Niulize chochote kuhusu Subwoofer na Sounds system

kelphin

JF-Expert Member
Dec 24, 2019
8,844
13,987
Ikiwa inakusumbua,ikiwa unataka kufahamu chochote kinachokutatiza.

Karibu
images.jpg


Nieleze kidogo kuhusu subwoofer
Je, unataka kununua, basi zingatia haya.

Zipo za aina mbili old model na digital. Siyo majina hapana ,yaani inaweza kua rising,seapiano,codjec,aborder au vyovyote Ila itakua digital au old model.

Hizo digital ni Aina ya subwoofer ambayo inamuundo wakisasa ,mala nyingi utakuta Ina (nob) kivingilisho Cha sauti kimoja tu.

Ila kinafanya multipurpose, ukibonyeza hyo hiyo nob unaweza ongeza sauti ,kuongeza bass, na mid.
kifupi mambo yote ni in one button.

Faida yake ni kuwa, aina ya power supply yake Ni ilitaka ifanane na ya home theater(Ila haijawahi[emoji2inakua na umeme mnyoofu kidogo.

Zinakua na music mkubwa na mdundo zaidi ni digital,yaani yakisasa,
lakini pia display yake ni LCD haitumii umeme mwingi.

Je utaijuaje?
Nob ya kuongezea sauti ni moja tu na zaidi utakuta button za menu na input inategemeana). Ukiigeuza nyuma ina kiplastic kidogo kilichozungushwa nati, yaani ikiwa italeta shida fundi huku nyuma hafungui mfuniko wote wa nyuma, hufungua ki plastic tu hapo nyuma ndio kimebeba card zoote na subwoofer.

Hasara zake
  1. Ikitokea imeharibu card yake hauwez kubadilisha ,sababu ndani Ina circuit Kama ya phone mafundi weeengi hawana(hatuna) technology yakuitengeneza kwahyo unaenda dukani unanunua Tena kard na si chini ya 40000.
  2. Ila ukifika unaipachika tu huangaiki.
  3. Inahitaji utulie ili uioperate maana inatumia single nob.
  4. Speaker yake ya bass huwekwa ohms ndogo ili idunde sana kwahiyo usipende kuweka sauti kubwa Sana kwa muda mrefu.

Aina ya pili ndio zile old model
Hizo zinaitwa dunda udundavyo ni nzuri kwenye uzuri wake. Yenyewe ukiingalia utakuta Ina nob yaani vile vyakuongezea sauti zaidi ya kimoja. Yaani cha master volume, bass, tweeter na mic, na ukivizungusha vinafika mwisho.

Yenyewe ndani power supply yake ni ya kawaida, inatumia mtransformer wake na diodes za kawaida. kisha umeme huingia kwenye capacitor ndio unaanza kusambazwa ndani. Yaweza kuwa Seapiano, Codjec Aborder au vyovyote. Ukiigeuza nyuma mfuniko wote unafunguka wa nyuma.

Faida yake
  1. ikizingua unaiweza kuirekebisha kiurahisi tu
  2. Zinavumilia sana
  3. Hata muziki upo pia
  4. Rahisi kuitumia
Hasara zake
  1. Display yake ni VFD kama ni seapiano hapa mbele inakioo,inavyoimba Kuna vitu vinacheza cheza kwenye kioo(hii ni kwa baadhi ya subwoofer)
  2. Muonekano wake ni wakizamani ikilinganishwa na hizi mpya

Soma hi pia
Ndani ya subwoofer panya hupenda kuishi humo, huzaliana na kuleta hitilafu kwa kukata nyaya na kula speaker.
Waya wa speaker una chumvi chumvi hivyo akiingia hauachi.

Simple way jinsi ya kudhibiti
Pale kwenye tobo kuna ki corn cha duara huwa wanakipachika unaweza kukitoa kwa kufuata mpangilio ufuatao:

  1. Chukua maji ya moto kidogo na kitambaa, kichovye kitambaa kwenye maji kisha kikande kuzunguka mduara kwa dakika tano.
  2. Kisha chukua kisu, tumia ncha yake kuingiza pembezoni mwa mduara bila kuikwajua. Huku ukiinua kidogo kidogo kuzunguka corn nzima,ukisha kitoa kitoboe vitundu vidogo kukizunguka upande wa ndani(sio Huku uliko Kanda kwa maji).
  3. Ukisha kitoa chukua waya mgumu usuke upande wa ndani kuzunguka uwazi wa duara wote mule ulimotoboa, kisuke hakikisha unaacha vyumba vidogovidogo kiasi kwamba kinaweza kupita kidore kidogo tu.
  4. Paka gundi upande wa ndani, huku ulikokua unakanda na maji kisha kibandike tena kama kilivyokuwa.

NB: Hii ni kwazile subwoofer kama pichani hapo juu, ambazo hutolea upepo pembeni kwenye kiduara. Wale zinazotolea mbele chini ni habari nyingine.

***
Kiasi chake mtanielewaView attachment 1560194View attachment 1560195

Some updates,
Je, music system yako haina bluetooth na unataka kuongezea? Easy sana na inawezekana pia, kwa mafundi ninaweza kuwaelekeza.

Lakini pia music system yako ulipenda itoe mp5, yaani picture, video inawezekana pia.
Hususani wale wenye TV za kizamani yaani unachomeka flash disk yako kwenye subwoofer, unapata mdundo alafu kuna cable itatoka kwenye subwoofer hadi kwenye TV yako.

Stay here.
More good things are here.
Welcome.

View attachment 1921368
View attachment 1921369
 
Yah sea piano zinakata miaka kwa kweli hesabu toka 2014-2021 na still ipo haijawahi kukanyaga kwa fundi

Mtaani kuna seapiano old model ya 2013 no Bluetooth na control zake ni analog ...inakita sana ina sauti nzuri in a way maza hawezi toa pesa nyingi kwa ajil ya mziki mwngne wakat ile inatosha pale ...hadi kuna mtu ana hometheatre ya 1000w ila alishangaa ule mkito hakuamin maana yake haifiki pale na katoa pesa ndefu
 
Mkubwa Habari. Nipo na new model Seapiano ila kwa Sasa inapiga only 1 speaker Tena ndogo. Ile kubwa ya bass haipigi inawasha display tu. Je, niitibuje au ndo keshakuwa mlemavu? Currently haina bass wala stereo!
 
Mtaani kuna seapiano old model ya 2013 no Bluetooth na control zake ni analog ...inakita sana ina sauti nzuri in a way maza hawezi toa pesa nyingi kwa ajil ya mziki mwngne wakat ile inatosha pale ...hadi kuna mtu ana hometheatre ya 1000w ila alishangaa ule mkito hakuamin maana yake haifiki pale na katoa pesa ndefu

Zile zilikua nzuri sana
Mchina kazitoa makusudi kabisa
 
Mkubwa Habari. Nipo na new model Seapiano ila kwa Sasa inapiga only 1 speaker Tena ndogo. Ile kubwa ya bass haipigi inawasha display tu. Je, niitibuje au ndo keshakuwa mlemavu? Currently haina bass wala stereo!

Pole sana mkuu
Matatizo yanaweza kua kama ma2 hapo
Kama sio speaker inamatatizo basi huenda ic inayoendesha hyo speak inashida

Ifungue huenda panya amekula waya za speaker hizo kwa ndani zinazoenda kwenye connector
Kisha utaniambia
Au fungua upige picha
 
Kusema ukweri sifahamu juu ya hilo
Ila hiyo BT mala nyingi huashilia kua system inakuja na Bluetooth option
Karedio kangu haka kanashika station tatu tu yan kanashshka redio free,clouds&TBC. Lakn mm nilinunua ili nisikilize Wasafi,Efm &Radio one. Je kuna namna naweza fanya ili haka karedio kaweze kushika station nyng zaid?

mwanzo nlidhan labda eneo nlilopo ndo tatzo lakn nikaondoka nako na kwenda sehem nyngne lakn bado ikashndwa kushka station nyngne!
View attachment 1747246
 
49 Reactions
Reply
Back
Top Bottom