johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,598
- 141,415
Naikumbuka Chadema ile ya Dr Slaa iliyojaa watu makini akina Prof Kitila, Zitto Kabwe, David Kafulila, Anna Mghwira, JJ Mnyika, David Silinde nk ilikuwa ni chama cha upinzani kweli. Ilidaiwa kuwa kuna kipindi KUB Hamad Rashidi alilazimika kukabidhi " mabomu" mazito ya ufisadi kwa Dr Slaa ili ayalipue bungeni. Na kuna wakati ilimlazimu mwenezi wa CCM Nape Nnauye amlipie Dr Slaa ada ya uanachama kule CCM ili kumpunguza kasi. Na hata sasa tunaona mchango wa Slaa, Kitila na Anna kule serikalini bila kusahau mchango wa Zitto issue ya Buzwagi na Kafulila kule Escrow. Chadema ya Dr Slaa ilichukia ufisadi kama ambavyo Rais Magufuli na serikali ya awamu ya 5 wanavyouchukia ufisadi. Chadema ya leo imekuwa na kigugumizi kikuu kila wakati mafisadi wanaposhughulikiwa.......chadema hii imekumbwa na ugonjwa gani?