Nitamuita Shujaa wa Taifa Mbunge yeyote atakayependekeza kodi kwa Wabunge

View attachment 1822510

View attachment 1822511

1. Mpango wa kupinga tofauti kubwa ya kipato baina ya wabunge na watumishi wa serikali (hasa walimu, madaktari na wanajeshi) utaanza kwa kusambaza jumbe, picha na video, ili kuwajulisha watumishi husika juu ya tofauti iliopo. Nitaandaa jumbe hizo kwa lugha inayotafakarisha.

2. Ifahamike, ninapinga ni utofauti wa kipato baina ya wabunge na watumishi kwa sababu malipo yao yanatokana na kodi za watanzania. Wenye mamlaka waamue kupunguza utofauti huu kwa kushusha malipo ya wabunge au kuwaongezea watumishi wengine. Wataaua wenye maamuzi. Lakini tofauti iliyopo sasa haikubaliki.

3. Sambamba na kusambaza jumbe hizo, nitaandaa 'online petition' kwa watu wote wanaoguswa waweze kutia saini. Pia nitaandika barua (nakala ngumu) kwenda kwa waziri mkuu ambaye ndo kiongozi wa shughuli za serikali bungeni kueleza jambo hili.

4. Kabla ya kuifikisha barua kwa w/mkuu, nitaisambaza kokote ninapoweza ili watumishi husika watie sahihi zao.
Hili ni zoezi endelevu lisolokoma (Continuous & endless). Mbinu ya mwisho itakuwa ni kuitisha mgomo wa watumishi kupinga tofauti hii kubwa ya mgawanyo wa kodi za watanzania.Hakuna sababu zozote za msingi za utofauti mkubwa wa malipo ya wabunge na watumishi wengine yanayotokana na kodi za wananchi. Katika nchi zinazojitambua, hili jambo halipo.


5. Nakaribisha maoni. Nitapokea yale yatakayosaidia mpango huu na kupuuza yale ya kukwamisha.
Watu wa video graphics, cartoonists na yyt anayeona anaweza kufanya kazi hii (overtly or covertly), anicheki kwa 0713933736 (whatssap and sms tu).
Anza na kodi mshahara wa Rais kwanza awe mfano
 
Wabunge ilitakiwa wakatwe kati ya 20% to 25% kwa kila mapato yao.

Kwa namna hii wangekuwa na feeling ya what it take ku-earn then kabla fedha haijaungia mfukoni, TRA inakata kutoka kwenye pay yao.

Otherwise tuna watu ambao hawana hisia za nini wafanyakazi wa nchi hii wanapitia.
Unajua hawa wabunge ni watu wa hovyo sana! Wanadhani huku mitaani kuna watu wasiowajua kabisaaa! Hili ni kundi lenye ubinafsi na upuuzi. Hawalipi kodi inayostahili halafu wanajidai kueleza umuhimu wa kulipa kodi.
 
Anza na kodi mshahara wa Rais kwanza awe mfano

Rais mara nyingi wana posho ,rais hata akipewa elfu 45 kwa mwezi hatoi hata 100 kujihudumia ,mahitaji yote yapo kwenye bajeti ya ikulu ambayo ni zaidi ya 900 bilioni kwa mwaka.
 
Swali mbona mshahara wake haukatwi kodi?

Kwani mshahara wake analipwa na nani? Maana nachojua ikulu ndio rais chochote anachotaka rais kinatekelezwa! Je bajeti ya ikulu inapelekwa wapi? Accounts za ikulu nani mwenye control DGIS au Sponsor?
 
Kila baada ya miaka mitano anakula milioni 300 kiinua mgongo hapo hujaweka maslahi mengine, ndiomaana wanakuwa mazuzu ilimradi tu hela yake aipate pindi muda wake unapoisha , yani ilitakiwa kama nchi zingine huko zilizoendelea kama mtu sio tajiri hakuna kuwa mbunge period, sio hawa wakwetu ambao ubunge ndio ajira
 
Hatmaye, shujaa niliyekuwa namtafuta amepatikana. Ni Mbunge Jerry Slaa ....!!

Kwa habari zaidi fungua link hapo chini.

1627043898634.png
 
Kwa kweli wananchi wa Tanzania hasa wafanyakazi wa serikali wamesota sana kwa miaka 6 iliyopita. Kuiishi miaka yote hiyo bila kuongezewa mshahara wakati ghalama za maisha zikiendelea kupanda kwa kweli siyo mchezo.

Hapa lazima tuwapongeze hawa wafanyakazi. ingekuwa nchi za wenzetu has kama za ndugu zetu kule Bondeni naamini kabisa wangeitisha Kunji za kufa mtu. Thanks God, this is Bongoland!

Straight to the point. Naona Wabunge wetu safari hii wamekuja na mapendekezo ya Uzalendo pamoja na ile kodi ya kidogo iliyoitwa na Mh. Zungu kuwa ni ya Uzalendo, ile ya makato ya siku kila uki-recharge voucher. Ni wazo zuri, ila kwa nini hatokei Mbunge mmoja akapendekeza makato kwenye mishahara na marupurupu yao manono. Mimi nitamuita SHUJAA WA TANZANIA.

Kwanini miaka yote hii hatokei walau Chizi moja tu humo mjengoni akaja na wazo hili; kila moja wetu anajua kuwa halitakubaliwa lakini litampa ushujaa mleta hoja.
Amepatikana shujaa na avikwe taji la Mbunge wa kitaifa

 
Back
Top Bottom