floow
JF-Expert Member
- Mar 20, 2017
- 411
- 852
Picha ya hapo juu ulikua ni Uzi wangu ambao niliuleta hapa hapa jamii forum mwaka 2017 mwezi wa 11 ,,kipindi ambacho nilikua nimechoka kufanya kazi niliyokuwa naifanya na nikawa naskia skia eti kupitia YOUTUBE unaweza kujiingizia pesa
Kwa bahati mbaya sikuweza kupata jibu lililo jitosheleza hapa jamii forum..ikanibidi niingie chaka la ma youtuber ili wanipe maujanja ya kuingiza hela ...
Nifupishe tuu kwa kusema nilihangaika sana kuhakikisha nakuwa mmoja wa watu wanaoingiza pesa kupitia youtube ..kwa Bahati nzuri jambo hilo limewezekana na kwa sasa YOUTUBE ndio maisha yangu..
Najua kuna vijana wengi wanatamani kujiingizia kipato kupitia YOUTUBE na hawajui wapi pa kuanzia ...haya sasa nakaribisha maswali