rifwima
JF-Expert Member
- Apr 21, 2010
- 507
- 212
Wan JF, Mimi ni kijana mwenye umri wa kutosha tu, karibia miaka 30 kasoro 1. Kila kona, kila siku, kila mara stakeholders wananiuliza "unaoa lini?". Nimechoshwa na hili swali kwani kwa sasa chini ya utawala wa MAGAMBA sioni nafuu ya maisha kujipa majukumu ya ndoa. Jawabu langu kwa sasa kwa kila anaeniuliza hilo swali ni "NITAOA 2015, LAKINI with one strong useful condition, MPAKA CHADEMA ICHUKUE NCHI". Wadau nisaidieni kuwahimiza ndugu, jamaa na marafiki wajiandikishe na wawe tayari kukipigia CHADEMA 2015 ili kijana mwenzenu nipata JIKO...SABABU HICHO NDO KIAPO CHANGU. Nawasilisha.