Farolito
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 11,634
- 26,372
Wakuu,
Kila kukicha tunashuhudia kuongezeka kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto wa kike na kiume hapa nchini.
Yale maeneo ambayo tulidhani ni salama zaidi kwao, nako tayari pameonesha kwamba kunaweza kujitokeza pia mambo haya ya ukatili. Sasa hivi si Kanisani/Msikitini, shuleni wala nyumbani pana usalama wa asilimia zote.
Tumeshuhudia Wachungaji, Masheikh, madereva wa mabasi ya shule (ma anko), walimu na hata baadhi ndugu wa karibu kabisa wakihusishwa na vitendo hivi viovu.
Kwahiyo kama mzazi huwezi kuwa maeneo hayo yote kumlinda mtoto wako, ni lazima atakuwa mikoni mwa hao niliowataja na hata ambao sijawataja kwa namna moja au nyingine hilo halikwepeki.
Kwa maneno mengine ni kwamba hapa lazima mtoto mwenyewe ajengwe au awezeshwe kujilinda yeye mwenyewe anapokuwa peke yake.
Hivyo kwa wale wazazi au wataalamu wa saikolojia za watoto naomba ushauri, nitumie maneno gani yanayofaa kuwatahadharisha watoto wa kike darasa la tatu na chekechea namna ya kujilinda na ukatili wa kijinsia maeneo mbalimbali kwa kadri ya uelewa wao ili wawe salama?
Ni muhimu kuchukua tahadhari kabla ya hatari, tusiache kuwaombea kwa Mungu awaepushe na maovu haya, lakini acha tufanye kadri ya uwezo wetu na Mungu atafanya yaliyobaki.
Karibuni kwa ushauri.
Kila kukicha tunashuhudia kuongezeka kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto wa kike na kiume hapa nchini.
Yale maeneo ambayo tulidhani ni salama zaidi kwao, nako tayari pameonesha kwamba kunaweza kujitokeza pia mambo haya ya ukatili. Sasa hivi si Kanisani/Msikitini, shuleni wala nyumbani pana usalama wa asilimia zote.
Tumeshuhudia Wachungaji, Masheikh, madereva wa mabasi ya shule (ma anko), walimu na hata baadhi ndugu wa karibu kabisa wakihusishwa na vitendo hivi viovu.
Kwahiyo kama mzazi huwezi kuwa maeneo hayo yote kumlinda mtoto wako, ni lazima atakuwa mikoni mwa hao niliowataja na hata ambao sijawataja kwa namna moja au nyingine hilo halikwepeki.
Kwa maneno mengine ni kwamba hapa lazima mtoto mwenyewe ajengwe au awezeshwe kujilinda yeye mwenyewe anapokuwa peke yake.
Hivyo kwa wale wazazi au wataalamu wa saikolojia za watoto naomba ushauri, nitumie maneno gani yanayofaa kuwatahadharisha watoto wa kike darasa la tatu na chekechea namna ya kujilinda na ukatili wa kijinsia maeneo mbalimbali kwa kadri ya uelewa wao ili wawe salama?
Ni muhimu kuchukua tahadhari kabla ya hatari, tusiache kuwaombea kwa Mungu awaepushe na maovu haya, lakini acha tufanye kadri ya uwezo wetu na Mungu atafanya yaliyobaki.
Karibuni kwa ushauri.