Nitumie mbinu ganii ili niweze kufanikisha kuwasaidia Wanafunzi wanaosahau haraka?

TEMBO WANGU

JF-Expert Member
Feb 21, 2014
927
1,274
Habari za muda huu,

Kwa sasa nipo darasani nafundisha shule za awali, hapa darasani kuna wanafunzi kama wawili, yaani nimetumia mbinu zote za ualimu ili hawa watoto waweze kukumbuka masomo darasani, yaani unamfundisha leo, kesho akija amesahau.

Kuchapa sio njia mbadala ya yet kuelewa japo nimejitahidi kuchapa, lakini sikupata mafanikio.

Je, walimu na wanataaluma kwa ujumla nitumie mbinu ganii ili niweze kufanikisha kuwasaidia hawa watoto wetu? Naamini nitapata msaada kutoka kwenu.

Asanteni
 
Mkuu kwanza hongera kwakuelimisha taifa

Ili niweze changia nihibu swali hili

Unafundisha hizi shule za akina "JUNIA" au akina "MWAJUMA"
 
Habari za muda huu,

Kwa sasa nipo darasani nafundisha shule za awali, hapa darasani kuna wanafunzi kama wawili, yaani nimetumia mbinu zote za ualimu ili hawa watoto waweze kukumbuka masomo darasani, yaani unamfundisha leo, kesho akija amesahau.

Kuchapa sio njia mbadala ya yet kuelewa japo nimejitahidi kuchapa, lakini sikupata mafanikio.

Je, walimu na wanataaluma kwa ujumla nitumie mbinu ganii ili niweze kufanikisha kuwasaidia hawa watoto wetu? Naamini nitapata msaada kutoka kwenu.

Asanteni


Kama ni shule awali kaa na wazazi... mfumo wa maisha yao huko wanakoishi ndo chanzo trust me.. jaribu kuwahoji mwenendo wa wa maisha ya kila siku na pia ongea na walez wao. Kuna vitu ambavyo vinateka akili zao mara wanapotoka hapo shule
 
Aisee inaoneka kuchapa kwako huwa unagusa ... wapeleke kwa Chalamila wa Mbeya hawatasahau tena
 
Habari za muda huu,

Kwa sasa nipo darasani nafundisha shule za awali, hapa darasani kuna wanafunzi kama wawili, yaani nimetumia mbinu zote za ualimu ili hawa watoto waweze kukumbuka masomo darasani, yaani unamfundisha leo, kesho akija amesahau.

Kuchapa sio njia mbadala ya yet kuelewa japo nimejitahidi kuchapa, lakini sikupata mafanikio.

Je, walimu na wanataaluma kwa ujumla nitumie mbinu ganii ili niweze kufanikisha kuwasaidia hawa watoto wetu? Naamini nitapata msaada kutoka kwenu.

Asanteni

"IF you Hear, you forget. If you see, you remember. But, if you do, you understand." -- msingi mkuu wa Elimu.

Inaonekana mbinu unazotumia ni za "IF you hear...". Maelezo meeeengi. Halafu unategemea baadaye watoto wa-regurgitate back to you kuthibitisha wameelewa. Ukijitahidi kidogo, ni kwa "IF you see..." Unachorachora tu mifano tuwili tutatu, na kuonyesha mfano ubaoni. Of course they will remember: "Mwalimu alionesha mfano darasani. Sijui alifanyaje?". Kwa mbinu zako za kuchapa darasani, 102.17% hutumii kipengele cha "IF you do...". Mwalimu yoyote anayetumia adhabu ya viboko kwenye matatizo ya kitaaluma, huyo ni muflisi.

Mtu yoyote asifundishe shule ya awali kabla ya kusoma
kitabu hiki mwanzo mpaka mwisho.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom