Niulize chochote kuhusu injini za magari madogo na pickup zinazotumia Petroli

Nimejaribu leo kuingia chini ya gari ili kusikiliza ule mlio unaogonga unatokea wapi,nimegundua unatokea ndani ya oil sump.Niliwahi pia kumuuliza fundi mmoja akaniambia inawezekana chekeche la oil sump lina mauchafu kwahiyo oil inapita kwa shida wakati wa kuwasha gari kwahiyo ikipata moto inalainika na ule mlio ndio maana huwa unaacha,ushauri alionipa nikufungua na kuisafisha,hapo napo ni vipi mkuu?pia ulinishauri niangalie lile bati la juu ya exhause pipe kama limelegea,lile liko tight kabisa na nut zote ziko vizuri...

kwanza kabla sijakupa utaalamu wa muhimu zaidi, hebu niambie kwanza iwapo gari lako linatumia automatic transmission au ni stick shift transmission.

kama ni Automatic Transmission, litakuwa na oili sump mbili; moja kwa ajili ya injini, na nyingine kwa ajili ya gearbox, je unasikia sauti hizo kutoka sump ipi? Nina wasiwasi kuwa itakuwa inatoka kwenye sump ya gearbox; na hilo litakuwa siyo jambo jema kabisa.
 
mkuu kwema nina honda accord 2000 uk version nimefanya service nimebadil sensor zote nilizoambiwa nibadili baada ya kuchekiwa kwenye computer , gari bado inawasha check engine nikiwauliza tatizo wananiambia oil nilioweka nikiweka castrol oil inayokaa kwenye kidumu cheupe mtakutimia no za iyo oil mara wanambie coz coolant fan sensor imeungea direct ndo maana inawasha taa je jinu lipi ni sahihi mkuu Kichuguu
Kichuguu amekujibu vizuri..niongeze kidogo..
Angalia pia Catalytic converter kama ipo...kuna baadhi ya mafundi ukiwaachia gari wanaiba yale masega na kuyauza bei ghali...

Baadhi ya magari yana Oxygen sensor 2, moja huwa kabla ya cat na nyingine huwa baada ya cat....endapo yale masega yameondolewa, basi ile sensor ya pili hushindwa kusoma kiwango cha oxygen ambacho hakijaunguzwa kwenye combustion chamber....kwa nini inashindwa kusoma..? kwa sababu hamna cat hivyo gesi zinapita pale kwa kasi zaidi kuliko kiwango kilichokuwepo mwanzo...Hivyo Oxygen sensor hupeleka taarifa kwwnye ECU kuwa kuna shida katika mfumo wa exhaust...ndiyo unapata check engine light...
Japo kuna magari unaweza ukaondoa Cat converter na check engine light isiwake....mfano gari nililonalo..

Kama hawajaiba hayo masega, fuata ushauri wa kichuguu...lakini zingatia zaidi Oxygen sensor na MAF sensor...

Usisahau, kuna magari hayataki shida..hata Air filter ikiwa chafu sana yanaonyesha check engine light.
 
mkuu kwema nina honda accord 2000 uk version nimefanya service nimebadil sensor zote nilizoambiwa nibadili baada ya kuchekiwa kwenye computer , gari bado inawasha check engine nikiwauliza tatizo wananiambia oil nilioweka nikiweka castrol oil inayokaa kwenye kidumu cheupe mtakutimia no za iyo oil mara wanambie coz coolant fan sensor imeungea direct ndo maana inawasha taa je jinu lipi ni sahihi mkuu Kichuguu

Kichuguu amekujibu vizuri..niongeze kidogo..
Angalia pia Catalytic converter kama ipo...kuna baadhi ya mafundi ukiwaachia gari wanaiba yale masega na kuyauza bei ghali...

Baadhi ya magari yana Oxygen sensor 2, moja huwa kabla ya cat na nyingine huwa baada ya cat....endapo yale masega yameondolewa, basi ile sensor ya pili hushindwa kusoma kiwango cha oxygen ambacho hakijaunguzwa kwenye combustion chamber....kwa nini inashindwa kusoma..? kwa sababu hamna cat hivyo gesi zinapita pale kwa kasi zaidi kuliko kiwango kilichokuwepo mwanzo...Hivyo Oxygen sensor hupeleka taarifa kwwnye ECU kuwa kuna shida katika mfumo wa exhaust...ndiyo unapata check engine light...
Japo kuna magari unaweza ukaondoa Cat converter na check engine light isiwake....mfano gari nililonalo..

Kama hawajaiba hayo masega, fuata ushauri wa kichuguu...lakini zingatia zaidi Oxygen sensor na MAF sensor...

Usisahau, kuna magari hayataki shida..hata Air filter ikiwa chafu sana yanaonyesha check engine light.

Kwa gari la mwaka 2000 kama kweli Emmanuel S Jonathan amebadilisha sensors zote, nina uhakika kwa 95% kuwa tatizo lake ni Catalytic Converter. Njia moja ambayo siyo professional lakini unaweza kuzima catalytic converter light forever ni ile ya kuunganisha downstream oxygen sensor mpya kwenye kipande kinachoitwa catalytic converter fouler. States nyingi Marekani haziruhusu matumizi yake lakini watu wanaziuza ebay na Amazon kama kawaida. Nina imani kuwa kitu hiki kwa Tanzania kinaruhusiwa tu, lakini sisi haturuhisiwi kuviweka kwenye magari ya wateja. Kukitumia, inabidi ukiweke sehemu ya Oxygen sensor kwenye cat conv yako, halafu unaingiza oxygen sensor ndani yake. Kwa hiyo Oxygen sensor itakuwa haisomi Oxygen level halisi ya kwenye exhaust bali level iliyoko kwenye fouler hiyo, ambayo ni nzuri. Computer (ECU) ya injini inakuwa inadanganywa kuwa mambo yote ni fit wakati siyo kweli, na hivyo taa haiwaki kabisa.

Mtu akivichangamkia Tanzania anaweza kulamba hela nzuri tu.

1567325841045.png
 
Mkuu
Iwapo mtu akiweka engine oil ya kupima ambayo haina ubora, je inaweza kusababisha engine kugonga pale unaiwasha gari na baadae kutulia?
 
Mkuu
Iwapo mtu akiweka engine oil ya kupima ambayo haina ubora, je inaweza kusababisha engine kugonga pale unaiwasha gari na baadae kutulia?

Samahani, swali lako sikulielewa; unaweza kufafanua zaidi? Hasa maneno "oil ya kupima" "haina ubora" na "engine kugonga" hayaeleweki vizuri.
 
Samahani, swali lako sikulielewa; unaweza kufafanua zaidi? Hasa maneno "oil ya kupima" "haina ubora" na "engine kugonga" hayaeleweki vizuri.
Kuna oil wanauza kwa kupima kama mafuta ya kupikia yaani ukitaka nusu lita, lita n.k na wengi husema ile haina ubora.
Engine kugonga ni kusikia milio ya ajabu ajabu kama mtu anafunda ila baada ya dk 2 mbili tatu inatulia safi kabisa....tatizo hili lilianza baada ya kuiongezea oil ya kupima ilihali iliyomo ni Total ilipungua kidogo
 
Kuna oil wanauza kwa kupima kama mafuta ya kupikia yaani ukitaka nusu lita, lita n.k na wengi husema ile haina ubora.
Engine kugonga ni kusikia milio ya ajabu ajabu kama mtu anafunda ila baada ya dk 2 mbili tatu inatulia safi kabisa....tatizo hili lilianza baada ya kuiongezea oil ya kupima ilihali iliyomo ni Total ilipungua kidogo
Ngoja niamini kuwa gari yako inatumia EFI; kwa hiyo inaonekana kama vile oil yako haiwezi kusukuma tappets kufunguka inavyotakiwa, kwa hiyo unaanza wakati injini ina misfire. Misfire ya namna hiyo inasababishwa kwa asilimia 90 na oil mbovu; asilimia zile 10 ni oil pump. Makosa ambayo watu wanafanya kuhusu engine oil ni kule kuongezea badala ya kumwaga ile ya zamani yote, kuondoa oil filter na kuweka oil mpya pamoja na oil filter mpya. Ukiwa na oil chafu, halafu ukaongezea oil mpya bado unabaki na oili chafu inayotaka kusukumwa kama mara mbil au tatu kabla haijafungua tappets. Kwa muda mrefu ni kuwa utakuwa pamoja na mambo mengine unaua piston rings, ambazo zinaaweza baadaye kuja kukucost engoine orverhaul.
 
Engine ni 4E
Shukran sana mkuu
Ngoja niamini kuwa gari yako inatumia EFI; kwa hiyo inaonekana kama vile oil yako haiwezi kusukuma tappets kufunguka inavyotakiwa, kwa hiyo unaanza wakati injini ina misfire. Misfire ya namna hiyo inasababishwa kwa asilimia 90 na oil mbovu; asilimia zile 10 ni oil pump. Makosa ambayo watu wanafanya kuhusu engine oil ni kule kuongezea badala ya kumwaga ile ya zamani yote, kuondoa oil filter na kuweka oil mpya pamoja na oil filter mpya. Ukiwa na oil chafu, halafu ukaongezea oil mpya bado unabaki na oili chafu inayotaka kusukumwa kama mara mbil au tatu kabla haijafungua tappets. Kwa muda mrefu ni kuwa utakuwa pamoja na mambo mengine unaua piston rings, ambazo zinaaweza baadaye kuja kukucost engoine orverhaul.
 
kwanza kabla sijakupa utaalamu wa muhimu zaidi, hebu niambie kwanza iwapo gari lako linatumia automatic transmission au ni stick shift transmission.

kama ni Automatic Transmission, litakuwa na oili sump mbili; moja kwa ajili ya injini, na nyingine kwa ajili ya gearbox, je unasikia sauti hizo kutoka sump ipi? Nina wasiwasi kuwa itakuwa inatoka kwenye sump ya gearbox; na hilo litakuwa siyo jambo jema kabisa.
Gari ni Prado,automatic,mlio unatokea kwenye sump ya engine mkuu(mlio ni ta ta ta ta ta) halafu unakata,na kama ni kwenye sump ya gearbox shida itakuwa ni nini...?
 
mkuu nna maswali 3,je timming belt inatakiwa kubadilishwa baada ya km ngap? kwa hizi mark ii. pili je nisahihi kutumia N gear wakati wa kushuka mlima?? 3.je nikiwa ktk foleni niweke N,P au nikanyage brake gari ikiwa kwenye D gear.ahsante
Usishangae kuhusu utambulisho huu. Mimi sasa ni ASE Certified Service Consultant wa magari madogo yanayotumia petroli hasa ya Ford, GM, na Chrysler. Nimepata license yangu hivi majuzi tu mwaka huu baada ya kuitafuta kwa muda kidogo through parttime activities kwani hiyo siyo kazi yangu kuu. Certification hiyo inahitaji siyo tu kufaulu mtihani wake lakini pia uwe na uzoefu wa kutosha kwenye auto repair shop. Nimekamilisha experience hiyo inayotakiwa mwaka huu na kupata license yangu.

Kwa vile injini nyingi za petroli zinafanana katika utendaji, jisikie free kuniuliza swali lolote kuhusu matatizo ya injini ya gari yako model yoyote inayotumia mafuta ya petroli.

Siahidi kuwa majibu yangu yote yatakuwa ni sahihi, lakini sehemu kubwa itakuwa ni sahihi, na hata yale ambayo hayatakuwa sahihi yanaweza kukusadia kujua wapi pa kuanzia.

NYONGEZA: Kwa vile ninashiriki kwenye majukwaa mengine ya JF, na vile vile nafungua JF randomly, ukiniuliza swali jitahidi uwe unanitag kusudi niweze kuliona swali hilo mapema. Maswali yanayohusu injini za petroli nitayajibu haraka sana kuliko mada nyingine yoyote ya JF.
 
mkuu nna maswali 3,je timming belt inatakiwa kubadilishwa baada ya km ngap? kwa hizi mark ii. pili je nisahihi kutumia N gear wakati wa kushuka mlima?? 3.je nikiwa ktk foleni niweke N,P au nikanyage brake gari ikiwa kwenye D gear.ahsante
(a) Timing Belt inatakiwa kubadilishwa kila baada ya km 100,000.

