UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,708
Kwanza kabisa niwape pole wale wote waliosongwa na shida za dunia kiasi kwamba hawajui la kufanya zaidi ya kukodoa macho na kupiga miayo isiyojulikana itakwisha lini!
Pili,niwape pole wale wote ambao tangu mwaka huu unaanza mpaka sasa hawajui ni lipi la kufanya kwasababu hali si shwari mtaani.
Tatu,niwape pole vijana wote waliohitimu, shule na vyuo na bado wameendelea kuwa mizigo majumbani kwao huku wakiendelea kusimangwa usiku na mchana, Mungu atawasimamia.
Nne,niwape pole wale wote tuliojiwekea malengo tokea mwaka huu unaanza lakini mpaka sasa hata robo ya malengo hatujatimiza!.
Tano na mwisho,niwape pole wale wote wanao haso lakini maisha yameendelea kuwa kichwa ngumu huku wakitamani kufanya ushirikina ili yalegee! Msikate tamaa ndugu zangu,Mungu amewasikia vilio vyenu!
Namshukuru Mungu mwaka huu nilibahatika kwenda nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya kumuona jamaa fulani kwa shughuli za kibiashara, hapo kabla sikuwahi kabisa kufika nchini Kenya, hivyo nilikuwa nasikia na kusoma makala za watu mbalimbali wakitoa maoni yao kuhusu nchi ya Kenya katika nyanja mbalimbali.
Safari yangu ilianzia mkoani Dodoma na kujikuta nimepiga kambi ya masaa kadhaa wilayani Tarime pale kwenye mpaka wa Kenya na Tanzania yaani Sirari,ingawa wenzetu wao wanaita "Sirare",Sababu ya kuzuiliwa masaa kadhaa pale Sirari ilikuwa ni kwamba sikuwa na pasi ya kusafiria(passport),hivyo nilitakiwa nirudi mpaka Tarime mjini kwa mkuu wa wilaya(bomani)kwenye ofisi za uhamiaji ili nikate pasipoti ya muda ili niweze kuruhusiwa kusafiri.
Baada ya kufika pale Tarime kwenye ofisi za Uhamiaji niliwakuta vijana wenzangu wakiwa ofisini wakiendelea kuchapa kazi,ingawa pia kuna vijana niliwakuta wameshikiliwa pale ofisini ikisemekana walikuwa wametokea burundi na walikamatwa kwa kuwa hawakuwa na documents zilizowafanya kuingia Tanzania.
Wakati pia nikiwa hapo ofisini huku jamaa wakiendelea kunikamilishia pasipoti yangu ya muda,kuna dada mmoja (demu) ambaye alikuja na jamaa mmoja hivi alikuwa mweupe kama mpemba,yule demu baadae wale jamaa waliniambia ni mkenya na wanamfahamu sana pale ofisini kwasababu haikuwa mara ya kwanza yeye kukanyaga pale akiwa na wanaume kadhaa wa kadhaa,kuna jamaa aliniambia yule demu ni muuzaji wa Kambale (nadhani tunaelewa), yule demu kiukweli niwe mkweli alikuwa pisi ya kimataifa,kama ukiwa na uchu na unahamu na kambale wabichi,basi kununua kambale kwa bei ya milioni ilikuwa ni jambo la kawaida!
Kwasababu mimi ni mtu mzima, inavyoonekana ni kwamba, yule demu huwa ametegesha pale Tarime na nadhani madereva mbalimbali ikiwemo wa malori huwa wanapeana namba za yule kiumbe,hivyo ukifika tu hapo Tarime kama unazo namba zake basi unamcheki mnavuka boda mnaenda kufurahia Ugali "Sima" kwa kambale mkiwa upande wa pili.Kiukweli Mungu alimuumba vyema sana yule mwanamke na anazo nyama za kutosha,bastola ndiyo usiseme!!.
Basi nilipokamilishiwa pasipoti yangu niliondoka zangu hapo ofisini nikawaacha huyo demu na jamaa yake nao wakiendelea kukamilisha documents zao.
Nilirudi tena Sirari nikagongewa muhuri ili nipite zangu kuingia Kenya, mpaka nakamilisha process zote na kuingia Kenya ilikuwa yapata saa 11 jioni.
