Nitaoa mwanamke asiye na kazi

Naona mleta mada anajadili jambo gumu, wakati hata kumbe hajaoa....teh
Hapa ni sawa na kuchoma battery ya gari la mafuta lililo anguka...teh
 
Ubinafsi ndio unaotusumbua wanaume. Kama mkeo hukumkuta na bikra ni wazi huyo alishakuwa 'used'. Na hata akitumika na mtu mwingine bado hicho kibox hakitabadilika rangi. Tujifunze kuwapenda wanawake na udhaifu wao. Ukijitoa kwa mwanamke kimwili na roho utateseka sana. Mwanamke hachungwi, anajichunga mwenyewe kutokana jinsi wewe unavyoishi nae. Ukimpenda nae atakupenda. Ukimthamini nae anakuthamini. Mungu alituagiza tuishi nao kwa kutumia akili, maana anazijua akili zao zilivyo.
Kunywa soda kwa mangi
 
Hakuna...labda upande wa mwanamke wawe na uwezo wamsaidie
Waishi vizuri kwa kipato kipi?.
Wengi huwa hawajui kutafuta ..kazi kupata pia ni issue ht km ana elimu
Mix ndugu wamnyanganye mali
Lazma watoto warudi kayumba na arudi kijijini
Kukaanga maandazi unajua kipato chake ni sh elf 10 kwa siku/laki 3 kwa mwezi..u can imagine

Kwa hiyo unakomaa kuniaminisha kwamba hakuna kabisa wanawake wajane magolikipa waliofanikiwa kulea watoto wao bila msaada wowote kutoka kwa ndugu?

acha kufanya assumptions za ajabu wewe! wapo sana tu tena wengine ni majirani zangu. Kuna father mmoja muislamu alifariki mimi nikiwa bado ni teenager aliacha wajane wawili na wote aliwahi anawahudumia yeye.

Leo hii tunavyoandika hapa watoto aliwaacha wako makazini na walisoma hivyo hivyo kwa shida shida.

Hizo kazi za kukaanga mihogo/maandazi zinazoingiza 10k kwa siku, wapo watu wanaendesha maisha yao kwa hivyo hivyo vipato unavyoiona kwako ni duni. Wanakula,wanavaa na wanasomesha.

Mwanamke yeyote akishajijua kwamba ana mzigo wa watoto hata kama alikuwa ajuhi fuma vitambaa! atajua mpaka bei ya cabbage bustanini ni shilling ngapi ili aweze kufanya biashara.

kwani unafikiri ni kwanini watu huwa wanawasifiaga single mothers humu jamvini?
 
Hayo mambo ya ujentoman ya kupitiana kazini nimemaachia wenye mioyo migumu kama jiwe. Ujentoman wangu mwenye moyo laini kama pamba... nimefanya tu busara ya kumzawadia kaPasso apambane na hali yake... Sipendagi ujinga mimi
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 hahahah hapo umemuweza sasa.
 
Kwa hiyo unakomaa kuniaminisha kwamba hakuna kabisa wanawake wajane magolikipa waliofanikiwa kulea watoto wao bila msaada wowote kutoka kwa ndugu?

acha kufanya assumptions za ajabu wewe! wapo sana tu tena wengine ni majirani zangu. Kuna father mmoja muislamu alifariki mimi nikiwa bado ni teenager aliacha wajane wawili na wote aliwahi anawahudumia yeye.

Leo hii tunavyoandika hapa watoto aliwaacha wako makazini na walisoma hivyo hivyo kwa shida shida.

Hizo kazi za kukaanga mihogo/maandazi zinazoingiza 10k kwa siku, wapo watu wanaendesha maisha yao kwa hivyo hivyo vipato unavyoiona kwako ni duni. Wanakula,wanavaa na wanasomesha.

Mwanamke yeyote akishajijua kwamba ana mzigo wa watoto hata kama alikuwa ajuhi fuma vitambaa! atajua mpaka bei ya cabbage bustanini ni shilling ngapi ili aweze kufanya biashara.

kwani unafikiri ni kwanini watu huwa wanawasifiaga single mothers humu jamvini?
Basi sawa kwa kua unaridhia maisha duni ya familia yako kipindi haupo
Umaskini si kitu kizuri
 
Kuna mambo mengine ukisikia unajihisi kichefu chefu maana mtu anataka kuingia kwenye ndoa na kitu chake kichwani kwamba wanawake wako hivi na wengine wako vile, tena kwa negative thinking na matokeo yake badala ya kumshape unavyopenda kuishi nae, wewe utakuwa unapima tabia yake na makosa yake na kisha kuweza kutumia Akili yako mbovu ulioingia nayo kwenye ndoa, ukichanganya na upofu wa kutokujua ndoa ni nini basi hasira yako na mengineyo unachanganya na kisha kutoa hukumu. Kwa mantiki hii ndoa huiwez brother. Ila ndoa ina mambo yafuatayo :-
1: chukua Muda mrefu kumchunguza mwanamke na kujua kama mnaendana au la. Suala la kupewa style nyingi za ngono au kungonoka kila siku sio kigezo cha ndoa. Ukikaa na mwanamke walau miaka 4 kabla ya kumuoa mnaweza kuwa na kitu flani in common.
2: maisha yako yawe ya kawaida na si kujikweza akija demu wako, mwisho wa siku akijua kuwa ulikuwa unakodi magari kumtoa out sehemu zenye hela, umekwisha. Hata ukijifanya kuwa wewe una hela kwa mwanamke ni kosa sana.
3: oa mwanamke ambae hana majivuno, asiependa pesa, wala kuweka ngono mbele. Hata wewe pia maana kuna wengine wanaume wanasema akija demu basi anataka kupiga bao 5 kwa siku, my friend, ukioa hayo yanaisha, mwisho wa siku ni bao moja tu tena kwa siku kadhaa, hata baada ya siku 4-5. Kama ulimzoesha mwanamke hivyo basi utasaidiwa. Kadri umri na kugonga sana kunapunguza shughuli hy ya mambo yetu. Kila kitu kina Muda wake.
4: angalia mwanamke alikuwa anafanya nini kabla na anawez kujishughulisha na nini na uweze kumsapoti maana zipo siku unaweza kufukuzwa kazi, mambo yakabana sana, hata kuingia majaribuni na ukashikiliwa hata siku 7 polisi, kama mke hana cha kufanya na ulimuachia buku 5, si ndo mwanzo wa kugongwa ili apate mahitaji yake?.
5: usioe mke kisa ni mzuri, uzuri unaweza kuisha au akawa anatumia mkorogo.
Mmmmh! Aisee ndugu una muda gani kwenye ndoa yako? Mbona umeongea vitu vya msingi na vizito namna hii? Mpaka nimekaa kurudirudia kusoma ulichoandika? Maneno yako si ya vijana kama mimi hapa ambao bado tunaparamia wanawake ovyo kwa kuangalia external factors, Hongera sana kwa kupata busara hiyo.
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom