Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Kichuguu nina ist ya wife ukiwasha AC baada ya muda mrefu na kwenye speed ndogo mfano foleni huwa gari inajizima, ukiiwasha inawaka kawaida tuu. Tatizo ili kama hujawasha AC huwa halitokei na hata kama ukiwasha ukiwa kwenye speed huwezi ona ili tatizo
 
Kichuguu nina ist ya wife ukiwasha AC baada ya muda mrefu na kwenye speed ndogo mfano foleni huwa gari inajizima, ukiiwasha inawaka kawaida tuu. Tatizo ili kama hujawasha AC huwa halitokei na hata kama ukiwasha ukiwa kwenye speed huwezi ona ili tatizo
Nilishawahi kujibu swali kama hilo hapa
 
Gearbox automatic ina oil yake maalum initwa ATF (Automatic Transmission fluid), na kuna aina nyingi sana za mafuta hayo. Kila gari ina aina yake. Ukiweka namba 90 utaua gearbox yote. Namba 90 ni kwa gearbox za stick shift na diff; usiiweke kwenye automatic transmission
Vipi oil namba 50 kwa gari ndogo (Rav4 kilitime)
 
Mkuu habari na hongera kwa kazi nzuri.

Nina shida na engine ya IZZ. Muungurumo wake umekuwa juu na pia kunakuwa na mlio wa kkkkkkk.

Fuel consuption imeongezeka tofauti na kawaida. Nimebadili plug lakini shida haijaisha bado.

Pia kunakuwa na vibration sana.
Ni mambo gani natakiwa kufanya na tatizo linaweza kuwa ni nini?
 
Mkuu habari na hongera kwa kazi nzuri.

Nina shida na engine ya IZZ. Muungurumo wake umekuwa juu na pia kunakuwa na mlio wa kkkkkkk.

Fuel consuption imeongezeka tofauti na kawaida. Nimebadili plug lakini shida haijaisha bado.

Pia kunakuwa na vibration sana.
Ni mambo gani natakiwa kufanya na tatizo linaweza kuwa ni nini?

Inawezekana tatizo lako ni dogo sana; je umeshabadili air filter au air cleaner? Baada ya hapo ndipo yanapofuata matatizo mengine madogomdogo pia kama vile air flow sensor kuwa chafu au baadhi ya injector kuwa zimeanza kuziba. Kuna mafuta ya kuzibulia injector, na vile vile kusaifishia air flow sensor, lakini tatizo lako kubwa linaweza kuwa ni air filter tu.
 
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler. Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through parttime activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu. Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto repair shop. Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
Mpwaa HONGERA sanaa sana aise
 
Soma kwanza kitabu cha gari yako, kuna injini nyingi zinataka 5W-30 na 5W-20. Hata hivyo kwa Dar es Salaam ambayo ni sehemu yenye joto sana, unaweza kutumia 10W-30 au 10W-20.
Na pia, matumizi ya oil yanategemea sana matumizi ya gari lenyewe. Maana low viscocity oils zinataka kubadilishwa baada ya kilometa chache zaidi ya high viscocity oils. Kwa hivyo ni chaguo la mtumiaji zaidi ingawa watengeneza magari wenyewe wana mapendekezo yao.
 
Inawezekana tatizo lako ni dogo sana; je umeshabadili air filter au air cleaner? Baada ya hapo ndipo yanapofuata matatizo mengine madogomdogo pia kama vile air flow sensor kuwa chafu au baadhi ya injector kuwa zimeanza kuziba. Kuna mafuta ya kuzibulia injector, na vile vile kusaifishia air flow sensor, lakini tatizo lako kubwa linaweza kuwa ni air filter tu.

Inawezekana tatizo lako ni dogo sana; je umeshabadili air filter au air cleaner? Baada ya hapo ndipo yanapofuata matatizo mengine madogomdogo pia kama vile air flow sensor kuwa chafu au baadhi ya injector kuwa zimeanza kuziba. Kuna mafuta ya kuzibulia injector, na vile vile kusaifishia air flow sensor, lakini tatizo lako kubwa linaweza kuwa ni air filter tu.

Ninakushukru sana mkuu kwa maelekezo mrua.
Nilishabadili air cleaner tu.
Kuna fundi nilimshirikisha akanambia huenda ikawa ni fuel pump, nozzle, mounting na oxygen sensor.

Na gari ina km 200.000 kwa sasa, unashauri nibadilishe kitu gani ili liendelee kubaki kwenye hali yake?

Pia naomba kujua ni mafuta gani ya kuzibulia injector na wapi naweza yapata? Na kuna wakati ac inachelewa kufanya kazi hasa ninapokuwa nimepaki kwenye jua kwa muda mrefu.

Ngoja nifanyie kazi ushauri ulonipa kisha nilete mrejesho.
 
Hongera!

Ingiwa nimechelewa kusoma thread mapema.

Nitarudi nikikwama na hawa watu wetu wa mitaani!

Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler. Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through parttime activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu. Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto repair shop. Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
 
Ninakushukru sana mkuu kwa maelekezo mrua.
Nilishabadili air cleaner tu.
Kuna fundi nilimshirikisha akanambia huenda ikawa ni fuel pump, nozzle, mounting na oxygen sensor.

Na gari ina km 200.000 kwa sasa, unashauri nibadilishe kitu gani ili liendelee kubaki kwenye hali yake?

Pia naomba kujua ni mafuta gani ya kuzibulia injector na wapi naweza yapata? Na kuna wakati ac inachelewa kufanya kazi hasa ninapokuwa nimepaki kwenye jua kwa muda mrefu.

Ngoja nifanyie kazi ushauri ulonipa kisha nilete mrejesho.
Hii air cleaner uliyoweka ni original? Swali linaanzia hapo? Maana watumiaji wa magari wengi hawapendi vitu original na ambavyo vitasaidia kumaliza tatizo la gari badala yake wanaweka vitu kwa kupenda urahisi
 
Iwapo ukishaliwashalikisha likapata joto hutulia kabisa mpka akesho yake basi ina maana kuwa senor moja iitwayo Mass Air Flow (MAF) sensor ni chafu sana; kuna mafuta maalumu ya kuisafishia. MAF ikiwa chafu inasabababisha injini kupata hewa nyingi sana kuliko mafuta wakati wa kustart, hivyo inashindwa kuchoma mafuta mpaka ipate joto la kutosha.

Labda nikueleze kidogo kwa nini matatizo ya namna hiyo hutokea. Injini ikiwa ya baridi huwa inataka mafuta mengi kuliko kawaida hadi ikishapata joto la kutosha. Kwa hiyo Computer husoma hiyo MAF na pamoja na sensor ya kupima joto la injini kuamua kiasi cha mafuta ya kupeleka kwenye injini. Sasa kama MAF haipeleki ujumbe mzuri kwenye computer ndipo unapokuta computer inaruhusu mafuta machache kuliko yanayotakiwa.

MAF huchafuka iwapo unatumia air cleaner ambayo ni chafu sana.

Kama kusafisha MAF hakusaidii kuoandoa tatizo basi huenda injector na valve zina masizi mengi; weka chupa moja ya mafuta ya kusafishia injector kwenye full tank ya mafuta, baada ya muda kama siku tatu hivi tatizo litatoweka lenyewe. Hata hivyo sababu kubwa ni hiyo ya MAF hapo juu.
Nishawahi kukatazwa na dealer wa Toyota kutumia injector cleaner,yeye alisema once ukianza basi inatakiwa utumie kila unapojaza mafuta hasa kwa kuwa filling station nyingi kwa bongo zinauza mafuta machafu (ambapo sikumuelewa kwa kweli)
1. Je, kuna ukweli katika hilo?
2. Nikiweka mafuta kwenye vituo vya kawaida gari haina mis,lakini nikiweka kwenye vituo vya TOTAL then nikarudi kwa vingine mis hutokea na sometimes gari kuzima na kusumbua kuwaka,Je,ni formula ya mafuta kutofautiana au kuna sensor kwenye gari haipo sawa?.
Shukrani.
 
NOAH 1AZ ya mwaka 2002, 280,000 km naenda nayo karibu mikoa yote kwa kazi zangu,je recommendations oil ni ipi kati ya 5W-30 na 20W-50?
Niliwahi kutumia SAE 40...gari lilikuwa likiwashwa asubuhi, silence inakuwa juu sana na kwa muda mrefu...ilikuwa inakaa kwenye RPM 3 kwa muda zaidi ya dakika 3 au 4ndiyo inashuka pole pole...wakati huo mlio ulikuwa si ule wa kawaida.....ikawa mpka niendeshe umbali fulani injini ipate moto wa kutosha ndiyo mambo yanakaa sawa....hivyo nashauri watu tuzoee 5w 30 utalifurahia gari lako..
Hizo SAE 4 hebu tuwaachei watu wa Canter, Hilux zile za zamani, DCM, Daladala Coaster zilizochoka n.k
 
Nina ist naendesha nikiwa na mizunguko mingi. Inatokea inashiwa nguvu na kuzima. ukiwasha Tena inapiga mwendo Kama kawaida. Limetokea mara ya tatu leo. Mara ya kwanza mwezi wa 8 na mara mbili mwezi huu. Tatizo yaweza kuwa Nini?
 
Hii air cleaner uliyoweka ni original? Swali linaanzia hapo? Maana watumiaji wa magari wengi hawapendi vitu original na ambavyo vitasaidia kumaliza tatizo la gari badala yake wanaweka vitu kwa kupenda urahisi
ni Original mkuu
 
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler. Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through parttime activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu. Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto repair shop. Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
gari yangu nikiendesha kwa muda taa ya check engine inawaka nikitoa terminal na kurudishia gari inawaka na taa inazima. ni tatizo gani?
 
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler. Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through parttime activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu. Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto repair shop. Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.
Niambie kuhusiana na engine ya Premio 7A 1760 CC
 
57 Reactions
Reply
Back
Top Bottom