Nilipofika upande wa pili,niliamua kubadili fedha yetu ya Tanzania na kupata shilingi ya Kenya, hapo sasa nikiwa eneo la Isebania. Nilipanda gari ndogo zilizokuwa zinaelekea sehemu moja inaitwa Migori, ingawa nilipokuwa naelekea ni Kisumu,lakini mwenyeji wangu aliniambia nikalale Migori ili nipumzike.
Basi nilipanda gari ndogo aina ya Toyota Pro box ambavyo vilikuwa vingi sana hapo Isebania. Isebania ni sehemu ya County ya Migori.
Nikiwa ndani ya gari niliendelea kuishangaa Isebania ilivyonakishiwa na nyumba za zamani kando kando ya barabara, kiukweli hapo Isebania kiujumla hali haikuwa tofauti sana na kwetu upande wa Tarime maana hata wenyeji wa Isebania pia ni wakurya lakini wakurya wa Kenya.
Ilitichukua takribani saa 1 mpaka kufika Migori. Kiukweli baada ya kufika sasa Migori ndipo niliona hali ni tofauti kwasababu Mwanzo nikiwa Isebania hali ya hewa na mazingira hazikupishana sana na Tarime, lakini kuanzia hapo Migori na kuendelea hali ya hewa na Mazingira yalianza kubadilika na kuwa yakupendeza sana.
Nilienda kutafuta chumba cha kulala ambapo nililipa Ksh 1000,kiukweli wenzetu kwenye suala la Lodge,Guests House bado naona wako nyuma sana, na ninasema hivyo kwasababu kuanzia hapo Migori mpaka nilipoishia (nitasema huko mbele), bado rooms hazikuwa vyema, yaani Guests ni gharama lakini haziendani na thamani ya pesa, kuna mtu nilimuuliza akaniambia wakenya si watu wa kwenda Guest sana ndiyo maana huwa hawajali, lakini nikajiuliza kwanini wasiweke mazingira bora kwasababu ya wageni?
Jamaa akaniambia logde hizi za kawaida huwa si nzuri tofauti na zile za kitalii, sasa hiyo Ksh 1000 niliyolipa ambayo kwa Tanzania ni kama 22000/= kiukweli hata ukiamua kulala pale Dodoma unapata Guests house nzuri sana.
Nitarudi kuendelea
Pili,niwape pole wale wote ambao tangu mwaka huu unaanza mpaka sasa hawajui ni lipi la kufanya kwasababu hali si shwari mtaani.
Tatu,niwape pole vijana wote waliohitimu, shule na vyuo na bado wameendelea kuwa mizigo majumbani kwao huku wakiendelea kusimangwa usiku na mchana, Mungu atawasimamia.
Nne,niwape pole wale wote tuliojiwekea malengo tokea mwaka huu unaanza lakini mpaka sasa hata robo ya malengo hatujatimiza!.
Tano na mwisho,niwape pole wale wote wanao haso lakini maisha yameendelea kuwa kichwa ngumu huku wakitamani kufanya ushirikina ili yalegee! Msikate tamaa ndugu zangu,Mungu amewasikia vilio vyenu!
Namshukuru Mungu mwaka huu nilibahatika kwenda nchi jirani ya Kenya kwa ajili ya kumuona jamaa fulani kwa shughuli za kibiashara, hapo kabla sikuwahi kabisa kufika nchini Kenya, hivyo nilikuwa nasikia na kusoma makala za watu mbalimbali wakitoa maoni yao kuhusu nchi ya Kenya katika nyanja mbalimbali.
Safari yangu ilianzia mkoani Dodoma na kujikuta nimepiga kambi ya masaa kadhaa wilayani Tarime pale kwenye mpaka wa Kenya na Tanzania yaani Sirari,ingawa wenzetu wao wanaita "Sirare",Sababu ya kuzuiliwa masaa kadhaa pale Sirari ilikuwa ni kwamba sikuwa na pasi ya kusafiria(passport),hivyo nilitakiwa nirudi mpaka Tarime mjini kwa mkuu wa wilaya(bomani)kwenye ofisi za uhamiaji ili nikate pasipoti ya muda ili niweze kuruhusiwa kusafiri.
