Niulize swali lolote kuhusu Pemba na Wapemba

Bussiness Man

JF-Expert Member
Mar 9, 2016
213
244
12938186_645289622284958_8673531003740101701_n.jpg 12938186_645289622284958_8673531003740101701_n.jpg
Nimeamua kuja hapa rasmi kuizungumzia hali ya Kisiwa cha Pemba kimazingira,
Uchumi,Afya,elimu, utamaduni na watu wake.
Nimezaliwa Pemba eneo moja la kaskazini mwa kisiwa hiki chenye urefu wa wastani wa kilomita 95, Ni kisiwa chenye amani iliyorithiwa na sio ya woga.
Watu wake ni wakarimu sana, lakini sio watu wanaopenda kuendeleza elimu kama msingi wa maisha yao. Hususani ni kipindi hicho ambacho tulikua tukisoma sisi sasa hivi ni tofauti kidogo zaidi kwa watoto wa kiume. Kwa upande wa watoto wa kike wazee hawaweki kipaumbele cha elimu.

Pemba imejigawa Miji mikuu 3, mizuri sana yenye huduma zote za jamii inayojitosheleza. Miji hii imejigawa na nikutoka kilomita 18 hadi mji mwingine. kwakua Miji hii imejigawa unaweza ukifika ukasema Pemba hakuna Maendeleo lakin Maendeleo yapo sababu kuu ya kutoyaona maendeleo hayo ni kila Mji na watu wake na Mambo yake 11796419_922716044436938_6507906242162783281_n.jpg . 12938300_522631377920308_2839808755009498085_n.jpg 1972276_584896188273706_445549572_n.jpg 11-underwater-room-Manta-Resort-Pemba-Island-Tanzania-yatzer.jpg Bahari ya Pemba ni Blue yenye beach nzuri sana, ikiwa ina navisiwa vidogo vidogo ndani yake.

Idadi ya Watu wa Pemba kwenye sensa ya mwaka 2012 ni 406,808 ingawa wengi kipindi kile hawakujiandikisha.
DSC01304.JPG DSC01332.JPG SAM_0885.JPG DSC01325.JPG DSC01327.JPG

Nimejifunza mengi sana katika maisha yangu ninayoishi pemba, kwakua nakielewa kisiwa hiki utandu na ukoko vizuri sana kuanzia ncha ya kusini mwa kisiwa mpaka kaskazini mwa kisiwa. Nimevutiwa kuweka bayana hapa kuhusu Hali yote ya pemba kwa sababu:

Nimepata changamoto nyingi niliposafiri sehemu tofauti watu wengi wana shauku ya kuijua Pemba na wapemba wakoje, wengi wanawaona wapemba kama hawasomeki au hawaeleweki, wengi wanawaona wapemba wana msimamo si watu wa kuyumba, wachawi ni watu wa kujituma.Wabaguzi hawapendi kujichanganya na wengine.

Nina majibu ya kutosha kuhusu hayo hapo kwa ufupi, ninapenda ukiwa na chochote ambacho umewahi kusikia kuhusu Pemba au kukukutokea niulize, nitajibu majibu yasiyopendelea upande wa kwetu au kujinasibu kwa majibu ya kejeli kwa wengine. nimeishi na watu tofauti nimesoma mazingira na tabia za watu wengi sana. 11800532_922716027770273_4734608859873431848_n.jpg 217971_331552500268288_1125401271_n.jpg
 
Eti naskia wapemba asili yao ni msumbijj. walikuja pemba kama watumwa.Baada ya biashara ya utumwa kukomeshwa ndio wakaanzia maisha hapo visiwa vya pemba.Na hawapendi kujichanganya na wabara. ni wabaguzi kama wahindi ni kweli?

Mkuu wapemba waliingia zaidi katika kisiwa cha pemba kuanzia karne ya 1300, hili la kusema wapemba na asili ya msumbiji halipo kwakua wale wamsumbiji walipoingia katika kisiwa hiki wao walijitenga sana, na wakawa wako katika sehemu ambayo waliishi na hawakujichanganya na waswahili hadi miaka inavokwenda baada ya kisiwa kujengwa watu hawa wachache waliobaki wakawa wanaishi na wapemba wengine.

