya chakula..

Kama Hali hii itaendelea ,Wananchi tujiandae kisaikolojia.Ukame umeeneo si tu Tanzania bali Hali ni mbaya zaidi Ethiopia,Kenya na Somalia.

Watu wa Hali ya hewa walitabiri hali hii toka mwezi wa tatu,wakarudia mwezi Juni na mwezi November.
mwachieni mbowe mvua zitanyesha za kutosha au endeleeni kumshikilia mpate ukame
 
Njaa?

Hebu nenda vijijini huko ndanindani, watu vyakula vimejaa hadi vinawashinda. Kiasi kwamba mgeni ukija na kurudi mjini wanakufungashia mizigo ya maana wapungukiwe kidogo tu. Na wana akiba ya kula mwaka mzima ila bado wanalima, tatizo hawafanyi biashara kama ilivyo wengine.

Balaa la mjini na gharama za maisha visikufanye uamini hivyo
Vitoto vya mjini hivi, vikikosa maji ya kuoga siku 2 tu vinalia dunia nzima
 
Kwa sisi wakulima kwetu ni sherehe, mvua ivute vute ianze January.

Unadhani hizo bei za mbolea tutaziweza mazao yasipopanda bei? Tumeshapata hasara sana....Mvua ikaze hivyo hivyo.
Na sisi Serikalini hatutakubali gunia livuke 65,000 ..

Kwanza hakuna mkulima humu ndani ni wafanyabiashara wamejaza magunia kwenye store wanajifanya wakulima.
 
Serikali inatakiwa iwezeshe miundombinu Wananchi wake waanze kutumia njia za umwagiliaji katika Kilimo maana ardhibyetu ina rutuba ya kuyosha tofauti na wenzetu wanaotuzunguka .

katika Soko huralia Serikali haitakiwi kuingilia mwisho wa Siku italeta matatizo ya kiuchumi ndani ya Nchi.
Hii nchi kila mtu anasubiria serikali, kweli kuongeza Tzn ni ngumu Sana
 
Habari za mida..

Kuna dalili za njaa mwaka ujao kutokana na Hali ya ukame inayoendelea Nchini kwa sasa.

Sio jambo la kawaida kwa mwezi huu wa disemba mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutokuwa na mvua.Sehemu nilipo wananchi bado hawajaotesha Mazao kwa sababu mvua hazipo.

Hali ya hewa ni jua,joto,upepo na manyunyu tuu huku nzi wakitamalaki.

Chonde chonde Serikali zuieni kuuza chakula nje ya Nchi maana hivi tunavyoongea bei za Mazao zimeanza kupanda.Hata wale wa mahindi waliokuwa wanalia saizi wanauza kwa bei ya Kati ya 45,000-55,000 kwa gunia huku mikoani.

Ili kunusuru chakula kilichopo,nashauri serikali ipige marufuku exports ya Mazao yote ya chakula..

Kama Hali hii itaendelea ,Wananchi tujiandae kisaikolojia.Ukame umeeneo si tu Tanzania bali Hali ni mbaya zaidi Ethiopia,Kenya na Somalia.

Watu wa Hali ya hewa walitabiri hali hii toka mwezi wa tatu,wakarudia mwezi Juni na mwezi November.
Jaribu kuingia kwenye kilimo japo kwa msimu mmoja tu afu utakuja ufute huu uhalo wako hujui ulisemalo kwani kuna mtu anapenda hasara?
 
Na sisi Serikalini hatutakubali gunia livuke 65,000 ..

Kwanza hakuna mkulima humu ndani ni wafanyabiashara wamejaza magunia kwenye store wanajifanya wakulima.
Mnaweza msikubali nyie na wanunuzi mitaani wakakubali.

Kwa hiyo wakulima hadhi yao ni ya chini kwamba hawawezi kumiliki smartphone au kwamba hawajui kama kuna kitu kinaitwa Jamii forum?

Mvua ikaze hivi hivi msiponunua serikali tutawauzia wafanyabiashara wa unga. Kwanza sisi hatutakagi kufanya biashara na serikali mahindi utoe leo pesa upewe mwaka umeisha.
 
Mnaweza msikubali nyie na wanunuzi mitaani wakakubali.

Kwa hiyo wakulima hadhi yao ni ya chini kwamba hawawezi kumiliki smartphone au kwamba hawajui kama kuna kitu kinaitwa Jamii forum?

Mvua ikaze hivi hivi msiponunua serikali tutawauzia wafanyabiashara wa unga. Kwanza sisi hatutakagi kufanya biashara na serikali mahindi utoe leo pesa upewe mwaka umeisha.

Achana na hao wahuni mkuu. Huu uhuni ndio umechangia mimi kuweka signature ya hivi.
 
  • Thanks
Reactions: Luv
Unataka wananchi mazao yao yawadodee si ndiyo.Wamelima kwa gharama kubwa nani atawarudishia gharama zao?
 
Back
Top Bottom