Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,125
- 10,834
Mbali na kampeni za uchaguzi zinazoelekea ukingoni kutoa mielekeo ya nani anafaa zaidi kukabidhiwa uongozi wa nchi.Ufuatao ni uelewa wangu kuhusiana na wagombea watatu wa nafasi hizo.Hao ni Ibrahim Lipumba,Jakaya Kikwete na Wilbroad Slaa.
Mimi binafsi kwa nafasi hii namuamini zaidi Ibrahim Haruna Lipumba.Namuona ana elimu ya mambo ya kiuchumi ambalo ndilo tatizo sugu la watanzania.Ana uchangamfu wa kiuraisi na huzungumza kwa hekima.Wale wanaompinga si kutokana na kukosa sifa bali zaidi ni kutokana na chuki zao za kidini.
Pamoja na hivyo ikiwa umesalia muda mfupi kabla ya uchaguzi wenyewe,mpambano unaonekana upo zaidi kati ya Slaa na Kikwete.
Waislamu kwa kiwango kikubwa wanaonekana kumuunga mkono Kikwete,si kwamba wanamuona bora bali ili kumpinga Slaa ambaye wametoa takwimu nyingi kuonesha hisia zao dhidi yake.
Mbali na kuwa ana historia ya kupinga ajenda za waislamu bali anaonekana ni mtu muovu wa tabia hasa kutokana na kosa la kumnadi mke wa mtu kuwa ni mchumba wake.Wanahisi pindi akishika uraisi atakuwa ni mtu wa nuhsi moja baada ya nyengine.
Hisia hizo unaweza kuzipata wazi wazi kupitia redio kadhaa za kiislamu na magazeti yao hasa An-nuur na ALhuda.
Kutokana na kupigwa pande na kundi kubwa la wapiga kura na kampeni za kawaida za CCM, ni dhahiri kuwa dkt.Slaa hatoweza kupita katika uchaguzi huu hata.
Mimi binafsi kwa nafasi hii namuamini zaidi Ibrahim Haruna Lipumba.Namuona ana elimu ya mambo ya kiuchumi ambalo ndilo tatizo sugu la watanzania.Ana uchangamfu wa kiuraisi na huzungumza kwa hekima.Wale wanaompinga si kutokana na kukosa sifa bali zaidi ni kutokana na chuki zao za kidini.
Pamoja na hivyo ikiwa umesalia muda mfupi kabla ya uchaguzi wenyewe,mpambano unaonekana upo zaidi kati ya Slaa na Kikwete.
Waislamu kwa kiwango kikubwa wanaonekana kumuunga mkono Kikwete,si kwamba wanamuona bora bali ili kumpinga Slaa ambaye wametoa takwimu nyingi kuonesha hisia zao dhidi yake.
Mbali na kuwa ana historia ya kupinga ajenda za waislamu bali anaonekana ni mtu muovu wa tabia hasa kutokana na kosa la kumnadi mke wa mtu kuwa ni mchumba wake.Wanahisi pindi akishika uraisi atakuwa ni mtu wa nuhsi moja baada ya nyengine.
Hisia hizo unaweza kuzipata wazi wazi kupitia redio kadhaa za kiislamu na magazeti yao hasa An-nuur na ALhuda.
Kutokana na kupigwa pande na kundi kubwa la wapiga kura na kampeni za kawaida za CCM, ni dhahiri kuwa dkt.Slaa hatoweza kupita katika uchaguzi huu hata.