Baada ya kufika pale Tarime kwenye ofisi za Uhamiaji niliwakuta vijana wenzangu wakiwa ofisini wakiendelea kuchapa kazi,ingawa pia kuna vijana niliwakuta wameshikiliwa pale ofisini ikisemekana walikuwa wametokea burundi na walikamatwa kwa kuwa hawakuwa na documents zilizowafanya kuingia Tanzania.
Wakati pia nikiwa hapo ofisini huku jamaa wakiendelea kunikamilishia pasipoti yangu ya muda,kuna dada mmoja (demu) ambaye alikuja na jamaa mmoja hivi alikuwa mweupe kama mpemba,yule demu baadae wale jamaa waliniambia ni mkenya na wanamfahamu sana pale ofisini kwasababu haikuwa mara ya kwanza yeye kukanyaga pale akiwa na wanaume kadhaa wa kadhaa,kuna jamaa aliniambia yule demu ni muuzaji wa Kambale (nadhani tunaelewa), yule demu kiukweli niwe mkweli alikuwa pisi ya kimataifa,kama ukiwa na uchu na unahamu na kambale wabichi,basi kununua kambale kwa bei ya milioni ilikuwa ni jambo la kawaida!
Kwasababu mimi ni mtu mzima, inavyoonekana ni kwamba, yule demu huwa ametegesha pale Tarime na nadhani madereva mbalimbali ikiwemo wa malori huwa wanapeana namba za yule kiumbe,hivyo ukifika tu hapo Tarime kama unazo namba zake basi unamcheki mnavuka boda mnaenda kufurahia Ugali "Sima" kwa kambale mkiwa upande wa pili.Kiukweli Mungu alimuumba vyema sana yule mwanamke na anazo nyama za kutosha,bastola ndiyo usiseme!!.
Basi nilipokamilishiwa pasipoti yangu niliondoka zangu hapo ofisini nikawaacha huyo demu na jamaa yake nao wakiendelea kukamilisha documents zao.
Nilirudi tena Sirari nikagongewa muhuri ili nipite zangu kuingia Kenya, mpaka nakamilisha process zote na kuingia Kenya ilikuwa yapata saa 11 jioni.
Nilipofika upande wa pili,niliamua kubadili fedha yetu ya Tanzania na kupata shilingi ya Kenya, hapo sasa nikiwa eneo la Isebania. Nilipanda gari ndogo zilizokuwa zinaelekea sehemu moja inaitwa Migori, ingawa nilipokuwa naelekea ni Kisumu,lakini mwenyeji wangu aliniambia nikalale Migori ili nipumzike.
Basi nilipanda gari ndogo aina ya Toyota Pro box ambavyo vilikuwa vingi sana hapo Isebania. Isebania ni sehemu ya County ya Migori.
Nikiwa ndani ya gari niliendelea kuishangaa Isebania ilivyonakishiwa na nyumba za zamani kando kando ya barabara, kiukweli hapo Isebania kiujumla hali haikuwa tofauti sana na kwetu upande wa Tarime maana hata wenyeji wa Isebania pia ni wakurya lakini wakurya wa Kenya.
Ilitichukua takribani saa 1 mpaka kufika Migori. Kiukweli baada ya kufika sasa Migori ndipo niliona hali ni tofauti kwasababu Mwanzo nikiwa Isebania hali ya hewa na mazingira hazikupishana sana na Tarime, lakini kuanzia hapo Migori na kuendelea hali ya hewa na Mazingira yalianza kubadilika na kuwa yakupendeza sana.
Nilienda kutafuta chumba cha kulala ambapo nililipa Ksh 1000,kiukweli wenzetu kwenye suala la Lodge,Guests House bado naona wako nyuma sana, na ninasema hivyo kwasababu kuanzia hapo Migori mpaka nilipoishia (nitasema huko mbele), bado rooms hazikuwa vyema, yaani Guests ni gharama lakini haziendani na thamani ya pesa, kuna mtu nilimuuliza akaniambia wakenya si watu wa kwenda Guest sana ndiyo maana huwa hawajali, lakini nikajiuliza kwanini wasiweke mazingira bora kwasababu ya wageni?
Jamaa akaniambia logde hizi za kawaida huwa si nzuri tofauti na zile za kitalii, sasa hiyo Ksh 1000 niliyolipa ambayo kwa Tanzania ni kama 22000/= kiukweli hata ukiamua kulala pale Dodoma unapata Guests house nzuri sana.
Nitarudi kuendelea