Ngigana
JF-Expert Member
- Apr 16, 2010
- 2,102
- 1,435
Inashangaza🙄Mimi nashindwa kuelewa sijui hua ni ibilisi gani anatua kwenye chama chetu? Niwaulize tena wanaCCM wenzangu,Spika Job Ndungai amekosea nini kiasi cha kumtolea maneno makali katika kila angle ya nchi?
Binafsi sijawahi kumpenda bayana Ndungai kutokana kejeli zake bungeni, sikuwahi kumpenda kwa sababu ya ubabe wake kwa wabunge wenzake hasa kubeba wabunge 19 wasiokua na vyama kinyume na katiba wanatafuna kodi za umma bure.Lakini kwa kauli zake za juzi juu ya Mikopo tunapaswa kushambulia hoja zake na siyo yeye binafsi. Ni wapi alikosea? Ni kweli alimlenga Mkuu wa nchi au alitoa angalizo tu?
Tunasahau kabisa kua bunge ni mhimili mwingine inayojitegemea, Spika alitoa maoni yake kama mhimili mwingine dhidi ya mhimili mwingine wenye mamlaka kukopa. Tulipaswa kuchukua hoja yake na kuifanyia kazi. Jamani, mtu anayekrwa na kukua kwa deni la taifa ni Mzalendo huyo tusimtukane. Sidhani kama Ndungai alimaamisha kua tusikope hapana, ilikua ni tahadhari tuu juu ya deni la taifa tusije tukapitiliza tukajikuta tunapigwa mnada.
Hii tabia tu ya kushambulia watu hasa viongozi wetu binafsi badala ya hoja zao si ustawi mzuri wa chama chetu. Ni hatari sana katika kutujengea uhasimu