Asili ya Wapemba ni mchanganyiko na wa mwanzo walianza kuingia Wagunya ambao ni kutoka Mombasa kwa upande wa Kaskazini Pemba.

Ubaguzi unaosemwa sio ni ubaguzi bali wapemba wanatabia ya Kumchunguza mtu kwa uaminifu wake, hili ndilo ambalo unaweza ukalitafsiri ni ubaguzi, hali hiyo inaweza ikakuchukua muda sana wa kuweza kufanya nae maisha ya pamoja Mpemba.
 
kwa sababu hawana matatizo ya nguvu za kiume
uvivu ndio unachangia sana watu kuzaa ovyo hususani mikoa ya pwani uzaliana sana na ndio mikoa inayoongoza kwa uvivu..naomba unijibu ili swali mtu mwenye upungufu wa nguvu za kiume ana uwezo kurutubisha yai?
 
Yakhe nasikia huko Pemba, Wapemba wakiwa katika mchezo wa Pool Table huwa hawasimami kama ilivyo kawaida ya mchezo wenyewe, na kama ikitokea kuna Mpemba kasimama basi anaweka ndoo kwa nyuma, kuna ukweli hapa? Lakini pia nasikia Wapemba ni washirikina sana, nadhani hili ndiyo la muhimu lenye kuhitaji majibu.
 
M
Yakhe nasikia huko Pemba, Wapemba wakiwa katika mchezo wa Pool Table huwa hawasimami kama ilivyo kawaida ya mchezo wenyewe, na kama ikitokea kuna Mpemba kasimama basi anaweka ndoo kwa nyuma, kuna ukweli hapa? Lakini pia nasikia Wapemba ni washirikina sana, nadhani hili ndiyo la muhimu lenye kuhitaji majibu.

Mkuu kuhusu suala la huo mchezo wa pool table sio kweli, na Ushirikina walionao wapemba sio wa kwenda kwa mganga wa ndunguli, wao kama ikitokea umefanyiwa ushirikina inawezekana hata yeye mwenyewe mpemba asijue kama kakufanyia, kwakua wengi wa wapemba wana majini ya asili vichwani mwao, ila hawa huwa hawana tatizo ila pale utakapomsumbua kichwa chake.
 
M


Mkuu kuhusu suala la huo mchezo wa pool table sio kweli, na Ushirikina walionao wapemba sio wa kwenda kwa mganga wa ndunguli, wao kama ikitokea umefanyiwa ushirikina inawezekana hata yeye mwenyewe mpemba asijue kama kakufanyia, kwakua wengi wa wapemba wanaongozwa na majini ya asli ya kwao.

Wanaongozwa na majini ya 'asli' au ulimaanisha ya asili? Hayo majini ya asli yanapatikana wapi?
 
Wanaongozwa na majini ya 'asli' au ulimaanisha ya asili? Hayo majini ya asli yanapatikana wapi?

Mkuu ni majini ya asili ambayo yamezunguka kisiwa cha Pemba chote, hawa ndio viumbe walioitawala Pemba kabla ya binadamu. Hawa majini wanapatikana Pemba miaka hiyo walipokuja waarabu ndio waliokua wanawatumilia kwa mambo yao ya biashara na maisha yao ya kila siku.
 
uvivu ndio unachangia sana watu kuzaa ovyo hususani mikoa ya pwani uzaliana sana na ndio mikoa inayoongoza kwa uvivu..naomba unijibu ili swali mtu mwenye upungufu wa nguvu za kiume ana uwezo kurutubisha yai?
Ingawa sio mpemba, ila swali limenigusa sababu umetaja mikoa ya pwani, tangu uzaliwe ni lini Pemba umesikia wanahitaji msaada eti wamezidi na njaa au shida yeyeto ya kimahitaji, pamoja kuwa na watoto wengi. Unataka kuniambia watu wa bara hawana nguvu ya kuzaa sababu kufanya kazi sana.
 
Back
Top Bottom