Nitaongoza mgomo wa vijana wa CCM nchi nzima

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga. akizungumza na Vijana wa CCM.
Vijana wa CCM tunataka maelezo ya kina juu ya waliotusaliti wakati mgumu wa kampeni kwa kuama chama? eti sasa wanarudi, ILI iweje?

Chama hiki si cha mtu, eeh kama katiba na kanuni tubadili tu, jambo la kupokelewa watu hawa liamuliwe na vikao vikubwa si Kata ama Wilaya tu, watu wakipewa Milioni.

KWANINI MNASAHAU MACHOZI YA WAPAMBANAJI HASA VIJANA MAPEMA HIVI? AMA KWAKUWA SISI TUMESHAPATA VYEO?

MTAKUJA KUTUONA WATUKUTU NA JEURI SASA HIVI.

Eti Mteketa karudi!
Nasikia yupo Waziri Mkuu Mstaafu anatakakurudi!
Nasikia Mzee Ngombale anataka kurudi!
Nasikia Mzee Msindai,Mgeja na Guninita wanarudi!

NITAONGOZA MGOMO WA VIJANA HAMASA WA CCM NCHI NZIMA endapo wasaliti wanarudi bila vijana kupewa maelezo ya kina na kushirikishwa, Haikubaliki.

Ehh Maana watu watasaliti tu wakijuwa wakirudi kwa kutoa Milioni moja watapokelewa.

TUACHE BESENGA HAMKAWII KUSEMA SISI WATUKUTU NA JEURI. Maana hakuna namna.

Chanzo: UVCCM Taifa
 
Wapo wengi wanataka kurudi
Hawana hamu walicho kikuta kule

Wali Ruka Mkojo na kukanyaga kinyesi
Waone eni huruma
Mkitoa msimamo Wa hivyo watakufa muda bado
Kule walipotea
 
Mpaka siku Tanzania itakapoachana na itikadi za vyama ndo mtaona maendeleo, zaid ya hapo mtasubiri sana sababu hamna maarifa na mnaendelea kuwaaminisha watu wenu kwenye vyama.
 
Sina chama ni shabiki tu ila hawa wasaliti waangaliwe kwa jicho la pili sio kurudi kienyeji hivi kwa kuvaa kishati cha kijani na njano basi walitoka kwa mbwembwe na dharau Leo wanarudi wamesahau nini?
 
Roho ya usaliti iliumbiwa ccm. Sioni sababu ya mnaojipambanua kuwa ccm ni yenu kutokwa na mapovu ilihali huijui ccm kwa kina. Enzi zile tulilazimishwa kuwa wanachama na tulikuwa hatuijui siasa na tuliponitambua tulivitupilia mbali vikadi vyenu tukabaki bila chama. Asenga tafuta shughuli kwani hao wanaorudi watakupiga zengwe hadi ukimbie kwani mbinu zao tu ni silaha tena za maangamizi. Sijui umejipangaje? Waweza mshirikisha alhadji Bulembo kwa mbinu zake za kuuchuna. Hasikiki tena zaidi ya kualikwa kwenye chai party hapo magogoni.
 
Huyu dogo yeye ni nani CCM?ha ha atakula matapishi yake!time will tell
 
Mpaka siku Tanzania itakapoachana na itikadi za vyama ndo mtaona maendeleo, zaid ya hapo mtasubiri sana sababu hamna maarifa na mnaendelea kuwaaminisha watu wenu kwenye vyama.
Vyama vingi vimekuja ya miaka ya tisini, je kabla ya hapo maendeleo yalikuwepo!? Au baada ya vyama vingi umasikini umezidi?
Hii hatua ya huyu kijana ni kielelezo tosha kwamba mchezo uliofanyika Dodoma wakati wa kumpata mgombea kwa mwenyekiti kuja na majina mfukoni kama baadhi ya wagombea walivyodai matokeo yake daima hayatakiacha chama salama. Tuwe wakweli, zaidi ya 95% ya wanaccm na hata wajumbe wa mkutano wenyewe hawakutegemea kama leo hii JPM angetinga Magogoni. Cha msingi kaeni muisome namba.
 
Wapo wengi wanataka kurudi
Hawana hamu walicho kikuta kule

Wali Ruka Mkojo na kukanyaga kinyesi
Waone eni huruma
Mkitoa msimamo Wa hivyo watakufa muda bado
Kule walipotea
Warudi tu kundini' walizania wakija huku itakuwa business as usual,huku kugumu watu wapo tayari kupigwa virungu,kukamatwa usiku wa Saa Saba,kukodiwa ndege na pamoja na ulinzi wa Hali ya juju..alafu kuhojiwa masaa matatu then kuachiliwa.
Huku hakuna mshiko wa bure,kunyenyekewa kama Miungu mtu .huku ni ukakamavu kwenda bure.
 
Huyu Asenga si ndio aligaragazwa na Peter Lijualikali kwenye kinyanganyiro cha ubunge jimbo la kilombero? Hana jipya ni wakupuuzwa tu. Alipataje hiyo nafasi huko uvccm?
 
Huyu Asenga si ndio aligaragazwa na Peter Lijualikali kwenye kinyanganyiro cha ubunge jimbo la kilombero? Hana jipya ni wakupuuzwa tu. Alipataje hiyo nafasi huko uvccm?
wew umepataje nafasi ya kupiga umbea , jamaa yuko sahihi
na ni wakuungwa mkono
 
Chanzo: UVCCM Taifa

Mdogo sana katika siasa za Tanzania hasa ndani ya CCM.

Wewe ni nani hata unahoji suala hili!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Angalia utakuja tolewa meno bila ganzi ushindwe kutafuna mahindi ya kuchoma ya kuchanganya ndimu na pilipili unga!!!!!!

Wenyewe wameamua kaa kimya wewe ni nani????

Eti unajiita ni Kaimu Katibu Idara ya Hamasa, Sera, Utafiti na Mawasiliano UVCCM TAIFA, Ndugu Abubakar D. Asenga.

profilepic 2015.JPG
 
Yeye mwenyewe kasema chama hiki si cha mtu. Sasa kwanini awe na kinyongo na wanaorudi hadi aongoze maandamano?
Ila naye masikio pamoja na uzoefu wa serikali kweli aliamini wangechukua madaraka? Alikuwa kwenye coma nini?
 
Back
Top Bottom