(b) Unaweza kuweka gari kwenye N wakati wa mtelemko, lakini huo siyo uendeshaji mzuri wa gari. Kwanza ukiweka kwenye N, unasababisha injini inyonye mafuta mengi zaidi ya kuliko inapokuwa kwenye D lakini ikitelemka mlima. Halafu wakati mwingine kukitokea hatari inayokutaka uongeze spidi ghafla hutaweza kuikwepa. Mamlaka nyingi za usalama barabarani huzuia matumizi ya N kwenye mitelemko.

(c) Transmission nyingi zina alama ya PRNDL, nyingine zina PRNDSL, na nyingine zina PRND321 na kadhalika. Driving ya kawaida ni kwenye position ya D na ukitaka kusimama unakanyaga breki tu, gari itasimama. Hata hivyo ukiwa kwenye barabara ya foleni tumia position ya L au namba moja wapo ya 1,2,3 kwa ajili ya mwendo wa kusimamasimama. Unaposimama wewe kanyaga breki tu; breki ile pia hu-act kama clucth ya kutenganisha injini na gearbox; huna haja ya kuhamishia kwenye N. Ukishaingia kwenye freeway ndipo unaihamishia kwenye D. Usijaribu kuweka kwenye alama ya P wakati uko barabarani, kuna sababu kadhaa za kiuslama hasa kwa vile kufanya hivyo unapitia kwenye gear ya R pia.
 
Gari ni Prado,automatic,mlio unatokea kwenye sump ya engine mkuu(mlio ni ta ta ta ta ta) halafu unakata,na kama ni kwenye sump ya gearbox shida itakuwa ni nini...?

Kama mlio unatoka kwenye sump kuu ya engine basi wakati wa kufanya service ijayo, angalia kichujio cha oil pump kama kitakuwa kimeziba. ndani ya oil sump huwa kuna sumaku inakamata vipande vinavyotokana na chuma kusagika visizibe oil pump, lakini kuna vinavyoweza kukwepa na kuziba chujio hilo.

Hata hivyo tatizo ambalo huonekana mara nyingi sana kwenye magari yenye automatic transmission ni kuwa kwa vile hazina flywheel, badala yake zina flexplate ambayo ina meno yanayoingiliana na stater motor wakati wa kustart engine. Plate (ni jina tu lakini siyo plate bali ni gear) hii ndiyo huunganisha injini na gearbox. Magari mengi hasa haya ya kimarekani ninayojua hupata hiyo kadhia ya flexplate kulegea au kupasuka, na hivyo kuanza kutoa kelele hizo wakati injini inapostart kwa vile starter motor inakuwa imeisukumia upande mmoja, starter motor ikishaiachia basi mzunguko wake unairudisha kwenye balance tena, na kelele zinakwisha; mlio huo husikika kama unatoka kwenye oil sump lakini unatoka kwenye hiyo flexplate iliyolegea au ina mpasuko. Kama ni hiyo, basi unaweza kuwa na matatizo mengine zaidi yanayosababisha flexplate iharibike. Baada ya muda kelele hizo zitaoiongezeka na kuwa zinasikika muda wote injini inapokuwa inaunguruma, siyo mwanzo tu.
 
Mkuu kwa gar hiz za toyoyota hali hyo mara nying hutokea ring piston zikiwa zimechoka, nasema hv kwa kuwa hata mm kuna siku nifanya hvyo nikaona oil inatoka kama mvuke hv nikashangaa...ikabidi niangalie gari nyingine yenye injin kma yangu na ni mpya zaid ya yakwangu, kiukweli gar ikiwa vizur ukichomoa dip stick haifanyi hvyo, kama huamini tafuta gari ambayo haitoi moshi halafu chomoa dip stk utaona, mm nilifatilia ya kwangu kweli nilibain kuwa inatoa moshi japo sio mwingi sana, nilivyobadili injin hata nikichomoa dip stk ile hali siioni tena, ebujaribu kufanja tafit kwenye injin nyingine mkuu ili ujiridhishe zaid.
Shukran sana mkuu maana uswahilini mafundi waliniambia nibadilishe piston ring eti haitakiwi oil iruke gari ikiwashwa.
Hata hivyo chombo ipo safi haina hitilafu yeyote.
 
20W-50 ni kwa ajili ya ajili ya magari makubwa na makuukuu kweli kweli; kama una gari lenye hali nzuri, oli nzuri ni 5W-20 mpaka 10W-30 ukihusisha grade zote za katikati, yaani 5W-30, na 10W-20. Kadri gari linavyochakaa na wakati wa joto sana ndipo unapandisha namba kidogo kidogo mpaka 10W-30 usizidi hapo kwa gari yoyote ndogo labda kwa basi na roli la mizigo.
Na oil za SAE40 kwa gari ndogo zina madhara gani?
 
Mkuu kwa gar hiz za toyoyota hali hyo mara nying hutokea ring piston zikiwa zimechoka, nasema hv kwa kuwa hata mm kuna siku nifanya hvyo nikaona oil inatoka kama mvuke hv nikashangaa...ikabidi niangalie gari nyingine yenye injin kma yangu na ni mpya zaid ya yakwangu, kiukweli gar ikiwa vizur ukichomoa dip stick haifanyi hvyo, kama huamini tafuta gari ambayo haitoi moshi halafu chomoa dip stk utaona, mm nilifatilia ya kwangu kweli nilibain kuwa inatoa moshi japo sio mwingi sana, nilivyobadili injin hata nikichomoa dip stk ile hali siioni tena, ebujaribu kufanja tafit kwenye injin nyingine mkuu ili ujiridhishe zaid.
Sawa mkuu...hili jambo lina mkanganyiko sana...gari yako ni ya petrol?
 
Mkuu kwa gar hiz za toyoyota hali hyo mara nying hutokea ring piston zikiwa zimechoka, nasema hv kwa kuwa hata mm kuna siku nifanya hvyo nikaona oil inatoka kama mvuke hv nikashangaa...ikabidi niangalie gari nyingine yenye injin kma yangu na ni mpya zaid ya yakwangu, kiukweli gar ikiwa vizur ukichomoa dip stick haifanyi hvyo, kama huamini tafuta gari ambayo haitoi moshi halafu chomoa dip stk utaona, mm nilifatilia ya kwangu kweli nilibain kuwa inatoa moshi japo sio mwingi sana, nilivyobadili injin hata nikichomoa dip stk ile hali siioni tena, ebujaribu kufanja tafit kwenye injin nyingine mkuu ili ujiridhishe zaid.

Sawa mkuu...hili jambo lina mkanganyiko sana...gari yako ni ya petrol?

Oil kusplash kwenye tundu la dipstick haisababishwi na piston rings, ila kweli iwapo unaona moshi ndio unatoka kwenye tundu hilo basi hapo ndipo unaweza kuhofia piston rings kwamba zinaruhusu moshi kuingia kwenye crankcase badala ya kwenda kwenye exhaust. Na ikitokea hali hiyo, moshi huo huanza kujitokeza pole pole hata bila kufunua dip stick, na vile vile injini huanza kusihiwa nguvu kupanda milimani.

Kama huoni moshi kwenye tundu hilo, usihanganike kabisa na piston rings. Sababu pekee inayoweza kuingia kichwani mwangu mara moja ni kuwa inawezekana ventilation valve inayoingiza hewa kwenye crankcase imeziba kwa hiyo ndani kuna vacuum inayosababisha mafuta yavutwe nje kwenye sehemu yoyote iliyofunguka. Valve hii unaweza kuibadilisha mwenyewe kwa kama dola 3 tu; inaitwa Postive Crankcase Ventilation (PCV).

For me lazima oil irukeruke kwakua pump inafanya kazi vizuri...
Hapana oil pump husukuma oli hiyo kwenye injini, dip stick inakwenda kwenye oil tank. Hiyo inayoruka nje ni kwa sababu inagongwa na crankshaft wakati injini inaunguruma. Kama ndani ya tank pressure ni ndogo basi matone yale yanaweza kuruka hadi nje ya tundu la dipstick.
 
Back
Top Bottom